< Psalms 41 >

1 For the Leader. A Psalm of David. Happy is he that considereth the poor; the LORD will deliver him in the day of evil.
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi. Heri mtu yule anayemjali mnyonge, Bwana atamwokoa wakati wa shida.
2 The LORD preserve him, and keep him alive, let him be called happy in the land; and deliver not Thou him unto the greed of his enemies.
Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake, atambariki katika nchi na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
3 The LORD support him upon the bed of illness; mayest Thou turn all his lying down in his sickness.
Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani, atamwinua kutoka kitandani mwake.
4 As for me, I said: 'O LORD, be gracious unto me; heal my soul; for I have sinned against Thee.'
Nilisema, “Ee Bwana nihurumie, niponye, maana nimekutenda dhambi wewe.”
5 Mine enemies speak evil of me: 'When shall he die, and his name perish?'
Adui zangu wanasema kwa hila, “Lini atakufa, na jina lake litokomee kabisa.”
6 And if one come to see me, he speaketh falsehood; his heart gathereth iniquity to itself; when he goeth abroad, he speaketh of it.
Kila anapokuja mtu kunitazama, huzungumza uongo, huku moyo wake hukusanya masingizio; kisha huondoka na kuyasambaza huku na huko.
7 All that hate me whisper together against me, against me do they devise my hurt:
Adui zangu wote hunongʼonezana dhidi yangu, hao huniwazia mabaya sana, wakisema,
8 'An evil thing cleaveth fast unto him; and now that he lieth, he shall rise up no more.'
“Ugonjwa mbaya sana umempata, kamwe hatainuka tena kitandani mwake.”
9 Yea, mine own familiar friend, in whom I trusted, who did eat of my bread, hath lifted up his heel against me.
Hata rafiki yangu wa karibu niliyemwamini, yule aliyekula chakula changu ameniinulia kisigino chake.
10 But Thou, O LORD, be gracious unto me, and raise me up, that I may requite them.
Lakini wewe, Ee Bwana, nihurumie, ukaniinue tena, ili niweze kuwalipiza kisasi.
11 By this I know that Thou delightest in me, that mine enemy doth not triumph over me.
Najua kwamba wapendezwa nami, kwa kuwa adui yangu hanishindi.
12 And as for me, Thou upholdest me because of mine integrity, and settest me before Thy face for ever.
Katika uadilifu wangu unanitegemeza na kuniweka kwenye uwepo wako milele.
13 Blessed be the LORD, the God of Israel, from everlasting and to everlasting. Amen, and Amen.
Msifuni Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele.

< Psalms 41 >