< Proverbs 27 >

1 Boast not thyself of to-morrow; for thou knowest not what a day may bring forth.
Usijisifu kwa ajili ya kesho, kwa kuwa hujui ni nini kitakachozaliwa kwa siku moja.
2 Let another man praise thee, and not thine own mouth; a stranger, and not thine own lips.
Mwache mwingine akusifu, wala si kinywa chako mwenyewe; mtu mwingine afanye hivyo na si midomo yako mwenyewe.
3 A stone is heavy, and the sand weighty; but a fool's vexation is heavier than they both.
Jiwe ni zito na mchanga ni mzigo, lakini kukasirishwa na mpumbavu ni kuzito kuliko vyote viwili.
4 Wrath is cruel, and anger is overwhelming; but who is able to stand before jealousy?
Hasira ni ukatili na ghadhabu kali ni gharika, lakini ni nani awezaye kusimama mbele ya wivu?
5 Better is open rebuke than love that is hidden.
Afadhali karipio la wazi kuliko upendo uliofichika.
6 Faithful are the wounds of a friend; but the kisses of an enemy are importunate.
Majeraha kutoka kwa rafiki yaonyesha uaminifu, bali kubusu kwa adui ni kwingi sana.
7 The full soul loatheth a honeycomb; but to the hungry soul every bitter thing is sweet.
Yeye aliyeshiba huchukia kabisa asali, bali kwa mwenye njaa hata kile kilicho kichungu kwake ni kitamu.
8 As a bird that wandereth from her nest, so is a man that wandereth from his place.
Kama ndege atangatangavyo mbali na kiota chake, ndivyo alivyo mtu atangatangaye mbali na nyumbani mwake.
9 Ointment and perfume rejoice the heart; so doth the sweetness of a man's friend by hearty counsel.
Manukato na uvumba huleta furaha moyoni, nao uzuri wa rafiki huchipuka kutoka kwenye ushauri wake wa uaminifu.
10 Thine own friend, and thy father's friend, forsake not; neither go into thy brother's house in the day of thy calamity; better is a neighbour that is near than a brother far off.
Usimwache rafiki yako wala rafiki wa baba yako, tena usiende nyumbani mwa ndugu yako wakati umepatwa na maafa. Bora jirani wa karibu kuliko ndugu aliye mbali.
11 My son, be wise, and make my heart glad, that I may answer him that taunteth me.
Mwanangu, uwe na hekima, nawe ulete furaha moyoni mwangu, ndipo nitakapoweza kumjibu yeyote anitendaye kwa dharau.
12 A prudent man seeth the evil, and hideth himself; but the thoughtless pass on, and are punished.
Mtu mwenye busara huona hatari na kujificha, bali mjinga huendelea mbele nayo ikamtesa.
13 Take his garment that is surety for a stranger; and hold him in pledge that is surety for an alien woman.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
14 He that blesseth his friend with a loud voice, rising early in the morning, it shall be counted a curse to him.
Kama mtu akimbariki jirani yake kwa sauti kuu asubuhi na mapema, itahesabiwa kama ni laana.
15 A continual dropping in a very rainy day and a contentious woman are alike;
Mke mgomvi ni kama matone yasiyokoma ya siku ya mvua.
16 He that would hide her hideth the wind, and the ointment of his right hand betrayeth itself.
Kumzuia yeye ni kama kuuzuia upepo au kukamata mafuta kwa kiganja cha mkono.
17 Iron sharpeneth iron; so a man sharpeneth the countenance of his friend.
Kama vile chuma kinoavyo chuma, ndivyo mtu amnoavyo mwenzake.
18 Whoso keepeth the fig-tree shall eat the fruit thereof; and he that waiteth on his master shall be honoured.
Yeye autunzaye mtini atakula tunda lake, naye amtunzaye bwana wake ataheshimiwa.
19 As in water face answereth to face, so the heart of man to man.
Kama uso uonekanavyo kwenye maji, ndivyo hivyo moyo wa mtu humwonyesha alivyo.
20 The nether-world and Destruction are never satiated; so the eyes of man are never satiated. (Sheol h7585)
Kuzimu na Uharibifu havishibi kadhalika macho ya mwanadamu. (Sheol h7585)
21 The refining pot is for silver, and the furnace for gold, and a man is tried by his praise.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru kwa ajili ya dhahabu, bali mtu hupimwa kwa sifa azipokeazo.
22 Though thou shouldest bray a fool in a mortar with a pestle among groats, yet will not his foolishness depart from him.
Hata ukimtwanga mpumbavu kwenye kinu, ukimtwanga kama nafaka kwa mchi, hutauondoa upumbavu wake.
23 Be thou diligent to know the state of thy flocks, and look well to thy herds;
Hakikisha kuwa unajua hali ya makundi yako ya kondoo na mbuzi, angalia kwa bidii ngʼombe zako.
24 For riches are not for ever; and doth the crown endure unto all generations?
Kwa kuwa utajiri haudumu milele, nayo taji haidumu vizazi vyote.
25 When the hay is mown, and the tender grass showeth itself, and the herbs of the mountains are gathered in;
Wakati majani makavu yameondolewa na mapya yamechipua, nayo majani toka milimani yamekusanywa,
26 The lambs will be for thy clothing, and the goats the price for a field.
wana-kondoo watakupatia mavazi na mbuzi thamani ya shamba.
27 And there will be goats' milk enough for thy food, for the food of thy household; and maintenance for thy maidens.
Utakuwa na maziwa mengi ya mbuzi kukulisha wewe na jamaa yako, na kuwalisha watumishi wako wa kike.

< Proverbs 27 >