< Psalms 141 >

1 A Psalm of David. LORD, I have called Thee; make haste unto me; give ear unto my voice, when I call unto Thee.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, ninakuita wewe, uje kwangu hima. Sikia sauti yangu ninapokuita.
2 Let my prayer be set forth as incense before Thee, the lifting up of my hands as the evening sacrifice.
Maombi yangu na yafike mbele zako kama uvumba; kuinua mikono yangu juu na kuwe kama dhabihu ya jioni.
3 Set a guard, O LORD, to my mouth; keep watch at the door of my lips.
Ee Bwana, weka mlinzi kinywani mwangu, weka ulinzi mlangoni mwa midomo yangu.
4 Incline not my heart to any evil thing, to be occupied in deeds of wickedness with men that work iniquity; and let me not eat of their dainties.
Usiuache moyo wangu uvutwe katika jambo baya, nisije nikashiriki katika matendo maovu pamoja na watu watendao mabaya, wala nisije nikala vyakula vyao vya anasa.
5 Let the righteous smite me in kindness, and correct me; oil so choice let not my head refuse; for still is my prayer because of their wickedness.
Mtu mwenye haki na anipige: ni jambo la huruma; na anikemee: ni mafuta kichwani mwangu. Kichwa changu hakitalikataa. Hata hivyo, maombi yangu daima ni kinyume cha watenda mabaya,
6 Their judges are thrown down by the sides of the rock; and they shall hear my words, that they are sweet.
watawala wao watatupwa chini kutoka kwenye majabali, waovu watajifunza kwamba maneno yangu yalikuwa kweli.
7 As when one cleaveth and breaketh up the earth, our bones are scattered at the grave's mouth. (Sheol h7585)
Watasema, “Kama mtu anavyolima na kuvunja ardhi, ndivyo mifupa yetu imetawanywa kwenye mlango wa kaburi.” (Sheol h7585)
8 For mine eyes are unto Thee, O GOD the Lord; in Thee have I taken refuge, O pour not out my soul.
Lakini nimekaza macho yangu kwako, Ee Bwana Mwenyezi, ndani yako nimekimbilia, usiniache nife.
9 Keep me from the snare which they have laid for me, and from the gins of the workers of iniquity.
Niepushe na mitego waliyonitegea, kutokana na mitego iliyotegwa na watenda mabaya.
10 Let the wicked fall into their own nets, whilst I withal escape.
Waovu na waanguke kwenye nyavu zao wenyewe, wakati mimi ninapita salama.

< Psalms 141 >