< Zechariah 1 >

1 IN THE eighth month, in the second year of Darius, came the word of the LORD unto Zechariah the son of Berechiah, the son of Iddo, the prophet, saying:
Katika mwezi wa nane wa mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia, mwana wa Ido, kusema:
2 'The LORD hath been sore displeased with your fathers.
“Bwana aliwakasirikia sana baba zako wa zamani.
3 Therefore say thou unto them, Thus saith the LORD of hosts: Return unto Me, saith the LORD of hosts, and I will return unto you, saith the LORD of hosts.
Kwa hiyo waambie watu: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Nirudieni mimi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitawarudia ninyi,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
4 Be ye not as your fathers, unto whom the former prophets proclaimed, saying: Thus saith the LORD of hosts: Return ye now from your evil ways, and from your evil doings; but they did not hear, nor attend unto Me, saith the LORD.
Msiwe kama baba zenu, ambao manabii waliotangulia waliwatangazia: Hivi ndivyo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemavyo: ‘Geukeni, mziache njia zenu mbaya na matendo yenu maovu.’ Lakini hawakunisikiliza wala kufuata maelekezo yangu, asema Bwana.
5 Your fathers, where are they? and the prophets, do they live for ever?
Wako wapi baba zako sasa? Nao manabii, je, wanaishi milele?
6 But My words and My statutes, which I commanded My servants the prophets, did they not overtake your fathers? so that they turned and said: Like as the LORD of hosts purposed to do unto us, according to our ways, and according to our doings, so hath He dealt with us.'
Je, maneno yangu na amri zangu nilizowaagiza manabii watumishi wangu, hayakuwapata baba zenu?” “Kisha walitubu na kusema, ‘Bwana Mwenye Nguvu Zote ametutenda sawasawa na njia zetu na matendo yetu yalivyostahili, kama alivyokusudia kufanya.’”
7 Upon the four and twentieth day of the eleventh month, which is the month Shebat, in the second year of Darius, came the word of the LORD unto Zechariah the son of Berechiah, the son of Iddo, the prophet, saying —
Katika siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kumi na moja, yaani mwezi uitwao Shebati, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario, neno la Bwana lilimjia nabii Zekaria mwana wa Berekia mwana wa Ido.
8 I saw in the night, and behold a man riding upon a red horse, and he stood among the myrtle-trees that were in the bottom; and behind him there were horses, red, sorrel, and white.
Wakati wa usiku nilipata maono, mbele yangu alikuwepo mtu akiendesha farasi mwekundu! Alikuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi kwenye bonde. Nyuma yake walikuwepo farasi wekundu, wa kikahawia na weupe.
9 Then said I: 'O my lord, what are these?' And the angel that spoke with me said unto me: 'I will show thee what these are.'
Nikauliza, “Hivi ni vitu gani bwana wangu?” Malaika aliyekuwa akizungumza na mimi akanijibu, “Nitakuonyesha kuwa ni nini.”
10 And the man that stood among the myrtle-trees answered and said: 'These are they whom the LORD hath sent to walk to and fro through the earth.'
Kisha yule mtu aliyesimama katikati ya miti ya mihadasi akaeleza, “Ni wale ambao Bwana amewatuma waende duniani kote.”
11 And they answered the angel of the LORD that stood among the myrtle-trees, and said: 'We have walked to and fro through the earth, and, behold, all the earth sitteth still, and is at rest.'
Nao wakatoa taarifa kwa yule malaika wa Bwana, aliyekuwa amesimama katikati ya miti ya mihadasi, “Tumepita duniani kote na kukuta ulimwengu wote umepumzika kwa amani.”
12 Then the angel of the LORD spoke and said: 'O LORD of hosts, how long wilt Thou not have compassion on Jerusalem and on the cities of Judah, against which Thou hast had indignation these threescore and ten years?
Kisha malaika wa Bwana akasema, “Bwana Mwenye Nguvu Zote, utazuia mpaka lini rehema kutoka Yerusalemu na miji ya Yuda, ambayo umeikasirikia kwa miaka hii sabini?”
13 And the LORD answered the angel that spoke with me with good words, even comforting words —
Kwa hiyo Bwana akazungumza maneno ya upole na ya kufariji kwa malaika aliyezungumza nami.
14 so the angel that spoke with me said unto me: 'Proclaim thou, saying: Thus saith the LORD of hosts: I am jealous for Jerusalem and for Zion with a great jealousy;
Kisha malaika yule aliyekuwa akizungumza nami akasema, “Tangaza neno hili: Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: ‘Nina wivu sana kwa ajili ya Yerusalemu na Sayuni,
15 and I am very sore displeased with the nations that are at ease; for I was but a little displeased, and they helped for evil.
lakini nimeyakasirikia sana mataifa yanayojisikia kuwa yako salama. Nilikuwa nimewakasirikia Israeli kidogo tu, lakini mataifa hayo yaliwazidishia maafa.’
16 Therefore thus saith the LORD: I return to Jerusalem with compassions: My house shall be built in it, saith the LORD of hosts, and a line shall be stretched forth over Jerusalem.
“Kwa hiyo, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Nitairudia Yerusalemu kwa rehema na huko nyumba yangu itajengwa tena. Nayo kamba ya kupimia itanyooshwa Yerusalemu,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.
17 Again, proclaim, saying: Thus saith the LORD of hosts: My cities shall again overflow with prosperity; and the LORD shall yet comfort Zion, and shall yet choose Jerusalem.'
“Endelea kutangaza zaidi kwamba: Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Miji yangu itafurika tena ustawi na Bwana atamfariji tena Sayuni na kumchagua Yerusalemu.’”
18 And I lifted up mine eyes, and saw, and behold four horns.
Kisha nikatazama juu, na pale mbele yangu nikaona pembe nne!
19 And I said unto the angel that spoke with me: 'What are these?' And he said unto me: 'These are the horns which have scattered Judah, Israel, and Jerusalem.'
Nikamuuliza yule malaika aliyekuwa akizungumza nami, “Ni nini hivi?” Akanijibu, “Hizi ni zile pembe zilizowatawanya Yuda, Israeli na Yerusalemu.”
20 And the LORD showed me four craftsmen.
Kisha Bwana akanionyesha mafundi wanne.
21 Then said I: 'What come these to do?' And he spoke, saying: 'These — the horns which scattered Judah, so that no man did lift up his head — these then are come to frighten them, to cast down the horns of the nations, which lifted up their horn against the land of Judah to scatter it.'
Nikauliza, “Hawa wanakuja kufanya nini?” Akanijibu, “Hizi ndizo pembe zilizowatawanya Yuda ili asiwepo atakayeweza kuinua kichwa chake, lakini mafundi wamekuja kuzitia hofu na kuzitupa chini hizi pembe za mataifa ambayo yaliinua pembe zao dhidi ya nchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.”

< Zechariah 1 >