< Joshua 21 >

1 Then came near the heads of fathers' houses of the Levites unto Eleazar the priest, and unto Joshua the son of Nun, and unto the heads of fathers' houses of the tribes of the children of Israel;
Basi viongozi wa jamaa ya Walawi, wakamwendea kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa jamaa nyingine za makabila ya Israeli
2 and they spoke unto them at Shiloh in the land of Canaan, saying: 'The LORD commanded by the hand of Moses to give us cities to dwell in, with the open land thereabout for our cattle.'
huko Shilo katika Kanaani na kuwaambia, “Bwana aliamuru kupitia Mose kuwa mtupe miji ya kuishi yenye sehemu za malisho kwa mifugo yetu.”
3 And the children of Israel gave unto the Levites out of their inheritance, according to the commandment of the LORD, these cities with the open land about them.
Hivyo kama vile Bwana alivyoamuru, Waisraeli wakawapa Walawi miji ifuatayo pamoja na sehemu zake za malisho kutoka urithi wao wenyewe.
4 And the lot came out for the families of the Kohathites; and the children of Aaron the priest, who were of the Levites, had by lot out of the tribe of Judah, and out of the tribe of the Simeonites, and out of the tribe of Benjamin, thirteen cities.
Kura ya kwanza ikaangukia Wakohathi, ukoo kwa ukoo. Walawi waliokuwa wazao wa kuhani Aroni walipewa miji kumi na mitatu kutoka makabila ya Yuda, Simeoni na Benyamini.
5 And the rest of the children of Kohath had by lot out of the families of the tribe of Ephraim, and out of the tribe of Dan, and out of the half-tribe of Manasseh, ten cities.
Wazao wengine waliobaki wa Wakohathi walipewa miji kumi kutoka koo za makabila ya Efraimu, Dani na nusu ya Manase.
6 And the children of Gershon had by lot out of the families of the tribe of Issachar, and out of the tribe of Asher, and out of the tribe of Naphtali, and out of the half-tribe of Manasseh in Bashan, thirteen cities.
Wazao wa Gershoni walipewa miji kumi na mitatu kutoka koo za makabila ya Isakari, Asheri, Naftali na nusu ya Manase huko Bashani.
7 The children of Merari according to their families had out of the tribe of Reuben, and out of the tribe of Gad, and out of the tribe of Zebulun, twelve cities.
Wazao wa Merari, ukoo kwa ukoo, walipewa miji kumi na miwili kutoka makabila ya Reubeni, Gadi na Zabuloni.
8 And the children of Israel gave by lot unto the Levites these cities with the open land about them, as the LORD commanded by the hand of Moses.
Kwa hiyo Waisraeli wakawapa Walawi miji hii pamoja na sehemu zake za malisho, kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru kupitia kwa Mose.
9 And they gave out of the tribe of the children of Judah, and out of the tribe of the children of Simeon, these cities which are here mentioned by name.
Kutoka makabila ya Yuda na Simeoni waligawa miji ifuatayo kwa majina
10 And they were for the children of Aaron, of the families of the Kohathites, who were of the children of Levi; for theirs was the first lot.
(miji hii walipewa wazao wa Aroni ambao walitokana na koo za Wakohathi wa Walawi, kwa sababu kura ya kwanza iliwaangukia):
11 And they gave them Kiriath-arba, which Arba was the father of Anak — the same is Hebron — in the hill-country of Judah, with the open land round about it.
Waliwapa Kiriath-Arba (yaani Hebroni), pamoja na sehemu zake za malisho zilizoizunguka, katika nchi ya vilima ya Yuda. (Arba alikuwa baba wa Anaki.)
12 But the fields of the city, and the villages thereof, gave they to Caleb the son of Jephunneh for his possession.
Lakini mashamba na vijiji vilivyozunguka mji mkubwa walikuwa wamempa Kalebu mwana wa Yefune kuwa milki yake.
13 And unto the children of Aaron the priest they gave Hebron with the open land about it, the city of refuge for the manslayer, and Libnah with the open land about it;
Kwa hiyo wazao wa kuhani Aroni wakapewa Hebroni (mji mkuu wa makimbilio kwa ajili ya yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji), Libna,
14 and Jattir with the open land about it, and Eshtemoa with the open land about it;
Yatiri, Eshtemoa,
15 and Holon with the open land about it, and Debir with the open land about it;
Holoni, Debiri,
16 and Ain with the open land about it, and Juttah with the open land about it, and Beth-shemesh with the open land about it; nine cities out of those two tribes.
Aini, Yuta na Beth-Shemeshi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji tisa kutoka kwa makabila haya mawili.
17 And out of the tribe of Benjamin, Gibeon with the open land about it, Geba with the open land about it;
Kutoka kabila la Benyamini wakawapa Gibeoni, Geba,
18 Anathoth with the open land about it, and Almon with the open land about it; four cities.
Anathothi na Almoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
19 All the cities of the children of Aaron, the priests, were thirteen cities with the open land about them.
Miji yote waliyopewa makuhani, wazao wa Aroni, ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
20 And the families of the children of Kohath, the Levites, even the rest of the children of Kohath, they had the cities of their lot out of the tribe of Ephraim.
Koo nyingine za Wakohathi, ambao pia ni Walawi, walipewa miji kutoka kabila la Efraimu:
21 And they gave them Shechem with the open land about it in the hill-country of Ephraim, the city of refuge for the manslayer, and Gezer with the open land about it;
Katika nchi ya vilima ya Efraimu walipewa Shekemu (mji mkubwa wa makimbilio kwa yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji) na Gezeri,
22 and Kibzaim with the open land about it, and Beth-horon with the open land about it; four cities.
Kibsaimu na Beth-Horoni, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
23 And out of the tribe of Dan, Elteke with the open land about it, Gibbethon with the open land about it;
Pia kutoka kabila la Dani wakapokea Elteke, Gibethoni,
24 Aijalon with the open land about it, Gath-rimmon with the open land about it; four cities.
Aiyaloni na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
25 And out of the half-tribe of Manasseh, Taanach with the open land about it, and Gath-rimmon with the open land about it; two cities.
Kutoka nusu ya kabila la Manase, wakapokea Taanaki na Gath-Rimoni pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili.
26 All the cities of the families of the rest of the children of Kohath were ten with the open land about them.
Miji yote hii kumi pamoja na sehemu zake za malisho ilipewa koo za Wakohathi zilizobaki.
27 And unto the children of Gershon, of the families of the Levites, out of the half-tribe of Manasseh they gave Golan in Bashan with the open land about it, the city of refuge for the manslayer; and Beeshterah with the open land about it; two cities.
Koo za Walawi za Wagershoni walipewa: kutoka nusu ya kabila la Manase, Golani katika Bashani (mji mkuu wa makimbilio kwa yeyote aliyeshtakiwa kwa mauaji) na Beeshtera, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji miwili;
28 And out of the tribe of Issachar, Kishion with the open land about it, Dobrath with the open land about it;
kutoka kabila la Isakari walipewa, Kishioni, Daberathi,
29 Jarmuth with the open land about it, En-gannim with the open land about it; four cities.
Yarmuthi na En-Ganimu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne
30 And out of the tribe of Asher, Mishal with the open land about it, Abdon with the open land about it;
kutoka kabila la Asheri walipewa, Mishali, Abdoni,
31 Helkath with the open land about it, and Rehob with the open land about it; four cities.
Helkathi na Rehobu, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
32 And out of the tribe of Naphtali, Kedesh in Galilee with the open land about it, the city of refuge for the manslayer, and Hammoth-dor with the open land about it, and Kartan with the open land about it; three cities.
Kutoka kabila la Naftali walipewa, Kedeshi katika Galilaya (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa mauaji), Hamoth-Dori na Kartani, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji mitano.
33 All the cities of the Gershonites according to their families were thirteen cities with the open land about them.
Miji yote ya koo za Wagershoni ilikuwa kumi na mitatu, pamoja na sehemu zake za malisho.
34 And unto the families of the children of Merari, the rest of the Levites, out of the tribe of Zebulun, Jokneam with the open land about it, and Kartah with the open land about it;
Koo za Wamerari (Walawi waliobaki) walipewa: kutoka kabila la Zabuloni, Yokneamu, Karta,
35 Dimnah with the open land about it, Nahalal with the open land about it; four cities.
Dimna na Nahalali, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
36 And out of the tribe of Reuben, Bezer with the open land about it, and Jahaz with the open land about it;
kutoka kabila la Reubeni walipewa Bezeri, Yahasa,
37 Kedemoth with the open land about it, and Mephaath with the open land about it; four cities.
Kedemothi na Mefaathi, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne;
38 And out of the tribe of Gad, Ramoth in Gilead with the open land about it, the city of refuge for the manslayer, and Mahanaim with the open land about it;
kutoka kabila la Gadi walipewa, Ramothi katika Gileadi (mji wa makimbilio kwa ajili ya yeyote anayeshtakiwa kwa ajili ya mauaji), Mahanaimu,
39 Heshbon with the open land about it, Jazer with the open land about it; four cities in all.
Heshboni na Yazeri, pamoja na sehemu zake za malisho, ilikuwa miji minne.
40 All these were the cities of the children of Merari according to their families, even the rest of the families of the Levites; and their lot was twelve cities.
Miji yote waliyopewa koo za Wamerari, waliokuwa mabaki ya Walawi, ilikuwa ni kumi na miwili.
41 All the cities of the Levites — forty and eight cities with the open land about them — shall be in the midst of the possession of the children of Israel,
Miji yote ya Walawi katika eneo lililoshikwa na Waisraeli lilikuwa arobaini na minane, pamoja na sehemu zake za malisho.
42 even these cities, every one with the open land round about it; thus it shall be with all these cities.
Kila mmoja wa miji hii ulikuwa na sehemu ya malisho kuuzunguka; ndivyo ilivyokuwa kwa miji hii yote.
43 So the LORD gave unto Israel all the land which He swore to give unto their fathers; and they possessed it, and dwelt therein.
Kwa hiyo Bwana akawapa Israeli nchi yote aliyokuwa ameapa kuwapa baba zao, nao wakaimiliki na kukaa humo.
44 And the LORD gave them rest round about, according to all that He swore unto their fathers; and there stood not a man of all their enemies against them; the LORD delivered all their enemies into their hand.
Bwana akawapa pumziko kila upande, kama vile alivyokuwa amewaapia baba zao, hakuna hata mmoja wa adui zao aliyeweza kusimama mbele yao, Bwana akawatia adui zao wote mikononi mwao.
45 There failed not aught of any good thing which the LORD had spoken unto the house of Israel; all came to pass.
Hakuna hata mojawapo ya ahadi nzuri ya Bwana kwa nyumba ya Israeli ambayo haikutimia; kila moja ilitimia.

< Joshua 21 >