< Numbers 20 >

1 And the children of Israel, even the whole congregation, came into the wilderness of Zin in the first month; and the people abode in Kadesh; and Miriam died there, and was buried there.
Katika mwezi wa kwanza jumuiya yote ya Kiisraeli ilifika kwenye Jangwa la Sini, nao wakakaa Kadeshi. Miriamu akafa huko na kuzikwa.
2 And there was no water for the congregation; and they assembled themselves together against Moses and against Aaron.
Mahali hapo hapakuwa na maji kwa ajili ya jumuiya hiyo, nao wakakusanyika ili kumpinga Mose na Aroni.
3 And the people strove with Moses, and spoke, saying: 'Would that we had perished when our brethren perished before the LORD!
Watu wakagombana na Mose, na kusema, “Laiti tungelikufa wakati ndugu zetu walipoanguka na kufa mbele za Bwana!
4 And why have ye brought the assembly of the LORD into this wilderness, to die there, we and our cattle?
Kwa nini mmeileta jumuiya ya Bwana kwenye jangwa hili, ili tufe humu, sisi na mifugo yetu?
5 And wherefore have ye made us to come up out of Egypt, to bring us in unto this evil place? it is no place of seed, or of figs, or of vines, or of pomegranates; neither is there any water to drink.'
Kwa nini mmetupandisha kutoka Misri mpaka mahali hapa pa kutisha? Hapa hakuna nafaka wala tini, zabibu au makomamanga. Wala hapa hakuna maji ya kunywa!”
6 And Moses and Aaron went from the presence of the assembly unto the door of the tent of meeting, and fell upon their faces; and the glory of the LORD appeared unto them.
Mose na Aroni wakaondoka pale kwenye kusanyiko mpaka kwenye mlango wa Hema la Kukutania na kuanguka kifudifudi, nao utukufu wa Bwana ukawatokea.
7 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
8 'Take the rod, and assemble the congregation, thou, and Aaron thy brother, and speak ye unto the rock before their eyes, that it give forth its water; and thou shalt bring forth to them water out of the rock; so thou shalt give the congregation and their cattle drink.'
“Chukua ile fimbo, na wewe na ndugu yako Aroni mkusanye kusanyiko pamoja. Nena na ule mwamba mbele ya macho yao, nao utatoa maji yake. Utatoa maji kutoka huo mwamba kwa ajili ya jumuiya ili wao na mifugo yao waweze kunywa.”
9 And Moses took the rod from before the LORD, as He commanded him.
Kwa hiyo Mose akaichukua hiyo fimbo kutoka pale ilipokuwa mbele za Bwana kama alivyomwagiza.
10 And Moses and Aaron gathered the assembly together before the rock, and he said unto them: 'Hear now, ye rebels; are we to bring you forth water out of this rock?'
Mose na Aroni wakakusanya kusanyiko pamoja mbele ya huo mwamba, naye Mose akawaambia, “Sikilizeni, enyi waasi. Je, ni lazima tuwatoleeni maji kutoka mwamba huu?”
11 And Moses lifted up his hand, and smote the rock with his rod twice; and water came forth abundantly, and the congregation drank, and their cattle.
Ndipo Mose akainua mkono wake na kuupiga mwamba mara mbili kwa fimbo yake. Maji yakabubujika, nayo jumuiya na mifugo yao wakanywa.
12 And the LORD said unto Moses and Aaron: 'Because ye believed not in Me, to sanctify Me in the eyes of the children of Israel, therefore ye shall not bring this assembly into the land which I have given them.'
Lakini Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Kwa sababu hamkuniamini mimi kiasi cha kuniheshimu kama mtakatifu machoni pa Waisraeli, hamtaiingiza jumuiya hii katika nchi ninayowapa.”
13 These are the waters of Meribah, where the children of Israel strove with the LORD, and He was sanctified in them.
Haya yalikuwa maji ya Meriba, mahali pale ambapo Waisraeli waligombana na Bwana, naye akajionyesha mwenyewe huko kuwa mtakatifu katikati yao.
14 And Moses sent messengers from Kadesh unto the king of Edom: 'Thus saith thy brother Israel: Thou knowest all the travail that hath befallen us;
Mose akawatuma wajumbe kutoka Kadeshi kwenda kwa mfalme wa Edomu, akisema: “Hili ndilo ndugu yako Israeli asemalo: Wewe unafahamu juu ya taabu zote ambazo zimetupata.
15 how our fathers went down into Egypt, and we dwelt in Egypt a long time; and the Egyptians dealt ill with us, and our fathers;
Baba zetu walishuka Misri, nasi tumeishi huko miaka mingi. Wamisri walitutesa sisi na baba zetu,
16 and when we cried unto the LORD, He heard our voice, and sent an angel, and brought us forth out of Egypt; and, behold, we are in Kadesh, a city in the uttermost of thy border.
lakini tulipomlilia Bwana, alisikia kilio chetu na akamtuma malaika akatutoa Misri. “Sasa tupo hapa Kadeshi, mji ulio mpakani mwa nchi yako.
17 Let us pass, I pray thee, through thy land; we will not pass through field or through vineyard, neither will we drink of the water of the wells; we will go along the king's highway, we will not turn aside to the right hand nor to the left, until we have passed thy border.'
Tafadhali turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutapita katika shamba lolote, wala shamba la mizabibu, au kunywa maji kutoka kwenye kisima chochote. Tutasafiri kufuata njia kuu ya mfalme, na hatutageuka kulia wala kushoto mpaka tuwe tumeshapita nchi yako.”
18 And Edom said unto him: 'Thou shalt not pass through me, lest I come out with the sword against thee.'
Lakini mfalme wa Edomu akajibu: “Hamtapita hapa; kama mkijaribu kupita, tutatoka na kuwashambulia kwa upanga.”
19 And the children of Israel said unto him: 'We will go up by the highway; and if we drink of thy water, I and my cattle, then will I give the price thereof; let me only pass through on my feet; there is no hurt.'
Waisraeli wakajibu: “Sisi tutafuata njia kuu; tena ikiwa sisi au mifugo yetu tutakunywa tone la maji yenu, tutalilipia. Sisi tunataka tu kupita kwa miguu, wala si kitu kingine chochote.”
20 And he said: 'Thou shalt not pass through.' And Edom came out against him with much people, and with a strong hand.
Watu wa Edomu wakajibu tena: “Hamwezi kupita hapa.” Ndipo watu wa Edomu wakatoka dhidi ya Waisraeli, jeshi kubwa lenye nguvu.
21 Thus Edom refused to give Israel passage through his border; wherefore Israel turned away from him.
Kwa kuwa Waedomu waliwakatalia Waisraeli kupita katika nchi yao, Israeli wakageuka, wakawaacha.
22 And they journeyed from Kadesh; and the children of Israel, even the whole congregation, came unto mount Hor.
Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka kutoka Kadeshi, wakafika kwenye Mlima Hori.
23 And the LORD spoke unto Moses and Aaron in mount Hor, by the border of the land of Edom, saying:
Kwenye Mlima Hori, karibu na mpaka wa Edomu, Bwana akamwambia Mose na Aroni,
24 'Aaron shall be gathered unto his people; for he shall not enter into the land which I have given unto the children of Israel, because ye rebelled against My word at the waters of Meribah.
“Aroni atakusanywa pamoja na watu wake. Hataingia katika nchi ninayowapa Waisraeli, kwa sababu ninyi wawili mliasi dhidi ya agizo langu kwenye maji ya Meriba.
25 Take Aaron and Eleazar his son, and bring them up unto mount Hor.
Watwae Aroni na Eleazari mwanawe, na uwapandishe juu katika Mlima wa Hori.
26 And strip Aaron of his garments, and put them upon Eleazar his son; and Aaron shall be gathered unto his people, and shall die there.'
Mvue Aroni mavazi yake, na umvike Eleazari mwanawe, kwa maana Aroni atakusanywa pamoja na watu wake; atakufa huko.”
27 And Moses did as the LORD commanded; and they went up into mount Hor in the sight of all the congregation.
Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza: Wakapanda Mlima Hori mbele ya macho ya jumuiya yote ya Kiisraeli.
28 And Moses stripped Aaron of his garments, and put them upon Eleazar his son; and Aaron died there in the top of the mount; and Moses and Eleazar came down from the mount.
Mose akamvua Aroni mavazi yake na kumvika mwanawe Eleazari mavazi hayo. Naye Aroni akafia pale juu ya mlima. Kisha Mose na Eleazari wakateremka kutoka mlimani.
29 And when all the congregation saw that Aaron was dead, they wept for Aaron thirty days, even all the house of Israel.
Jumuiya yote ilipofahamu kwamba Aroni amekufa, jamaa yote ya Kiisraeli wakamwomboleza kwa siku thelathini.

< Numbers 20 >