< Numbers 8 >

1 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
2 'Speak unto Aaron, and say unto him: When thou lightest the lamps, the seven lamps shall give light in front of the candlestick.'
“Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’”
3 And Aaron did so: he lighted the lamps thereof so as to give light in front of the candlestick, as the LORD commanded Moses.
Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
4 And this was the work of the candlestick, beaten work of gold; unto the base thereof, and unto the flowers thereof, it was beaten work; according unto the pattern which the LORD had shown Moses, so he made the candlestick.
Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.
5 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose:
6 'Take the Levites from among the children of Israel, and cleanse them.
“Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada.
7 And thus shalt thou do unto them, to cleanse them: sprinkle the water of purification upon them, and let them cause a razor to pass over all their flesh, and let them wash their clothes, and cleanse themselves.
Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe.
8 Then let them take a young bullock, and its meal-offering, fine flour mingled with oil, and another young bullock shalt thou take for a sin-offering.
Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi.
9 And thou shalt present the Levites before the tent of meeting; and thou shalt assemble the whole congregation of the children of Israel.
Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli.
10 And thou shalt present the Levites before the LORD; and the children of Israel shall lay their hands upon the Levites.
Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi.
11 And Aaron shall offer the Levites before the LORD for a wave-offering from the children of Israel, that they may be to do the service of the LORD.
Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.
12 And the Levites shall lay their hands upon the heads of the bullocks; and offer thou the one for a sin-offering, and the other for a burnt-offering, unto the LORD, to make atonement for the Levites.
“Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi.
13 And thou shalt set the Levites before Aaron, and before his sons, and offer them for a wave-offering unto the LORD.
Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana.
14 Thus shalt thou separate the Levites from among the children of Israel; and the Levites shall be Mine.
Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.
15 And after that shall the Levites go in to do the service of the tent of meeting; and thou shalt cleanse them, and offer them for a wave-offering.
“Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania.
16 For they are wholly given unto Me from among the children of Israel; instead of all that openeth the womb, even the first-born of all the children of Israel, have I taken them unto Me.
Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli.
17 For all the first-born among the children of Israel are Mine, both man and beast; on the day that I smote all the first-born in the land of Egypt I sanctified them for Myself.
Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe.
18 And I have taken the Levites instead of all the first-born among the children of Israel.
Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli.
19 And I have given the Levites — they are given to Aaron and to his sons from among the children of Israel, to do the service of the children of Israel in the tent of meeting, and to make atonement for the children of Israel, that there be no plague among the children of Israel, through the children of Israel coming nigh unto the sanctuary.'
Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”
20 Thus did Moses, and Aaron, and all the congregation of the children of Israel, unto the Levites; according unto all that the LORD commanded Moses touching the Levites, so did the children of Israel unto them.
Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose.
21 And the Levites purified themselves, and they washed their clothes; and Aaron offered them for a sacred gift before the LORD; and Aaron made atonement for them to cleanse them.
Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa.
22 And after that went the Levites in to do their service in the tent of meeting before Aaron, and before his sons; as the LORD had commanded Moses concerning the Levites, so did they unto them.
Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.
23 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
24 'This is that which pertaineth unto the Levites: from twenty and five years old and upward they shall go in to perform the service in the work of the tent of meeting;
“Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania,
25 and from the age of fifty years they shall return from the service of the work, and shall serve no more;
lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee.
26 but shall minister with their brethren in the tent of meeting, to keep the charge, but they shall do no manner of service. Thus shalt thou do unto the Levites touching their charges.'
Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”

< Numbers 8 >