< Job 28 >

1 For there is a mine for silver, and a place for gold which they refine.
“Kuna machimbo ya fedha, na mahali dhahabu isafishwapo.
2 Iron is taken out of the dust, and brass is molten out of the stone.
Chuma hupatikana ardhini, nayo shaba huyeyushwa kutoka mawe ya madini.
3 Man setteth an end to darkness, and searcheth out to the furthest bound the stones of thick darkness and of the shadow of death.
Mwanadamu hukomesha giza; huyatafuta hadi sehemu iliyo mbali, kwa ajili ya kuchimbua mawe yenye madini katika giza jeusi sana.
4 He breaketh open a shaft away from where men sojourn; they are forgotten of the foot that passeth by; they hang afar from men, they swing to and fro.
Huchimba shimo jembamba mbali na makao ya watu, mahali paliposahaulika na nyayo za wanadamu; mbali na wanadamu huningʼinia na kupembea kwa kamba.
5 As for the earth, out of it cometh bread, and underneath it is turned up as it were by fire.
Ardhi, ambako chakula hutoka, chini hugeuzwa kwa moto;
6 The stones thereof are the place of sapphires, and it hath dust of gold.
yakuti samawi hutoka katika miamba yake, nalo vumbi lake lina vipande vya dhahabu.
7 That path no bird of prey knoweth, neither hath the falcon's eye seen it;
Hakuna ndege awindaye aijuaye njia ile iliyofichika, wala hakuna jicho la mwewe lililoiona.
8 The proud beasts have not trodden it, nor hath the lion passed thereby.
Wanyama wa porini wanaotamba hawajawahi kupakanyaga, wala simba azungukaye huko.
9 He putteth forth his hand upon the flinty rock; He overturneth the mountains by the roots.
Mikono ya mwanadamu hushambulia miamba migumu sana, na kuiacha wazi mizizi ya milima.
10 He cutteth out channels among the rocks; and his eye seeth every precious thing.
Hutoboa shimo refu la kupenya chini kwa chini kwenye miamba; macho yake huona hazina zake zote.
11 He bindeth the streams that they trickle not; and the thing that is hid bringeth he forth to light.
Hutafuta vyanzo vya mito na kuvileta vitu vilivyofichika katika nuru.
12 But wisdom, where shall it be found? And where is the place of understanding?
“Lakini hekima inaweza kupatikana wapi? Ufahamu unakaa wapi?
13 Man knoweth not the price thereof; neither is it found in the land of the living.
Mwanadamu hatambui thamani yake; haiwezi kupatikana katika nchi ya walio hai.
14 The deep saith: 'It is not in me'; and the sea saith: 'It is not with me.'
Kilindi husema, ‘Haiko ndani yangu’; bahari nayo husema, ‘Haiko pamoja nami.’
15 It cannot be gotten for gold, neither shall silver be weighed for the price thereof.
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi kuliko zote, wala thamani yake haiwezi kupimwa kwa fedha.
16 It cannot be valued with the gold of Ophir, with the precious onyx, or the sapphire.
Haiwezi kununuliwa kwa dhahabu ya Ofiri, kwa shohamu ya thamani kubwa au yakuti samawi ya thamani kubwa.
17 Gold and glass cannot equal it; neither shall the exchange thereof be vessels of fine gold.
Dhahabu wala mawe maangavu haviwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi hubadilishwa na vito vya dhahabu.
18 No mention shall be made of coral or of crystal; yea, the price of wisdom is above rubies.
Marijani na yaspi hazistahili kutajwa; thamani ya hekima ni zaidi ya akiki nyekundu.
19 The topaz of Ethiopia shall not equal it, neither shall it be valued with pure gold.
Yakuti manjano ipatikanayo Kushi haiwezi kulinganishwa nayo, wala haiwezi kununuliwa kwa dhahabu safi.
20 Whence then cometh wisdom? And where is the place of understanding?
“Ni wapi basi hekima itokako? Ufahamu hukaa wapi?
21 Seeing it is hid from the eyes of all living, and kept close from the fowls of the air.
Imefichika machoni pa kila kitu kilicho hai, imesitiriwa hata kwa ndege wa angani.
22 Destruction and Death say: 'We have heard a rumor thereof with our ears.'
Uharibifu na Mauti husema, ‘Ni uvumi wake tu uliotufikia masikioni mwetu.’
23 God understandeth the way thereof, and He knoweth the place thereof.
Mungu anaifahamu njia ya kuiendea hekima na ndiye peke yake anayefahamu inakokaa,
24 For He looketh to the ends of the earth, and seeth under the whole heaven;
kwa maana yeye huitazama miisho ya dunia na huona kila kitu chini ya mbingu.
25 When He maketh a weight for the wind, and meteth out the waters by measure.
Alipofanyiza nguvu za upepo na kuyapima maji,
26 When He made a decree for the rain, and a way for the storm of thunders;
alipofanya maagizo kwa ajili ya mvua na njia kwa ajili ya umeme wa radi,
27 Then did He see it, and declare it; He established it, yea, and searched it out.
ndipo alipoitazama hekima na kuikadiria thamani yake, akaithibitisha na kuihakikisha.
28 And unto man He said: 'Behold, the fear of the Lord, that is wisdom; and to depart from evil is understanding.'
Naye Mungu akamwambia mwanadamu, ‘Kumcha Bwana: hiyo ndiyo hekima, nako kujitenga na uovu ndio ufahamu.’”

< Job 28 >