< Proverbs 29 >

1 He that being often reproved hardeneth his neck shall suddenly be broken, and that without remedy.
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 When the righteous are increased, the people rejoice; but when the wicked beareth rule, the people sigh.
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 Whoso loveth wisdom rejoiceth his father; but he that keepeth company with harlots wasteth his substance.
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 The king by justice establisheth the land; but he that exacteth gifts overthroweth it.
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 A man that flattereth his neighbour spreadeth a net for his steps.
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 In the transgression of an evil man there is a snare; but the righteous doth sing and rejoice.
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 The righteous taketh knowledge of the cause of the poor; the wicked understandeth not knowledge.
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 Scornful men set a city in a blaze; but wise men turn away wrath.
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 If a wise man contendeth with a foolish man, whether he be angry or laugh, there will be no rest.
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 The men of blood hate him that is sincere; and as for the upright, they seek his life.
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 A fool spendeth all his spirit; but a wise man stilleth it within him.
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
12 If a ruler hearkeneth to falsehood, all his servants are wicked.
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
13 The poor man and the oppressor meet together; the LORD giveth light to the eyes of them both.
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 The king that faithfully judgeth the poor, his throne shall be established for ever.
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 The rod and reproof give wisdom; but a child left to himself causeth shame to his mother.
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
16 When the wicked are increased, transgression increaseth; but the righteous shall gaze upon their fall.
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 Correct thy son, and he will give thee rest; yea, he will give delight unto thy soul.
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
18 Where there is no vision, the people cast off restraint; but he that keepeth the law, happy is he.
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19 A servant will not be corrected by words; for though he understand, there will be no response.
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
20 Seest thou a man that is hasty in his words? there is more hope for a fool than for him.
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21 He that delicately bringeth up his servant from a child shall have him become master at the last.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
22 An angry man stirreth up strife, and a wrathful man aboundeth in transgression.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
23 A man's pride shall bring him low; but he that is of a lowly spirit shall attain to honour.
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
24 Whoso is partner with a thief hateth his own soul: he heareth the adjuration and uttereth nothing.
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 The fear of man bringeth a snare; but whoso putteth his trust in the LORD shall be set up on high.
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 Many seek the ruler's favour; but a man's judgment cometh from the LORD.
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 An unjust man is an abomination to the righteous; and he that is upright in the way is an abomination to the wicked.
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.

< Proverbs 29 >