< Psalms 1 >

1 BOOK I HAPPY IS the man that hath not walked in the counsel of the wicked, nor stood in the way of sinners, nor sat in the seat of the scornful.
Heri mtu yule ambaye haendi katika shauri la watu waovu, wala hasimami katika njia ya wenye dhambi, au kuketi katika baraza la wenye mizaha.
2 But his delight is in the law of the LORD; and in His law doth he meditate day and night.
Bali huifurahia sheria ya Bwana, naye huitafakari hiyo sheria usiku na mchana.
3 And he shall be like a tree planted by streams of water, that bringeth forth its fruit in its season, and whose leaf doth not wither; and in whatsoever he doeth he shall prosper.
Mtu huyo ni kama mti uliopandwa kando ya vijito vya maji, ambao huzaa matunda kwa majira yake na majani yake hayanyauki. Lolote afanyalo hufanikiwa.
4 Not so the wicked; but they are like the chaff which the wind driveth away.
Sivyo walivyo waovu! Wao ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
5 Therefore the wicked shall not stand in the judgment, nor sinners in the congregation of the righteous.
Kwa hiyo waovu hawatastahimili hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
6 For the LORD regardeth the way of the righteous; but the way of the wicked shall perish.
Kwa maana Bwana huziangalia njia za mwenye haki, bali njia ya waovu itaangamia.

< Psalms 1 >