< Psalms 81 >

1 For the Leader; upon the Gittith. A Psalm of Asaph. Sing aloud unto God our strength; shout unto the God of Jacob.
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya Asafu. Mwimbieni kwa furaha, Mungu aliye nguvu yetu; mpigieni kelele za shangwe Mungu wa Yakobo!
2 Take up the melody, and sound the timbrel, the sweet harp with the psaltery.
Anzeni wimbo, pigeni matari, pigeni kinubi na zeze kwa sauti nzuri.
3 Blow the horn at the new moon, at the full moon for our feast-day.
Pigeni baragumu za pembe za kondoo dume wakati wa Mwandamo wa Mwezi, na wakati wa mwezi mpevu, katika siku ya Sikukuu yetu;
4 For it is a statute for Israel, an ordinance of the God of Jacob.
hii ni amri kwa Israeli, agizo la Mungu wa Yakobo.
5 He appointed it in Joseph for a testimony, when He went forth against the land of Egypt. The speech of one that I knew not did I hear:
Aliiweka iwe kama sheria kwa Yosefu alipotoka dhidi ya Misri, huko tulikosikia lugha ambayo hatukuielewa.
6 'I removed his shoulder from the burden; His hands were freed from the basket.
Asema, “Nimeondoa mzigo mabegani mwao; mikono yao iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.
7 Thou didst call in trouble, and I rescued thee; I answered thee in the secret place of thunder; I proved thee at the waters of Meribah. (Selah)
Katika shida yako uliniita nami nikakuokoa, nilikujibu katika mawingu yenye ngurumo; nilikujaribu katika maji ya Meriba.
8 Hear, O My people, and I will admonish thee: O Israel, if thou wouldest hearken unto Me!
“Enyi watu wangu, sikieni, nami nitawaonya: laiti kama mngenisikiliza, ee Israeli!
9 There shall no strange god be in thee; neither shalt thou worship any foreign god.
Hamtakuwa na mungu mgeni miongoni mwenu; msimsujudie mungu wa kigeni.
10 I am the LORD thy God, who brought thee up out of the land of Egypt; open thy mouth wide, and I will fill it.
Mimi ni Bwana Mungu wako, niliyekutoa nchi ya Misri. Panua sana kinywa chako nami nitakijaza.
11 But My people hearkened not to My voice; and Israel would none of Me.
“Lakini watu wangu hawakutaka kunisikiliza; Israeli hakutaka kunitii.
12 So I let them go after the stubbornness of their heart, that they might walk in their own counsels.
Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.
13 Oh that My people would hearken unto Me, that Israel would walk in My ways!
“Laiti kama watu wangu wangalinisikiliza, kama Israeli wangalifuata njia zangu,
14 I would soon subdue their enemies, and turn My hand against their adversaries.
ningaliwatiisha adui zao kwa haraka, na kuugeuza mkono wangu dhidi ya watesi wao!
15 The haters of the LORD should dwindle away before Him; and their punishment should endure for ever.
Wale wanaomchukia Bwana wangalinyenyekea mbele zake, na adhabu yao ingedumu milele.
16 They should also be fed with the fat of wheat; and with honey out of the rock would I satisfy thee.'
Bali ninyi mngalilishwa ngano iliyo bora, na kuwatosheleza kwa asali itokayo kwenye mwamba.”

< Psalms 81 >