< Job 16 >

1 Then Job answered and said:
Kisha Ayubu akajibu:
2 I have heard many such things; sorry comforters are ye all.
“Nimepata kusikia mambo mengi kama haya, nanyi nyote ni wafariji wenye kutaabisha!
3 Shall windy words have an end? Or what provoketh thee that thou answerest?
Je, maneno yenu mengi yasiyo na maana hayana mwisho? Mna nini hata mwendelee kushindana kwa maneno?
4 I also could speak as ye do; if your soul were in my soul's stead, I could join words together against you, and shake my head at you.
Mimi pia ningeweza kuzungumza kama ninyi, kama mngekuwa katika hali yangu; ningeweza kutoa hotuba nzuri dhidi yenu, na kuwatikisia ninyi kichwa changu.
5 I would strengthen you with my mouth, and the moving of my lips would assuage your grief.
Lakini kinywa changu kingewatia moyo; faraja kutoka midomoni mwangu, ingewaletea nafuu.
6 Though I speak, my pain is not assuaged; and though I forbear, what am I eased?
“Lakini kama nikisema, maumivu yangu bado hayatulizwi; nami kama nikijizuia, wala hayaondoki.
7 But now He hath made me weary; Thou hast made desolate all my company.
Ee Mungu, hakika umenichakaza; umewaangamiza kabisa watu wa nyumbani mwangu wote.
8 And Thou hast shrivelled me up, which is a witness against me; and my leanness riseth up against me, it testifieth to my face.
Umenikunjakunja, nalo limekuwa ushahidi; nako kukonda kwangu kumeongezeka sana na kushuhudia dhidi yangu.
9 He hath torn me in His wrath, and hated me; He hath gnashed upon me with His teeth; mine adversary sharpeneth his eyes upon me.
Mungu amenishambulia na kunirarua katika hasira yake, na kunisagia meno yake; adui yangu hunikazia macho yake makali.
10 They have gaped upon me with their mouth; they have smitten me upon the cheek scornfully; they gather themselves together against me.
Watu wamenifumbulia vinywa vyao kunidhihaki; hunipiga shavuni mwangu kwa dharau, na kuungana pamoja dhidi yangu.
11 God delivereth me to the ungodly, and casteth me into the hands of the wicked.
Mungu amenigeuzia kwa watu wabaya, na kunitupa katika makucha ya waovu.
12 I was at ease, and He broke me asunder; yea, He hath taken me by the neck, and dashed me to pieces; He hath also set me up for His mark.
Mambo yote yalikuwa mazuri, lakini alinivunjavunja; amenikamata shingo na kuniponda. Amenifanya mimi kuwa shabaha yake;
13 His archers compass me round about, He cleaveth my reins asunder, and doth not spare; He poureth out my gall upon the ground.
wapiga upinde wake wananizunguka. Bila huruma, huchoma figo zangu, na kuimwaga nyongo yangu juu ya nchi.
14 He breaketh me with breach upon breach; He runneth upon me like a giant.
Huniponda tena na tena; hunishambulia kama shujaa wa vita.
15 I have sewed sackcloth upon my skin, and have laid my horn in the dust.
“Nimejishonea nguo ya gunia juu ya mwili wangu nami nimekizika kipaji cha uso wangu kwenye vumbi.
16 My face is reddened with weeping, and on my eyelids is the shadow of death;
Uso wangu umekuwa mwekundu kwa kulia, macho yangu yamepigwa na giza kuu.
17 Although there is no violence in my hands, and my prayer is pure.
Hata hivyo mikono yangu haijafanya jeuri, na maombi yangu ni safi.
18 O earth, cover not thou my blood, and let my cry have no resting-place.
“Ee nchi, usiifunike damu yangu, nacho kilio changu kisinyamazishwe kamwe.
19 Even now, behold, my Witness is in heaven, and He that testifieth of me is on high.
Hata sasa shahidi wangu yuko mbinguni; wakili wangu yuko juu.
20 Mine inward thoughts are my intercessors, mine eye poureth out tears unto God;
Mwombezi wangu ni rafiki yangu macho yangu yamwagapo machozi kwa Mungu;
21 That He would set aright a man contending with God, as a son of man setteth aright his neighbour!
kwa niaba ya mtu anamsihi Mungu kama mtu anavyosihi kwa ajili ya rafiki yake.
22 For the years that are few are coming on, and I shall go the way whence I shall not return.
“Ni miaka michache tu itapita kabla sijaenda safari ambayo sitarudi.

< Job 16 >