< Job 1 >

1 THERE was a man in the land of Uz, whose name was Job; and that man was whole-hearted and upright, and one that feared God, and shunned evil.
Katika nchi ya Usi paliishi mtu ambaye aliitwa Ayubu. Mtu huyu alikuwa hana hatia, naye alikuwa mkamilifu; alimcha Mungu na kuepukana na uovu.
2 And there were born unto him seven sons and three daughters.
Alikuwa na wana saba na binti watatu,
3 His possessions also were seven thousand sheep, and three thousand camels, and five hundred yoke of oxen, and five hundred she-asses, and a very great household; so that this man was the greatest of all the children of the east.
naye alikuwa na kondoo elfu saba, ngamia elfu tatu, jozi mia tano za maksai, na punda mia tano, tena alikuwa na idadi kubwa ya watumishi. Alikuwa mtu mkuu sana miongoni mwa watu wa Mashariki.
4 And his sons used to go and hold a feast in the house of each one upon his day; and they would send and invite their three sisters to eat and to drink with them.
Wanawe walikuwa na desturi ya kufanya karamu katika nyumba zao kwa zamu, nao wangewaalika umbu zao watatu ili kula na kunywa pamoja nao.
5 And it was so, when the days of their feasting were gone about, that Job sent and sanctified them, and rose up early in the morning, and offered burnt-offerings according to the number of them all; for Job said: 'It may be that my sons have sinned, and blasphemed God in their hearts.' Thus did Job continually.
Wakati kipindi cha karamu kilimalizika, Ayubu angetuma waitwe na kuwafanyia utakaso. Angetoa dhabihu ya sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya kila mmoja wao asubuhi na mapema, akifikiri, “Pengine wanangu wametenda dhambi na kumlaani Mungu mioyoni mwao.” Hii ilikuwa ndiyo desturi ya kawaida ya Ayubu.
6 Now it fell upon a day, that the sons of God came to present themselves before the LORD, and Satan came also among them.
Siku moja wana wa Mungu walikwenda kujionyesha mbele za Bwana. Shetani naye akaja pamoja nao.
7 And the LORD said unto Satan: 'Whence comest thou?' Then Satan answered the LORD, and said: 'From going to and fro in the earth, and from walking up and down in it.'
Bwana akamwambia Shetani, “Umetoka wapi?” Shetani akamjibu Bwana, “Natoka kuzunguka pote duniani, nikitembea huku na huko humo.”
8 And the LORD said unto Satan: 'Hast thou considered My servant Job, that there is none like him in the earth, a whole-hearted and an upright man, one that feareth God, and shunneth evil?'
Ndipo Bwana akamwambia Shetani, “Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Hakuna mtu mwingine duniani aliye kama yeye, asiye na hatia, ni mnyofu, mwenye kumcha Mungu, na kuepukana na uovu.”
9 Then Satan answered the LORD, and said: 'Doth Job fear God for nought?
Shetani akamjibu Bwana, “Je, Ayubu anamcha Mungu bure?
10 Hast not Thou made a hedge about him, and about his house, and about all that he hath, on every side? Thou hast blessed the work of his hands, and his possessions are increased in the land.
Je, wewe hukumjengea boma pande zote yeye na wa nyumbani mwake pamoja na kila kitu alicho nacho? Kazi za mikono yake umezibariki na hivyo makundi yake ya kondoo na mbuzi pamoja na ya wanyama yameenea katika nchi nzima.
11 But put forth Thy hand now, and touch all that he hath, surely he will blaspheme Thee to Thy face.'
Lakini nyoosha mkono wako na kupiga kila kitu alicho nacho, naye kwa hakika atakulaani mbele za uso wako.”
12 And the LORD said unto Satan: 'Behold, all that he hath is in thy power; only upon himself put not forth thy hand.' So Satan went forth from the presence of the LORD.
Bwana akamwambia Shetani, “Vema sana, kwa hiyo, kila kitu alicho nacho kiko mikononi mwako, lakini juu ya huyo mtu mwenyewe usimguse hata kwa kidole.” Ndipo Shetani akatoka mbele za Bwana.
13 And it fell on a day when his sons and his daughters were eating and drinking wine in their eldest brother's house,
Siku moja watoto wa Ayubu walipokuwa wakifanya karamu wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
14 that there came a messenger unto Job, and said: 'The oxen were plowing, and the asses feeding beside them;
akaja mjumbe kwa Ayubu na kusema, “Maksai walikuwa wakilima na punda walikuwa wakilisha karibu nao,
15 and the Sabeans made a raid, and took them away; yea, they have slain the servants with the edge of the sword; and I only am escaped alone to tell thee.'
Waseba wakawashambulia na kuchukua mifugo. Kisha wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
16 While he was yet speaking, there came also another, and said: 'A fire of God is fallen from heaven, and hath burned up the sheep, and the servants, and consumed them; and I only am escaped alone to tell thee.'
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Moto wa Mungu ulishuka kutoka mbinguni na kuteketeza kondoo na watumishi, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
17 While he was yet speaking, there came also another, and said: 'The Chaldeans set themselves in three bands, and fell upon the camels, and have taken them away, yea, and slain the servants with the edge of the sword; and I only am escaped alone to tell thee.'
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wakaldayo waliunda vikosi vitatu vya uvamizi na kuwaangukia ngamia wako na kuwachukua wakaondoka nao. Wakawaua watumishi kwa upanga, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari.”
18 While he was yet speaking, there came also another, and said: 'Thy sons and thy daughters were eating and drinking wine in their eldest brother's house;
Alipokuwa bado ananena, mjumbe mwingine akaja na kusema, “Wana wako na binti zako walipokuwa wakifanya karamu, wakila na kunywa divai katika nyumba ya ndugu yao mkubwa,
19 And, behold, there came a great wind from across the wilderness, and smote the four corners of the house, and it fell upon the young people, and they are dead; and I only am escaped alone to tell thee.'
ghafula upepo wenye nguvu ukavuma kutoka jangwani, nao ukaipiga nyumba hiyo pembe zake nne. Ikawaangukia hao watoto nao wamekufa, nami ndimi peke yangu niliyenusurika kukuletea habari!”
20 Then Job arose, and rent his mantle, and shaved his head, and fell down upon the ground, and worshipped;
Ndipo Ayubu akasimama, akararua joho lake na kunyoa nywele zake. Kisha akaanguka chini katika kuabudu
21 And he said; naked came I out of my mother's womb, and naked shall I return thither; the LORD gave, and the LORD hath taken away; blessed be the name of the LORD.
na kusema: “Nilitoka tumboni mwa mama yangu uchi, nami nitaondoka uchi, Bwana alinipa, naye Bwana ameviondoa, jina la Bwana litukuzwe.”
22 For all this Job sinned not, nor ascribed aught unseemly to God.
Katika mambo haya yote, Ayubu hakutenda dhambi kwa kumlaumu Mungu kwa kufanya ubaya.

< Job 1 >