< John 1 >

1 In the beginning was the Word, and the Word was with God, and the Word was God.
Mwanzoni kulikuwako Neno, na Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa Mungu.
2 The same was in the beginning with God.
Huyu, Neno, Mwanzoni alikuwa pamoja na Mungu.
3 All things were made by him; and without him was not any thing made that was made.
Vitu vyote vilifanyika kupitia yeye, na pasipo yeye hakuna hata kitu kimoja kilichokuwa kimefanyika.
4 In him was life; and the life was the light of men.
Ndani yake kulikuwa uzima, na huo uzima ulikuwa nuru ya wanadamu wote.
5 And the light shineth in darkness; and the darkness comprehended it not.
Nuru yang'aa gizani, wala giza halikuizimisha.
6 There was a man sent from God, whose name was John.
Palikuwa na mtu aliyetumwa kutoka kwa Mungu, ambaye jina lake alikuwa Yohana.
7 The same came for a witness, to bear witness of the Light, that all men through him might believe.
Alikuja kama shahidi kushuhudia kuhusu ile nuru, ili kwamba wote waweze kuamini kupitia yeye.
8 He was not that Light, but was sent to bear witness of that Light.
Yohana hakuwa ile nuru, bali alikuja ili ashuhudie kuhusu ile nuru
9 That was the true Light, which lighteth every man that cometh into the world.
Hiyo ilikuwa nuru ya kweli ambayo ilikuwa inakuja katika dunia nayo humtia nuru kila mmoja
10 He was in the world, and the world was made by him, and the world knew him not.
Alikuwa katika dunia, na dunia iliumbwa kupitia yeye, na dunia haikumjua.
11 He came unto his own, and his own received him not.
Alikuja kwa vitu vyake, na watu wake hawakumpokea.
12 But as many as accepted him, to them gave he power to become the sons of God, even to them that believe on his name:
Bali kwa wale wengi waliompokea, ambao waliamini jina lake, kwa hao aliwapa haki ya kuwa wana wa Mungu,
13 Which were born, not of blood, nor of the will of the flesh, nor of the will of man, but of God.
Ambao walizaliwa, sio kwa damu, wala kwa mapenzi ya mwili, wala kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu mwenyewe.
14 And the Word was made flesh, and dwelt among us, ( and we beheld his glory, the glory as of the only begotten of the Father, ) full of grace and truth.
Naye Neno alifanyika mwili na akaishi miongoni mwetu, tumeuona utukufu wake, utukufu kama wa mtu pekee wa kipekee aliyekuja kutoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.
15 John bare witness of him, and cried, saying, This was he of whom I spake, He that cometh after me is preferred before me: for he was before me.
Yohana alishuhudia kuhusu yeye, na alipaza sauti akisema, “Huyu ndiye ambaye nilisema habari zake nikisema, “Yule ajaye baada yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa sababu amekuwako kabla yangu.”
16 And of his fulness have all we received, and grace for grace.
Kwa kuwa kutoka katika utimilifu wake, sisi sote tumepokea bure kipawa baada ya kipawa.
17 For the law was given by Moses, but grace and truth came by Jesus Christ.
Kwa kuwa sheria ililetwa kupitia Musa. Neema na kweli vilikuja kupitia Yesu Kristo.
18 No man hath seen God at any time; the only begotten Son, which is in the bosom of the Father, he hath declared him.
Hakuna mwanadamu aliyemwona Mungu wakati wowote. Mtu pekee ambaye ni Mungu, aliye katika kifua cha Baba, amemfanya yeye ajulikane.
19 And this is the record of John, when the Jews sent priests and Levites from Jerusalem to ask him, Who art thou?
Na huu ndio ushuhuda wa Yohana wakati makuhani na walawi waliotumwa kwake na Wayahudi kumwuliza, “Wewe ni nani?”
20 And he confessed, and denied not; but confessed, I am not the Christ.
Bila kusitasita na hakukana, bali alijibu, “Mimi sio Kristo.”
21 And they asked him, What then? Art thou Elijah? And he saith, I am not. Art thou that prophet? And he answered, No.
Hivyo wakamuuliza, “kwa hiyo wewe ni nani sasa?” Wewe ni Eliya? Akasema, “Mimi siye.” Wakasema, Wewe ni nabii? Akajibu,” Hapana.”
22 Then said they unto him, Who art thou? that we may give an answer to them that sent us. What sayest thou of thyself?
Kisha wakamwambia, “Wewe ni nani, ili kwamba tuwape jibu waliotutuma”? Wajishuhudiaje wewe mwenyewe?”
23 He said, I am the voice of one crying in the wilderness, Make straight the way of the Lord, as said the prophet Isaiah.
Akasema, “Mimi ni sauti yake aliaye nyikani: 'Inyosheni njia ya Bwana,' kama nabii Isaya alivyosema.”
24 And they which were sent were of the Pharisees.
Basi kulikuwa na watu wametumwa pale kutoka kwa Mafarisayo. Wakamuuliza na kusema,
25 And they asked him, and said unto him, Why baptizest thou then, if thou be not that Christ, nor Elijah, neither that prophet?
“Kwa nini unabatiza basi kama wewe sio Kristo wala Eliya wala nabii?”
26 John answered them, saying, I baptize with water: but there standeth one among you, whom ye know not;
Yohana aliwajibu akisema, “Ninabatiza kwa maji. Hata hivyo, miongoni mwenu anasimama mtu msiyemtambua.
27 He it is, who coming after me is preferred before me, whose shoe’s latchet I am not worthy to unloose.
Huyu ndiye ajaye baada yangu. Mimi sisitahili kulegeza kamba za viatu vyake.”
28 These things were done in Bethabara beyond Jordan, where John was baptizing.
Mambo haya yalitendeka huko Bethania, ng'ambo ya Yordani, mahali ambapo Yohana alikuwa akibatiza.
29 The next day John seeth Jesus coming unto him, and saith, Behold the Lamb of God, which taketh away the sin of the world.
Siku iliyofuata Yohana alimwona Yesu akija kwake akasema, “Tazama mwanakondoo wa Mungu aichukuae dhambi ya ulimwengu!
30 This is he of whom I said, After me cometh a man which is preferred before me: for he was before me.
huyu ndiye niliyesema habari zake nikisema, “Yeye ajaye nyuma yangu ni mkuu kuliko mimi, kwa kuwa alikuwa kabla yangu.'
31 And I knew him not: but that he should be made manifest to Israel, therefore am I come baptizing with water.
Sikumtambua yeye, lakini ilifanyika hivyo ili kwamba afunuliwe katika Israeli, kwamba nilikuja nikibatiza kwa maji.”
32 And John bare record, saying, I saw the Spirit descending from heaven like a dove, and it abode upon him.
Yohana alishuhudia, “Niliona Roho akishuka kutoka mbinguni mfano wa hua, na ilibaki juu yake.
33 And I knew him not: but he that sent me to baptize with water, the same said unto me, Upon whom thou shalt see the Spirit descending, and remaining on him, the same is he which baptizeth with the Holy Ghost.
Mimi sikumtambua lakini yeye aliyenituma ili nibatize kwa maji aliniambia, 'yule ambaye utaona Roho akishuka na kukaa juu yake, Huyo ndiye abatizaye kwa Roho Mtakatifu.'
34 And I saw, and bare record that this is the Son of God.
Nimeona na nimeshuhudia kwamba huyu ni Mwana wa Mungu.”
35 Again the next day after John stood, and two of his disciples;
Tena siku iliyofuata Yohana alikuwa amesimama pamoja na wanafunzi wake wawili,
36 And looking upon Jesus as he walked, he saith, Behold the Lamb of God!
walimwona Yesu akitembea na Yohana akasema, “Tazama, Mwana kondoo wa Mungu!”
37 And the two disciples heard him speak, and they followed Jesus.
Wanafunzi wawili walimsikia Yohana akisema haya wakamfuata Yesu.
38 Then Jesus turned, and saw them following, and saith unto them, What seek ye? They said unto him, Rabbi, ( which is to say, being interpreted, Master, ) where dwellest thou?
Tena Yesu aligeuka na kuwaona wanafunzi wale wakimfuata, na akawambia, “Mnataka nini?” Wakajibu, “Rabbi, (maana yake 'mwalimu,' unaishi wapi?”
39 He saith unto them, Come and see. They came and saw where he dwelt, and abode with him that day: for it was about the tenth hour.
Akawambia, “Njooni na mwone.”Kisha walikwenda na kuona mahali alipokuwa akiishi; walikaa pamoja naye siku hiyo, kwa kuwa ilikuwa yapata kama saa kumi hivi.
40 One of the two which heard John speak, and followed him, was Andrew, Simon Peter’s brother.
Mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana akiongea na kisha kumfuata Yesu alikuwa ni Andrea, ndugu yake Simoni Petro.
41 He first findeth his own brother Simon, and saith unto him, We have found the Messiah, which is, being interpreted, the Christ.
Akamwona ndugu yake Simoni na akamwambia, “Tumempata Masihi” (ambayo inatafsiriwa Kristo).
42 And he brought him to Jesus. And when Jesus beheld him, he said, Thou art Simon the son of Jonah: thou shalt be called Cephas, which is by interpretation, A stone.
Akamleta kwa Yesu. Yesu akamtazama na akasema, “Wewe ni Simoni mwana wa Yohana” utaitwa Kefa,” (maana yake 'Petro').
43 The day following Jesus would go forth into Galilee, and findeth Philip, and saith unto him, Follow me.
Siku iliyofuata wakati Yesu alipotaka kuondoka kwenda Galilaya, alimpata Filipo na akamwambia, “Nifuate mimi.”
44 Now Philip was of Bethsaida, the city of Andrew and Peter.
Filipo alikuwa ni mwenyeji wa Bethsaida, mji wa Andrea na Petro.
45 Philip findeth Nathanael, and saith unto him, We have found him, of whom Moses in the law, and the prophets, did write, Jesus of Nazareth, the son of Joseph.
Filipo alimpata Nathanaeli na kumwambia, Tumempata yule ambaye Musa aliandika habari zake katika sheria na Manabii. Yesu mwana wa Yusufu, kutoka Nazareti.
46 And Nathanael said unto him, Can there any good thing come out of Nazareth? Philip saith unto him, Come and see.
Nathanaeli akamwambia, “Je kitu chema chaweza kutokea Nazareti?” Filipo akamwambia, Njoo na uone.”
47 Jesus saw Nathanael coming to him, and saith of him, Behold an Israelite indeed, in whom is no guile!
Yesu akamwona Nathanaeli akija kwake na akasema, “Tazama, Mwisraeli kweli kweli asiye na udanganyifu ndani yake!”
48 Nathanael saith unto him, Whence knowest thou me? Jesus answered and said unto him, Before that Philip called thee, when thou wast under the fig tree, I saw thee.
Nathanaeli akamwambia, “Umenifahamuje mimi?” Yesu akajibu na akamwambia, “Kabla Filipo hajakuita ulipokuwa chini ya mtini, nalikuona.”
49 Nathanael answered and saith unto him, Rabbi, thou art the Son of God; thou art the King of Israel.
Nathanaeli akajibu, “Rabi wewe u Mwana wa Mungu! Wewe ni Mfalme wa Israeli”!
50 Jesus answered and said unto him, Because I said unto thee, I saw thee under the fig tree, believest thou? thou shalt see greater things than these.
Yesu akajibu akamwambia, Kwa sababu nilikuambia 'nilikuona chini ya mtini' je waamini? utaona matendo makubwa kuliko haya.”
51 And he saith unto him, Verily, verily, I say unto you, Hereafter ye shall see heaven open, and the angels of God ascending and descending upon the Son of man.
Yesu akasema, “Amini amini nawambieni mtaziona mbingu zikifunguka, na kuwaona malaika wakipanda na kushuka juu ya Mwana wa Adamu.”

< John 1 >