< Luke 12 >

1 In the mean time, when there were gathered together an innumerable multitude of people, so that they stepped one on another, he began to say to his disciples first of all, Beware you of the leaven of the Pharisees, which is hypocrisy.
Wakati huo, umati mkubwa wa watu maelfu, walipokuwa wamekusanyika hata wakawa wanakanyagana, Yesu akaanza kuzungumza kwanza na wanafunzi wake, akawaambia: “Jihadharini na chachu ya Mafarisayo, yaani, unafiki wao.
2 For there is nothing covered, that shall not be revealed; neither hid, that shall not be known.
Hakuna jambo lolote lililositirika ambalo halitafunuliwa, au lililofichwa ambalo halitajulikana.
3 Therefore whatever you have spoken in darkness shall be heard in the light; and that which you have spoken in the ear in closets shall be proclaimed on the housetops.
Kwa hiyo, lolote mlilosema gizani litasikiwa nuruni. Na kile mlichonongʼona masikioni mkiwa kwenye vyumba vya ndani, kitatangazwa juu ya paa.
4 And I say to you my friends, Be not afraid of them that kill the body, and after that have no more that they can do.
“Nawaambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, lakini baada ya hilo hawawezi kufanya lolote zaidi.
5 But I will forewarn you whom you shall fear: Fear him, which after he has killed has power to cast into hell; yes, I say to you, Fear him. (Geenna g1067)
Lakini nitawaambia nani wa kumwogopa: Mwogopeni yule ambaye baada ya kuua mwili, ana mamlaka ya kuwatupa motoni. Naam, nawaambia, mwogopeni huyo! (Geenna g1067)
6 Are not five sparrows sold for two farthings, and not one of them is forgotten before God?
Mnajua kwamba shomoro watano huuzwa kwa senti mbili? Lakini Mungu hamsahau hata mmoja wao.
7 But even the very hairs of your head are all numbered. Fear not therefore: you are of more value than many sparrows.
Naam, hata nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa thamani kubwa kuliko shomoro wengi.
8 Also I say to you, Whoever shall confess me before men, him shall the Son of man also confess before the angels of God:
“Ninawaambia kwamba yeyote atakayenikiri mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkiri mbele za malaika wa Mungu.
9 But he that denies me before men shall be denied before the angels of God.
Lakini yeye atakayenikana mimi mbele ya watu, Mwana wa Adamu naye atamkana mbele ya malaika wa Mungu.
10 And whoever shall speak a word against the Son of man, it shall be forgiven him: but to him that blasphemes against the Holy Ghost it shall not be forgiven.
Naye kila atakayenena neno baya dhidi ya Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini yeyote atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa.
11 And when they bring you to the synagogues, and to magistrates, and powers, take you no thought how or what thing you shall answer, or what you shall say:
“Watakapowapeleka katika masinagogi, na mbele ya watawala na wenye mamlaka, msiwe na wasiwasi kuhusu namna mtakavyojitetea au mtakavyosema.
12 For the Holy Ghost shall teach you in the same hour what you ought to say.
Kwa maana Roho Mtakatifu atawafundisha wakati huo huo mnachopaswa kusema.”
13 And one of the company said to him, Master, speak to my brother, that he divide the inheritance with me.
Mtu mmoja katika umati wa watu akamwambia Yesu, “Mwalimu, mwambie ndugu yangu tugawane naye urithi wetu.”
14 And he said to him, Man, who made me a judge or a divider over you?
Lakini Yesu akamwambia, “Rafiki, ni nani aliyeniweka mimi kuwa hakimu wenu au msuluhishi juu yenu?”
15 And he said to them, Take heed, and beware of covetousness: for a man’s life consists not in the abundance of the things which he possesses.
Ndipo Yesu akawaambia, “Jihadharini! Jilindeni na aina zote za choyo. Kwa maana maisha ya mtu hayatokani na wingi wa mali alizo nazo.”
16 And he spoke a parable to them, saying, The ground of a certain rich man brought forth plentifully:
Kisha akawaambia mfano huu: “Shamba la mtu mmoja tajiri lilizaa sana.
17 And he thought within himself, saying, What shall I do, because I have no room where to bestow my fruits?
Akawaza moyoni mwake, ‘Nifanye nini? Sina mahali pa kuhifadhi mavuno yangu.’
18 And he said, This will I do: I will pull down my barns, and build greater; and there will I bestow all my fruits and my goods.
“Ndipo huyo tajiri akasema, ‘Nitafanya hivi: Nitabomoa ghala zangu za nafaka na kujenga nyingine kubwa zaidi na huko nitayahifadhi mavuno yangu yote na vitu vyangu.
19 And I will say to my soul, Soul, you have much goods laid up for many years; take your ease, eat, drink, and be merry.
Nami nitaiambia nafsi yangu, “Nafsi, unavyo vitu vingi vizuri ulivyojiwekea akiba kwa miaka mingi. Pumzika; kula, unywe, ufurahi.”’
20 But God said to him, You fool, this night your soul shall be required of you: then whose shall those things be, which you have provided?
“Lakini Mungu akamwambia, ‘Mpumbavu wewe! Usiku huu uhai wako unatakiwa. Sasa hivyo vitu ulivyojiwekea akiba vitakuwa vya nani?’
21 So is he that lays up treasure for himself, and is not rich toward God.
“Hivyo ndivyo ilivyo kwa wale wanaojiwekea mali lakini hawajitajirishi kwa Mungu.”
22 And he said to his disciples, Therefore I say to you, Take no thought for your life, what you shall eat; neither for the body, what you shall put on.
Kisha Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Kwa hiyo nawaambia, msisumbukie maisha yenu kwamba mtakula nini; au msumbukie miili yenu kwamba mtavaa nini.
23 The life is more than meat, and the body is more than raiment.
Maisha ni zaidi ya chakula, na mwili ni zaidi ya mavazi.
24 Consider the ravens: for they neither sow nor reap; which neither have storehouse nor barn; and God feeds them: how much more are you better than the fowls?
Fikirini ndege! Wao hawapandi wala hawavuni, hawana ghala wala popote pa kuhifadhi nafaka; lakini Mungu huwalisha. Ninyi ni wa thamani zaidi kuliko ndege!
25 And which of you with taking thought can add to his stature one cubit?
Ni nani miongoni mwenu ambaye kwa kujitaabisha kwake anaweza kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha yake?
26 If you then be not able to do that thing which is least, why take you thought for the rest?
Kama hamwezi kufanya jambo dogo kama hilo, kwa nini basi kuyasumbukia hayo mengine?
27 Consider the lilies how they grow: they toil not, they spin not; and yet I say to you, that Solomon in all his glory was not arrayed like one of these.
“Angalieni maua jinsi yameavyo: Hayafanyi kazi wala hayafumi. Lakini nawaambia, hata Solomoni katika fahari yake yote hakuvikwa vizuri kama mojawapo ya hayo maua.
28 If then God so clothe the grass, which is to day in the field, and to morrow is cast into the oven; how much more will he clothe you, O you of little faith?
Basi ikiwa Mungu huyavika hivi majani ya shambani, ambayo leo yapo, na kesho yanatupwa motoni, si atawavika ninyi vizuri zaidi, enyi wa imani haba!
29 And seek not you what you shall eat, or what you shall drink, neither be you of doubtful mind.
Wala msisumbuke mioyoni mwenu mtakula nini au mtakunywa nini. Msiwe na wasiwasi juu ya haya.
30 For all these things do the nations of the world seek after: and your Father knows that you have need of these things.
Watu wa mataifa ya duniani husumbuka sana kuhusu vitu hivi vyote, lakini Baba yenu anafahamu kuwa mnahitaji haya yote.
31 But rather seek you the kingdom of God; and all these things shall be added to you.
Bali utafuteni Ufalme wa Mungu, na haya yote atawapa pia.
32 Fear not, little flock; for it is your Father’s good pleasure to give you the kingdom.
“Msiogope enyi kundi dogo, kwa maana Baba yenu ameona vyema kuwapa ninyi Ufalme.
33 Sell that you have, and give alms; provide yourselves bags which wax not old, a treasure in the heavens that fails not, where no thief approaches, neither moth corrupts.
Uzeni mali zenu mkawape maskini. Jifanyieni mifuko isiyochakaa, mkajiwekee hazina mbinguni isiyokwisha, mahali ambapo mwizi hakaribii wala nondo haharibu.
34 For where your treasure is, there will your heart be also.
Kwa sababu mahali hazina yako ilipo, hapo ndipo moyo wako utakapokuwa pia.
35 Let your loins be girded about, and your lights burning;
“Kuweni tayari mkiwa mmevikwa kwa ajili ya huduma na taa zenu zikiwa zinawaka,
36 And you yourselves like to men that wait for their lord, when he will return from the wedding; that when he comes and knocks, they may open to him immediately.
kama watumishi wanaomngojea bwana wao arudi kutoka kwenye karamu ya arusi, ili ajapo na kubisha mlango waweze kumfungulia mara.
37 Blessed are those servants, whom the lord when he comes shall find watching: truly I say to you, that he shall gird himself, and make them to sit down to meat, and will come forth and serve them.
Heri wale watumishi ambao bwana wao atakapokuja atawakuta wakiwa wanakesha. Amin, nawaambia, atajifunga mkanda wake na kuwaketisha ili wale, naye atakuja na kuwahudumia.
38 And if he shall come in the second watch, or come in the third watch, and find them so, blessed are those servants.
Itakuwa heri kwa watumwa hao ikiwa bwana wao atakapokuja atawakuta wamekesha hata kama atakuja mnamo usiku wa manane, au karibu na mapambazuko.
39 And this know, that if the manager of the house had known what hour the thief would come, he would have watched, and not have suffered his house to be broken through.
Lakini fahamuni jambo hili: Kama mwenye nyumba angalijua saa mwizi atakuja, asingaliiacha nyumba yake kuvunjwa.
40 Be you therefore ready also: for the Son of man comes at an hour when you think not.
Ninyi nanyi hamna budi kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja saa msiyotazamia.”
41 Then Peter said to him, Lord, speak you this parable to us, or even to all?
Ndipo Petro akamuuliza, “Bwana, mfano huu unatuambia sisi peke yetu au watu wote?”
42 And the Lord said, Who then is that faithful and wise steward, whom his lord shall make ruler over his household, to give them their portion of meat in due season?
Yesu akamjibu, “Ni yupi basi wakili mwaminifu na mwenye busara, ambaye bwana wake atamfanya msimamizi juu ya watumishi wake wote, ili awape watumishi wengine chakula chao wakati unaofaa?
43 Blessed is that servant, whom his lord when he comes shall find so doing.
Heri mtumishi yule ambaye bwana wake atakaporudi atamkuta akifanya hivyo.
44 Of a truth I say to you, that he will make him ruler over all that he has.
Amin nawaambia, atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa mali yake yote.
45 But and if that servant say in his heart, My lord delays his coming; and shall begin to beat the menservants and maidens, and to eat and drink, and to be drunken;
Lakini kama yule mtumishi atasema moyoni mwake, ‘Bwana wangu anakawia kurudi,’ kisha akaanza kuwapiga wale watumishi wa kiume na wa kike, na kula na kunywa na kulewa.
46 The lord of that servant will come in a day when he looks not for him, and at an hour when he is not aware, and will cut him in sunder, and will appoint him his portion with the unbelievers.
Basi bwana wa mtumishi huyo atakuja siku asiyodhani na saa asiyoijua. Atamkata vipande vipande na kumweka katika sehemu moja pamoja na wale wasioamini.
47 And that servant, which knew his lord’s will, and prepared not himself, neither did according to his will, shall be beaten with many stripes.
“Yule mtumishi anayefahamu vyema mapenzi ya bwana wake na asijiandae wala kufanya kama apendavyo bwana wake, atapigwa kwa mapigo mengi.
48 But he that knew not, and did commit things worthy of stripes, shall be beaten with few stripes. For to whomsoever much is given, of him shall be much required: and to whom men have committed much, of him they will ask the more.
Lakini yeyote ambaye hakujua naye akafanya yale yastahiliyo kupigwa, atapigwa kidogo. Yeyote aliyepewa vitu vingi, atadaiwa vingi; na yeyote aliyekabidhiwa vingi, kwake vitatakiwa vingi.
49 I am come to send fire on the earth; and what will I, if it be already kindled?
“Nimekuja kuleta moto duniani; laiti kama ungekuwa tayari umewashwa!
50 But I have a baptism to be baptized with; and how am I straitened till it be accomplished!
Lakini ninao ubatizo ambao lazima nibatizwe, nayo dhiki yangu ni kuu mpaka ubatizo huo ukamilike!
51 Suppose you that I am come to give peace on earth? I tell you, No; but rather division:
Mnadhani nimekuja kuleta amani duniani? La, nawaambia sivyo, nimekuja kuleta mafarakano.
52 For from now on there shall be five in one house divided, three against two, and two against three.
Kuanzia sasa, kutakuwa na watu watano katika nyumba moja, watatu dhidi ya wawili, na wawili dhidi ya watatu.
53 The father shall be divided against the son, and the son against the father; the mother against the daughter, and the daughter against the mother; the mother in law against her daughter in law, and the daughter in law against her mother in law.
Watafarakana baba dhidi ya mwanawe na mwana dhidi ya babaye, mama dhidi ya bintiye na binti dhidi ya mamaye, naye mama mkwe dhidi ya mkwewe na mkwe dhidi ya mama mkwe wake.”
54 And he said also to the people, When you see a cloud rise out of the west, straightway you say, There comes a shower; and so it is.
Pia Yesu akauambia ule umati wa watu, “Mwonapo wingu likitokea magharibi, mara mwasema, ‘Mvua itanyesha,’ nayo hunyesha.
55 And when you see the south wind blow, you say, There will be heat; and it comes to pass.
Nanyi mwonapo upepo wa kusini ukivuma, ninyi husema, ‘Kutakuwa na joto,’ na huwa hivyo.
56 You hypocrites, you can discern the face of the sky and of the earth; but how is it that you do not discern this time?
Enyi wanafiki! Mnajua jinsi ya kutambua kuonekana kwa dunia na anga. Inakuwaje basi kwamba mnashindwa kutambua wakati huu wa sasa?
57 Yes, and why even of yourselves judge you not what is right?
“Kwa nini hamwamui wenyewe lililo haki?
58 When you go with your adversary to the magistrate, as you are in the way, give diligence that you may be delivered from him; lest he hale you to the judge, and the judge deliver you to the officer, and the officer cast you into prison.
Uwapo njiani na mshtaki wako kwenda kwa hakimu, jitahidi kupatana naye mkiwa njiani. La sivyo, atakupeleka kwa hakimu, naye hakimu atakukabidhi kwa afisa, naye afisa atakutupa gerezani.
59 I tell you, you shall not depart there, till you have paid the very last mite.
Nakuambia, hautatoka humo hadi uwe umelipa senti ya mwisho.”

< Luke 12 >