< Jonah 3 >

1 And the word of the LORD came unto Jonah the second time, saying:
Ndipo neno la Bwana likamjia Yona mara ya pili:
2 'Arise, go unto Nineveh, that great city, and make unto it the proclamation that I bid thee.'
“Ondoka uende katika mji mkubwa wa Ninawi, ukautangazie ujumbe ninaokupa.”
3 So Jonah arose, and went unto Nineveh, according to the word of the LORD. Now Nineveh was an exceeding great city, of three days' journey.
Yona akalitii neno la Bwana naye akaenda Ninawi. Basi Ninawi ulikuwa mji maarufu sana, ilichukua siku tatu kuuzunguka.
4 And Jonah began to enter into the city a day's journey, and he proclaimed, and said: 'Yet forty days, and Nineveh shall be overthrown.'
Siku ya kwanza, Yona aliingia mjini. Akatangaza: “Baada ya siku arobaini Ninawi utaangamizwa.”
5 And the people of Nineveh believed God; and they proclaimed a fast, and put on sackcloth, from the greatest of them even to the least of them.
Watu wa Ninawi wakamwamini Mungu, wakatangaza kufunga, watu wote kuanzia mkubwa sana hadi yule mdogo kabisa, wakavaa nguo za gunia.
6 And the tidings reached the king of Nineveh, and he arose from his throne, and laid his robe from him, and covered him with sackcloth, and sat in ashes.
Habari zilipomfikia mfalme wa Ninawi, aliondoka kwenye kiti chake cha enzi, akavua majoho yake ya kifalme, akajifunika nguo ya gunia kisha akaketi chini mavumbini.
7 And he caused it to be proclaimed and published through Nineveh by the decree of the king and his nobles, saying: 'Let neither man nor beast, herd nor flock, taste any thing; let them not feed, nor drink water;
Ndipo akatoa tangazo katika Ninawi yote: “Kwa amri ya mfalme na wakuu wake: “Msiruhusu mtu yeyote au mnyama, makundi ya ngʼombe au wanyama wengine wafugwao, kuonja kitu chochote, msiwaruhusu kula wala kunywa.
8 but let them be covered with sackcloth, both man and beast, and let them cry mightily unto God; yea, let them turn every one from his evil way, and from the violence that is in their hands.
Bali wanadamu na wanyama wafunikwe kwa nguo za gunia. Kila mmoja afanye hima kumwomba Mungu. Waziache njia zao mbaya na udhalimu ulio mikononi mwao.
9 Who knoweth whether God will not turn and repent, and turn away from His fierce anger, that we perish not?'
Ni nani ajuaye? Huenda Mungu akaghairi kwa huruma yake akaacha hasira yake kali ili tusiangamie.”
10 And God saw their works, that they turned from their evil way; and God repented of the evil, which He said He would do unto them; and He did it not.
Mungu alipoona walivyofanya na jinsi walivyogeuka kutoka njia zao mbaya, akawa na huruma wala hakuleta maangamizi juu yao kama alivyokuwa ameonya.

< Jonah 3 >