< Zechariah 7 >

1 And it came to pass in the fourth year of king Darius, that the word of the LORD came unto Zechariah in the fourth day of the ninth month, even in Chislev;
Katika mwaka wa nne wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia Zekaria siku ya nne ya mwezi wa tisa, mwezi wa Kisleu.
2 When Bethel-sarezer, and Regem-melech and his men, had sent to entreat the favour of the LORD,
Watu wa Betheli walikuwa wamemtuma Shareza na Regem-Meleki pamoja na watu wao, kumsihi Bwana
3 and to speak unto the priests of the house of the LORD of hosts, and to the prophets, saying: 'Should I weep in the fifth month, separating myself, as I have done these so many years?'
kwa kuwauliza makuhani wa nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote na manabii, “Je, imempasa kuomboleza na kufunga katika mwezi wa tano, kama ambavyo nimekuwa nikifanya kwa miaka mingi?”
4 Then came the word of the LORD of hosts unto me, saying:
Kisha neno la Bwana Mwenye Nguvu Zote likanijia kusema:
5 'Speak unto all the people of the land, and to the priests, saying: When ye fasted and mourned in the fifth and in the seventh month, even these seventy years, did ye at all fast unto Me, even to Me?
“Waulize watu wote wa nchi na makuhani, ‘Je, mlipofunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba kwa miaka sabini iliyopita, mlifunga kweli kwa ajili yangu?
6 And when ye eat, and when ye drink, are ye not they that eat, and they that drink?
Na mlipokuwa mkila na kunywa, je, hamkuwa mnasherehekea kwa ajili ya nafsi zenu?
7 Should ye not hearken to the words which the LORD hath proclaimed by the former prophets, when Jerusalem was inhabited and in prosperity, and the cities thereof round about her, and the South and the Lowland were inhabited?'
Je, haya sio maneno ya Bwana aliyosema kupitia manabii waliotangulia, wakati Yerusalemu pamoja na miji inayoizunguka ilipokuwa katika hali ya utulivu na ya mafanikio, wakati Negebu na Shefala zikiwa zimekaliwa na watu?’”
8 And the word of the LORD came unto Zechariah, saying:
Neno la Bwana likamjia tena Zekaria:
9 'Thus hath the LORD of hosts spoken, saying: Execute true judgment, and show mercy and compassion every man to his brother;
“Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Fanyeni hukumu za haki, onyesheni rehema na huruma ninyi kwa ninyi.
10 and oppress not the widow, nor the fatherless, the stranger, nor the poor; and let none of you devise evil against his brother in your heart.
Msimwonee mjane wala yatima, mgeni wala maskini. Msiwaziane mabaya mioyoni mwenu ninyi kwa ninyi.’
11 But they refused to attend, and turned a stubborn shoulder, and stopped their ears, that they might not hear.
“Lakini wakakataa kusikiliza, wakanipa kisogo kwa ukaidi na kuziba masikio yao.
12 Yea, they made their hearts as an adamant stone, lest they should hear the law, and the words which the LORD of hosts had sent by His spirit by the hand of the former prophets; therefore came there great wrath from the LORD of hosts.
Wakaifanya mioyo yao migumu kama jiwe gumu na hawakuisikiliza sheria au maneno ambayo Bwana Mwenye Nguvu Zote aliyatuma kwa njia ya Roho wake kupitia manabii waliotangulia. Kwa hiyo Bwana Mwenye Nguvu Zote alikasirika sana.
13 And it came to pass that, as He called, and they would not hear; so they shall call, and I will not hear, said the LORD of hosts;
“‘Wakati nilipoita, hawakusikiliza, kwa hiyo walipoita, sikusikiliza,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
14 but I will scatter them with a whirlwind among all the nations whom they have not known. Thus the land was desolate after them, so that no man passed through nor returned; for they laid the pleasant land desolate.'
‘Niliwatawanya kwa upepo wa kisulisuli miongoni mwa mataifa yote, mahali ambapo walikuwa wageni. Nchi ikaachwa ukiwa nyuma yao kiasi kwamba hakuna aliyeweza kuingia au kutoka. Hivi ndivyo walivyoifanya ile nchi iliyokuwa imependeza kuwa ukiwa.’”

< Zechariah 7 >