< Job 12 >

1 Then Job answered and said:
Ndipo Ayubu akajibu:
2 No doubt but ye are the people, and wisdom shall die with you.
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 But I have understanding as well as you; I am not inferior to you; yea, who knoweth not such things as these?
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 I am as one that is a laughing-stock to his neighbour, a man that called upon God, and He answered him; the just, the innocent man is a laughing-stock,
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 A contemptible brand in the thought of him that is at ease, a thing ready for them whose foot slippeth.
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 The tents of robbers prosper, and they that provoke God are secure, in whatsoever God bringeth into their hand.
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 But ask now the beasts, and they shall teach thee; and the fowls of the air, and they shall tell thee;
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 Or speak to the earth, and it shall teach thee; and the fishes of the sea shall declare unto thee;
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 Who knoweth not among all these, that the hand of the LORD hath wrought this?
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 In whose hand is the soul of every living thing, and the breath of all mankind. —
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 Doth not the ear try words, even as the palate tasteth its food?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 Is wisdom with aged men, and understanding in length of days? —
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 With Him is wisdom and might; He hath counsel and understanding.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 Behold, He breaketh down, and it cannot be built again; He shutteth up a man, and there can be no opening.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 Behold, He withholdeth the waters, and they dry up; also He sendeth them out, and they overturn the earth.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 With Him is strength and sound wisdom; the deceived and the deceiver are His.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 He leadeth counsellors away stripped, and judges maketh He fools.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 He looseth the bond of kings, and bindeth their loins with a girdle.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 He leadeth priests away stripped, and overthroweth the mighty.
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 He removeth the speech of men of trust, and taketh away the sense of the elders.
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 He poureth contempt upon princes, and looseth the belt of the strong.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22 He uncovereth deep things out of darkness, and bringeth out to light the shadow of death.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 He increaseth the nations, and destroyeth them; He enlargeth the nations, and leadeth them away.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 He taketh away the heart of the chiefs of the people of the land, and causeth them to wander in a wilderness where there is no way.
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 They grope in the dark without light, and He maketh them to stagger like a drunken man.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.

< Job 12 >