< Numbers 31 >

1 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
2 'Avenge the children of Israel of the Midianites; afterward shalt thou be gathered unto thy people.'
“Uwalipize kisasi Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli. Halafu baada ya hayo, utakufa.”
3 And Moses spoke unto the people, saying: 'Arm ye men from among you for the war, that they may go against Midian, to execute the LORD'S vengeance on Midian.
Kwa hiyo Mose akawaambia watu, “Waandaeni baadhi ya wanaume wenu waende vitani kupigana na Wamidiani ili wawalipize kisasi cha Bwana.
4 Of every tribe a thousand, throughout all the tribes of Israel, shall ye send to the war.'
Peleka wanaume 1,000 vitani kutoka kila kabila la Israeli.”
5 So there were delivered, out of the thousands of Israel, a thousand of every tribe, twelve thousand armed for war.
Kwa hiyo waliandaliwa wanaume 12,000 kwa vita, wanaume 1,000 kutoka kila kabila, walitolewa kutoka koo za Israeli.
6 And Moses sent them, a thousand of every tribe, to the war, them and Phinehas the son of Eleazar the priest, to the war, with the holy vessels and the trumpets for the alarm in his hand.
Mose aliwatuma vitani, watu 1,000 kutoka kila kabila, pamoja na Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, ambaye alichukua vyombo vya mahali patakatifu na tarumbeta za kuashiria.
7 And they warred against Midian, as the LORD commanded Moses; and they slew every male.
Walipigana dhidi ya Wamidiani, kama Bwana alivyomwagiza Mose, nao waliua kila mwanaume.
8 And they slew the kings of Midian with the rest of their slain: Evi, and Rekem, and Zur, and Hur, and Reba, the five kings of Midian; Balaam also the son of Beor they slew with the sword.
Miongoni mwa watu waliouawa walikuwepo wafalme watano wa Midiani, nao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile walimuua Balaamu mwana wa Beori kwa upanga.
9 And the children of Israel took captive the women of Midian and their little ones; and all their cattle, and all their flocks, and all their goods, they took for a prey.
Waisraeli waliwateka wanawake wa Kimidiani pamoja na watoto wao na walichukua makundi ya ngʼombe, kondoo na mali zao kama nyara.
10 And all their cities in the places wherein they dwelt, and all their encampments, they burnt with fire.
Walichoma moto miji yote ambayo Wamidiani walikuwa wanaishi, pamoja na kambi zao zote.
11 And they took all the spoil, and all the prey, both of man and of beast.
Walichukua nyara zote na mateka, pamoja na watu na wanyama,
12 And they brought the captives, and the prey, and the spoil, unto Moses, and unto Eleazar the priest, and unto the congregation of the children of Israel, unto the camp, unto the plains of Moab, which are by the Jordan at Jericho.
nao waliwaleta wafungwa mateka na nyara kwa Mose na kwa kuhani Eleazari, nao Waisraeli walikusanyika kwenye kambi zao katika tambarare za nchi ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
13 And Moses, and Eleazar the priest, and all the princes of the congregation, went forth to meet them without the camp.
Mose, kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya wakatoka kuwalaki nje ya kambi.
14 And Moses was wroth with the officers of the host, the captains of thousands and the captains of hundreds, who came from the service of the war.
Mose aliwakasirikia maafisa wa jeshi, yaani hao wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, ambao walirudi kutoka vitani.
15 And Moses said unto them: 'Have ye saved all the women alive?
Mose akawauliza, “Je, mmewaacha wanawake wote hai?”
16 Behold, these caused the children of Israel, through the counsel of Balaam, to revolt so as to break faith with the LORD in the matter of Peor, and so the plague was among the congregation of the LORD.
“Wanawake hao ndio waliofuata ushauri wa Balaamu, nao ndio waliowasababisha Waisraeli wamwasi Bwana kwa kile kilichotokea kule Peori, na kwa hiyo pigo liliwapata watu wa Bwana.
17 Now therefore kill every male among the little ones, and kill every woman that hath known man by lying with him.
Sasa waue wavulana wote. Pia muue kila mwanamke ambaye alikwisha fanya tendo la ndoa,
18 But all the women children, that have not known man by lying with him, keep alive for yourselves.
lakini mwacheni hai kwa ajili yenu kila msichana ambaye kamwe hajawahi kuzini na mwanaume.
19 And encamp ye without the camp seven days; whosoever hath killed any person, and whosoever hath touched any slain, purify yourselves on the third day and on the seventh day, ye and your captives.
“Ninyi nyote ambao mmeua mtu yeyote au kumgusa mtu yeyote ambaye ameuawa, lazima mkae nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Katika siku ya tatu na ya saba lazima mjitakase wenyewe pamoja na wafungwa wenu.
20 And as to every garment, and all that is made of skin, and all work of goats' hair, and all things made of wood, ye shall purify.'
Takaseni kila vazi pamoja na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa singa za mbuzi au kwa mti.”
21 And Eleazar the priest said unto the men of war that went to the battle: 'This is the statute of the law which the LORD hath commanded Moses:
Kisha kuhani Eleazari aliwaambia askari waliokuwa wamekwenda vitani, “Haya ndiyo matakwa ya sheria ambayo Bwana alimpa Mose:
22 Howbeit the gold, and the silver, the brass, the iron, the tin, and the lead,
Dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, risasi,
23 every thing that may abide the fire, ye shall make to go through the fire, and it shall be clean; nevertheless it shall be purified with the water of sprinkling; and all that abideth not the fire ye shall make to go through the water.
na kitu kingine chochote ambacho kinaweza kuhimili moto lazima mkipitishe kwenye moto, kisha kitakuwa safi. Lakini ni lazima pia kitakaswe kwa maji ya utakaso. Kitu chochote kisichoweza kuhimili moto lazima kipitishwe kwenye yale maji ya utakaso.
24 And ye shall wash your clothes on the seventh day, and ye shall be clean, and afterward ye may come into the camp.'
Katika siku ya saba fueni nguo zenu, nanyi mtakuwa safi. Kisha mtaweza kuingia kambini.”
25 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
26 'Take the sum of the prey that was taken, both of man and of beast, thou, and Eleazar the priest, and the heads of the fathers' houses of the congregation;
“Wewe na kuhani Eleazari pamoja na viongozi wa jamaa ya jumuiya mtahesabu watu wote na wanyama ambao walitekwa.
27 and divide the prey into two parts: between the men skilled in war, that went out to battle, and all the congregation;
Gawanyeni hizo nyara kati ya askari ambao walishiriki katika vita na kwa jumuiya.
28 and levy a tribute unto the LORD of the men of war that went out to battle: one soul of five hundred, both of the persons, and of the beeves, and of the asses, and of the flocks;
Kutoka fungu la wale waliokwenda kupigana vitani, tenga kama ushuru kwa ajili ya Bwana kitu kimoja kati ya kila mia tano, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo au mbuzi.
29 take it of their half, and give it unto Eleazar the priest, as a portion set apart for the LORD.
Chukua ushuru huu kutoka fungu lao, umpe kuhani Eleazari kama sehemu ya Bwana.
30 And of the children of Israel's half, thou shalt take one drawn out of every fifty, of the persons, of the beeves, of the asses, and of the flocks, even of all the cattle, and give them unto the Levites, that keep the charge of the tabernacle of the LORD.'
Kutoka fungu la Waisraeli, chukua kitu kimoja kati ya kila hamsini, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo, mbuzi au wanyama wengine. Hivyo uwape Walawi, ambao wanawajibika kutunza Maskani ya Bwana.”
31 And Moses and Eleazar the priest did as the LORD commanded Moses.
Kwa hiyo Mose na kuhani Eleazari wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.
32 Now the prey, over and above the booty which the men of war took, was six hundred thousand and seventy thousand and five thousand sheep,
Nyara zilizobaki kutoka mateka ambayo askari walichukua ni kondoo 675,000,
33 and threescore and twelve thousand beeves,
ngʼombe 72,000,
34 and threescore and one thousand asses,
punda 61,000,
35 and thirty and two thousand persons in all, of the women that had not known man by lying with him.
na wanawake 32,000 ambao hawakumjua mume kwa kufanya tendo la ndoa.
36 And the half, which was the portion of them that went out to war, was in number three hundred thousand and thirty thousand and seven thousand and five hundred sheep.
Nusu ya fungu la wale waliokwenda kupigana vitani lilikuwa: Kondoo 337,500
37 And the LORD'S tribute of the sheep was six hundred and threescore and fifteen.
ambayo ushuru kwa ajili ya Bwana ilikuwa kondoo 675;
38 And the beeves were thirty and six thousand, of which the LORD'S tribute was threescore and twelve.
ngʼombe 36,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa ngʼombe 72;
39 And the asses were thirty thousand and five hundred, of which the LORD'S tribute was threescore and one.
punda 30,500 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa punda 61;
40 And the persons were sixteen thousand, of whom the LORD'S tribute was thirty and two persons.
Watu 16,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa watu 32.
41 And Moses gave the tribute, which was set apart for the LORD, unto Eleazar the priest, as the LORD commanded Moses.
Mose alimpa kuhani Eleazari ushuru kama sehemu ya Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
42 And of the children of Israel's half, which Moses divided off from the men that warred —
Ile nusu iliyokuwa ya Waisraeli, ambayo Mose aliitenga kutoka kwa ile ya watu waliokwenda vitani,
43 now the congregation's half was three hundred thousand and thirty thousand and seven thousand and five hundred sheep,
nusu iliyokuwa ya jumuiya, ilikuwa kondoo 337,500,
44 and thirty and six thousand beeves,
ngʼombe 36,000,
45 and thirty thousand and five hundred asses,
punda 30,500,
46 and sixteen thousand persons —
na wanadamu 16,000.
47 even of the children of Israel's half, Moses took one drawn out of every fifty, both of man and of beast, and gave them unto the Levites, that kept the charge of the tabernacle of the LORD; as the LORD commanded Moses.
Kutoka hiyo nusu iliyokuwa ya Waisraeli, Mose alichagua moja kati ya kila hamsini ya wanadamu na wanyama, kama Bwana alivyomwagiza, naye aliwapa Walawi, ambao waliwajibika kutunza Maskani ya Bwana.
48 And the officers that were over the thousands of the host, the captains of thousands, and the captains of hundreds, came near unto Moses;
Kisha maafisa waliokuwa juu ya vikosi vya jeshi, wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, walimwendea Mose
49 and they said unto Moses: 'Thy servants have taken the sum of the men of war that are under our charge, and there lacketh not one man of us.
na kumwambia, “Watumishi wako wamehesabu askari walio chini ya amri yetu na hakuna hata mmoja aliyekosekana.
50 And we have brought the LORD'S offering, what every man hath gotten, of jewels of gold, armlets, and bracelets, signet-rings, ear-rings, and girdles, to make atonement for our souls before the LORD.'
Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”
51 And Moses and Eleazar the priest took the gold of them, even all wrought jewels.
Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa.
52 And all the gold of the gift that they set apart for the LORD, of the captains of thousands, and of the captains of hundreds, was sixteen thousand seven hundred and fifty shekels. —
Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,750
53 For the men of war had taken booty, every man for himself. —
Kila askari alikuwa amejichukulia nyara zake binafsi.
54 And Moses and Eleazar the priest took the gold of the captains of thousands and of hundreds, and brought it into the tent of meeting, for a memorial for the children of Israel before the LORD.
Mose na kuhani Eleazari walipokea dhahabu kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, wakazileta katika Hema la Kukutania kama ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana.

< Numbers 31 >