< Leviticus 17 >

1 And the LORD spoke unto Moses, saying:
Bwana akamwambia Mose,
2 Speak unto Aaron, and unto his sons, and unto all the children of Israel, and say unto them: This is the thing which the LORD hath commanded, saying:
“Sema na Aroni na wanawe, pamoja na Waisraeli wote, uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana aliloagiza:
3 What man soever there be of the house of Israel, that killeth an ox, or lamb, or goat, in the camp, or that killeth it without the camp,
Mwisraeli yeyote atakayetoa dhabihu ya maksai, mwana-kondoo au mbuzi ndani ya kambi au nje yake,
4 and hath not brought it unto the door of the tent of meeting, to present it as an offering unto the LORD before the tabernacle of the LORD, blood shall be imputed unto that man; he hath shed blood; and that man shall be cut off from among his people.
badala ya kuileta kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili kuileta kama sadaka kwa Bwana mbele ya Maskani ya Bwana, mtu huyo atahesabiwa kuwa na hatia ya kumwaga damu; ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
5 To the end that the children of Israel may bring their sacrifices, which they sacrifice in the open field, even that they may bring them unto the LORD, unto the door of the tent of meeting, unto the priest, and sacrifice them for sacrifices of peace-offerings unto the LORD.
Hii ni ili Waisraeli wamletee Bwana dhabihu wanazozifanya sasa mahali pa wazi mashambani. Ni lazima wazilete kwa makuhani, yaani kwa Bwana, katika ingilio la Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu kama sadaka za amani.
6 And the priest shall dash the blood against the altar of the LORD at the door of the tent of meeting, and make the fat smoke for a sweet savour unto the LORD.
Kuhani atanyunyiza damu kwenye madhabahu ya Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania, na kuyateketeza mafuta ya hiyo dhabihu kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
7 And they shall no more sacrifice their sacrifices unto the satyrs, after whom they go astray. This shall be a statute for ever unto them throughout their generations.
Hawatatoa kamwe dhabihu zao kwa sanamu za mbuzi ambazo wamekuwa wakijifanyia nazo ukahaba. Hili litakuwa agizo la kudumu kwao na kwa ajili ya vizazi vijavyo.’
8 And thou shalt say unto them: Whatsoever man there be of the house of Israel, or of the strangers that sojourn among them, that offereth a burnt-offering or sacrifice,
“Waambie: ‘Mwisraeli yeyote au mgeni yeyote anayeishi miongoni mwao atakayetoa sadaka ya kuteketezwa au dhabihu
9 and bringeth it not unto the door of the tent of meeting, to sacrifice it unto the LORD, even that man shall be cut off from his people.
bila kuileta kwenye ingilio la Hema la Kukutania ili kutoa dhabihu kwa Bwana, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake.
10 And whatsoever man there be of the house of Israel, or of the strangers that sojourn among them, that eateth any manner of blood, I will set My face against that soul that eateth blood, and will cut him off from among his people.
“‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi miongoni mwao ambaye atakunywa damu yoyote, nitakuwa kinyume cha mtu huyo atakayekunywa damu na kumkatilia mbali na watu wake.
11 For the life of the flesh is in the blood; and I have given it to you upon the altar to make atonement for your souls; for it is the blood that maketh atonement by reason of the life.
Kwa kuwa uhai wa kiumbe uko ndani ya damu, nami nimewapa hiyo damu ili mfanyie upatanisho kwa ajili yenu wenyewe juu ya madhabahu; damu ndiyo ifanyayo upatanisho kwa ajili ya maisha ya mtu.
12 Therefore I said unto the children of Israel: No soul of you shall eat blood, neither shall any stranger that sojourneth among you eat blood.
Kwa hiyo, ninawaambia Waisraeli, “Hakuna hata mmoja wenu anayeruhusiwa kunywa damu, wala mgeni anayeishi miongoni mwenu haruhusiwi kunywa damu.”
13 And whatsoever man there be of the children of Israel, or of the strangers that sojourn among them, that taketh in hunting any beast or fowl that may be eaten, he shall pour out the blood thereof, and cover it with dust.
“‘Mwisraeli yeyote au mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye atamwinda mnyama au ndege anayeruhusiwa kuliwa ni lazima aimwage damu na kuifunika kwa udongo,
14 For as to the life of all flesh, the blood thereof is all one with the life thereof; therefore I said unto the children of Israel: Ye shall eat the blood of no manner of flesh; for the life of all flesh is the blood thereof; whosoever eateth it shall be cut off.
kwa sababu uhai wa kila kiumbe ni katika damu yake. Ndiyo sababu nimewaambia Waisraeli, “Kamwe msinywe damu ya kiumbe chochote, kwa sababu uhai wa kila kiumbe ni katika damu yake; yeyote atakayekunywa damu ni lazima akatiliwe mbali.”
15 And every soul that eateth that which dieth of itself, or that which is torn of beasts, whether he be home-born or a stranger, he shall wash his clothes, and bathe himself in water, and be unclean until the even; then shall he be clean.
“‘Mtu yeyote, awe mzawa au mgeni, ambaye atakula mzoga wa kitu chochote ama kilichouawa na wanyama mwitu ni lazima afue nguo zake na aoge kwa maji, naye atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni, kisha atakuwa safi.
16 But if he wash them not, nor bathe his flesh, then he shall bear his iniquity.
Lakini kama hakufua nguo zake na kuoga, atakuwa na hatia kwa kosa hilo.’”

< Leviticus 17 >