< Jonah 1 >

1 NOW THE WORD of the LORD came unto Jonah the son of Amittai, saying:
Neno la Bwana lilimjia Yona mwana wa Amitai:
2 'Arise, go to Nineveh, that great city, and proclaim against it; for their wickedness is come up before Me.'
“Nenda katika mji mkubwa wa Ninawi ukahubiri juu yake, kwa sababu uovu wake umekuja juu mbele zangu.”
3 But Jonah rose up to flee unto Tarshish from the presence of the LORD; and he went down to Joppa, and found a ship going to Tarshish; so he paid the fare thereof, and went down into it, to go with them unto Tarshish, from the presence of the LORD.
Lakini Yona alimkimbia Bwana na kuelekea Tarshishi. Alishuka mpaka Yafa, ambapo alikuta meli iliyokuwa imepangwa kuelekea bandari ile. Baada ya kulipa nauli, akapanda melini na kuelekea Tarshishi ili kumkimbia Bwana.
4 But the LORD hurled a great wind into the sea, and there was a mighty tempest in the sea, so that the ship was like to be broken.
Ndipo Bwana akatuma upepo mkali baharini, nayo dhoruba kali sana ikavuma hata meli ikawa hatarini kuvunjika.
5 And the mariners were afraid, and cried every man unto his god; and they cast forth the wares that were in the ship into the sea, to lighten it unto them. But Jonah was gone down into the innermost parts of the ship; and he lay, and was fast asleep.
Mabaharia wote waliogopa na kila mmoja akamlilia mungu wake mwenyewe. Nao wakatupa mizigo baharini ili meli ipungue uzito. Lakini Yona alikuwa ameteremkia chumba cha ndani ya meli, mahali ambapo alilala na kupatwa na usingizi mzito.
6 So the shipmaster came to him, and said unto him: 'What meanest thou that thou sleepest? arise, call upon thy God, if so be that God will think upon us, that we perish not.'
Nahodha akamwendea na kusema, “Wewe unawezaje kulala? Amka ukamwite mungu wako! Huenda akatuangalia, tusiangamie.”
7 And they said every one to his fellow: 'Come, and let us cast lots, that we may know for whose cause this evil is upon us.' So they cast lots, and the lot fell upon Jonah.
Kisha mabaharia wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tupige kura tumtafute anayehusika na maafa haya.” Wakapiga kura, kura ikamwangukia Yona.
8 Then said they unto him: 'Tell us, we pray thee, for whose cause this evil is upon us: what is thine occupation? and whence comest thou? what is thy country? and of what people art thou?'
Kwa hiyo walimuuliza, “Tuambie, ni nani anayehusika kwa kutuletea tatizo hili lote? Unafanya kazi gani? Umetoka wapi? Nchi yako ni ipi? Wewe ni kutoka taifa lipi?”
9 And he said unto them: 'I am an Hebrew; and I fear the LORD, the God of heaven, who hath made the sea and the dry land.'
Akajibu, “Mimi ni Mwebrania, nami namwabudu Bwana, Mungu wa Mbinguni, aliyeumba bahari na nchi kavu.”
10 Then were the men exceedingly afraid, and said unto him: 'What is this that thou hast done?' For the men knew that he fled from the presence of the LORD, because he had told them.
Hili liliwaogopesha nao wakamuuliza, “Umefanya nini?” (Walijua alikuwa anamkimbia Bwana, kwa sababu alishawaambia hivyo.)
11 Then said they unto him: 'What shall we do unto thee, that the sea may be calm unto us?' for the sea grew more and more tempestuous.
Bahari ilikuwa inazidi kuchafuka. Kwa hiyo walimuuliza, “Tukutendee nini ili kufanya bahari itulie kwa ajili yetu?”
12 And he said unto them: 'Take me up, and cast me forth into the sea; so shall the sea be calm unto you; for I know that for my sake this great tempest is upon you.'
Akawajibu, “Niinueni mnitupe baharini, nayo itakuwa shwari. Ninajua mawimbi haya makubwa yamewatokea kwa ajili ya kosa langu.”
13 Nevertheless the men rowed hard to bring it to the land; but they could not; for the sea grew more and more tempestuous against them.
Badala yake, wale watu walijitahidi kupiga makasia wawezavyo ili wapate kurudi pwani. Lakini hawakuweza, kwa kuwa bahari ilizidi kuchafuka kuliko mwanzo.
14 Wherefore they cried unto the LORD, and said: 'We beseech Thee, O LORD, we beseech Thee, let us not perish for this man's life, and lay not upon us innocent blood; for Thou, O LORD, hast done as it pleased Thee.'
Ndipo wakamlilia Bwana, “Ee Bwana, tafadhali usituue kwa kuondoa uhai wa mtu huyu. Usituhesabie hatia kwa kuutoa uhai wa mtu asiyekuwa na hatia, kwa kuwa wewe, Ee Bwana, umefanya kama ilivyokupendeza.”
15 So they took up Jonah, and cast him forth into the sea; and the sea ceased from its raging.
Kisha walimchukua Yona, wakamtupa baharini nayo bahari iliyokuwa imechafuka ikatulia.
16 Then the men feared the LORD exceedingly; and they offered a sacrifice unto the LORD, and made vows.
Katika jambo hili watu wakamwogopa Bwana sana, wakamtolea Bwana dhabihu na kumwekea nadhiri.
17 And the LORD prepared a great fish to swallow up Jonah; and Jonah was in the belly of the fish three days and three nights.
Lakini Bwana akamwandaa nyangumi kummeza Yona, naye Yona alikuwa ndani ya tumbo la nyangumi kwa siku tatu, usiku na mchana.

< Jonah 1 >