< Jeremiah 23 >

1 Woe unto the shepherds that destroy and scatter the sheep of My pasture! saith the LORD.
“Ole wao wachungaji wanaoharibu na kutawanya kondoo wa malisho yangu!” asema Bwana.
2 Therefore thus saith the LORD, the God of Israel, against the shepherds that feed My people: Ye have scattered My flock, and driven them away, and have not taken care of them; behold, I will visit upon you the evil of your doings, saith the LORD.
Kwa hiyo hili ndilo Bwana, Mungu wa Israeli, analowaambia wachungaji wanaowachunga watu wangu: “Kwa sababu mmelitawanya kundi langu na kuwafukuzia mbali, wala hamkuwatunza, basi mimi nitawaadhibu kwa ajili ya uovu mliofanya,” asema Bwana.
3 And I will gather the remnant of My flock out of all the countries whither I have driven them, and will bring them back to their folds; and they shall be fruitful and multiply.
“Mimi mwenyewe nitayakusanya mabaki ya kundi langu kutoka nchi zote ambazo nimewafukuzia, nami nitawarudisha katika malisho yao, mahali ambapo watazaa na kuongezeka idadi yao.
4 And I will set up shepherds over them, who shall feed them; and they shall fear no more, nor be dismayed, neither shall any be lacking, saith the LORD.
Nitaweka wachungaji juu yao ambao watawachunga, nao hawataogopa tena au kutishwa, wala hatapotea hata mmoja,” asema Bwana.
5 Behold, the days come, saith the LORD, that I will raise unto David a righteous shoot, and he shall reign as king and prosper, and shall execute justice and righteousness in the land.
Bwana asema, “Siku zinakuja, nitakapomwinulia Daudi Tawi lenye haki, Mfalme atakayetawala kwa hekima, na kutenda lililo haki na sawa katika nchi.
6 In his days Judah shall be saved, and Israel shall dwell safely; and this is his name whereby he shall be called, The LORD is our righteousness.
Katika siku zake, Yuda ataokolewa na Israeli ataishi salama. Hili ndilo jina atakaloitwa: Bwana Haki Yetu.
7 Therefore, behold, the days come, saith the LORD, that they shall no more say: 'As the LORD liveth, that brought up the children of Israel out of the land of Egypt';
“Hivyo basi, siku zinakuja, wakati ambapo watu hawatasema tena, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewapandisha Waisraeli kutoka Misri,’
8 but: 'As the LORD liveth, that brought up and that led the seed of the house of Israel out of the north country, and from all the countries whither I had driven them'; and they shall dwell in their own land.
bali watasema, ‘Hakika kama Bwana aishivyo, aliyewatoa wazao wa Israeli kutoka nchi ya kaskazini na nchi zote alizokuwa amewafukuzia,’ asema Bwana. Ndipo wataishi katika nchi yao wenyewe.”
9 Concerning the prophets. My heart within me is broken, all my bones shake; I am like a drunken man, and like a man whom wine hath overcome; because of the LORD, and because of His holy words.
Kuhusu manabii: Moyo wangu umevunjika ndani yangu; mifupa yangu yote inatetemeka. Nimekuwa kama mtu aliyelewa, kama mtu aliyelemewa na divai, kwa sababu ya Bwana na maneno yake matakatifu.
10 For the land is full of adulterers; for because of swearing the land mourneth, the pastures of the wilderness are dried up; and their course is evil, and their force is not right.
Nchi imejaa wazinzi; kwa sababu ya laana, nchi imekauka na malisho yaliyoko nyikani yamekauka. Mwenendo wa manabii ni mbaya na mamlaka yao si ya haki.
11 For both prophet and priest are ungodly; yea, in My house have I found their wickedness, saith the LORD.
“Nabii na kuhani wote si wacha Mungu; hata hekaluni mwangu ninaona uovu wao,” asema Bwana.
12 Wherefore their way shall be unto them as slippery places in the darkness, they shall be thrust, and fall therein; for I will bring evil upon them, even the year of their visitation, saith the LORD.
“Kwa hiyo mapito yao yatakuwa utelezi, watafukuziwa mbali gizani na huko wataanguka. Nitaleta maafa juu yao katika mwaka wa kuadhibiwa kwao,” asema Bwana.
13 And I have seen unseemliness in the prophets of Samaria: they prophesied by Baal, and caused My people Israel to err.
“Miongoni mwa manabii wa Samaria nililiona jambo la kuchukiza: Walitabiri kwa Baali na kuwapotosha Israeli watu wangu.
14 But in the prophets of Jerusalem I have seen a horrible thing: they commit adultery, and walk in lies, and they strengthen the hands of evil-doers, that none doth return from his wickedness; they are all of them become unto Me as Sodom, and the inhabitants thereof as Gomorrah.
Nako miongoni mwa manabii wa Yerusalemu nimeona jambo baya sana: Wanafanya uzinzi na kuenenda katika uongo. Wanatia nguvu mikono ya watenda mabaya, kwa ajili hiyo hakuna yeyote anayeachana na uovu wake. Wote wako kama Sodoma kwangu; watu na Yerusalemu wako kama Gomora.”
15 Therefore thus saith the LORD of hosts concerning the prophets: Behold, I will feed them with wormwood, and make them drink the water of gall; for from the prophets of Jerusalem is ungodliness gone forth into all the land.
Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo kuhusu manabii: “Nitawafanya wale chakula kichungu na kunywa maji yaliyotiwa sumu, kwa sababu kutokana na manabii wa Yerusalemu kutokumcha Mungu kumeenea katika nchi yote.”
16 Thus saith the LORD of hosts: Hearken not unto the words of the prophets that prophesy unto you, they lead you unto vanity; they speak a vision of their own heart, and not out of the mouth of the LORD.
Hili ndilo Bwana Mwenye Nguvu Zote asemalo: “Msisikilize wanachowatabiria manabii, wanawajaza matumaini ya uongo. Wanasema maono kutoka akili zao wenyewe, hayatoki katika kinywa cha Bwana.
17 They say continually unto them that despise Me: 'The LORD hath said: Ye shall have peace'; and unto every one that walketh in the stubbornness of his own heart they say: 'No evil shall come upon you';
Huendelea kuwaambia wale wanaonidharau mimi, ‘Bwana asema: Mtakuwa na amani.’ Kwa wale wote wafuatao ugumu wa mioyo yao, wao husema, ‘Hakuna dhara litakalowapata.’
18 For who hath stood in the council of the LORD, that he should perceive and hear His word? Who hath attended to His word, and heard it?
Lakini ni yupi miongoni mwao aliyesimama katika baraza la Bwana ili kuona au kusikia neno lake? Ni nani aliyesikiliza na kusikia neno lake?
19 Behold, a storm of the LORD is gone forth in fury, yea, a whirling storm; it shall whirl upon the head of the wicked.
Tazama, dhoruba ya Bwana itapasuka kwa ghadhabu, kisulisuli kitazunguka na kuanguka vichwani vya waovu.
20 The anger of the LORD shall not return, until He have executed, and till He have performed the purposes of His heart; in the end of days ye shall consider it perfectly.
Hasira ya Bwana haitageuka mpaka amelitimiza kusudi la moyo wake. Siku zijazo mtalifahamu kwa wazi.
21 I have not sent these prophets, yet they ran; I have not spoken to them, yet they prophesied.
Mimi sikuwatuma manabii hawa, lakini bado wamekimbia wakitangaza ujumbe wao. Mimi sikusema nao, lakini wametabiri.
22 But if they have stood in My council, then let them cause My people to hear My words, and turn them from their evil way, and from the evil of their doings.
Lakini kama wangesimama barazani mwangu, wangetangaza maneno yangu kwa watu wangu, nao wangewageuza kutoka njia zao mbaya na kutoka matendo yao maovu.”
23 Am I a God near at hand, saith the LORD, and not a God afar off?
“Je, mimi ni Mungu aliyeko hapa karibu tu,” Bwana asema, “wala si Mungu aliyeko pia mbali?
24 Can any hide himself in secret places that I shall not see him? saith the LORD. Do not I fill heaven and earth? saith the LORD.
Je, mtu yeyote aweza kujificha mahali pa siri ili nisiweze kumwona?” Bwana asema. “Je, mimi sikuijaza mbingu na nchi?” Bwana asema.
25 I have heard what the prophets have said, that prophesy lies in My name, saying: 'I have dreamed, I have dreamed.'
“Nimesikia wanayoyasema manabii, hao wanaotabiri uongo kwa jina langu. Wanasema, ‘Nimeota ndoto! Nimeota ndoto!’
26 How long shall this be? Is it in the heart of the prophets that prophesy lies, and the prophets of the deceit of their own heart?
Mambo haya yataendelea mpaka lini ndani ya mioyo ya hawa manabii wa uongo, ambao hutabiri maono ya uongo ya akili zao wenyewe?
27 That think to cause My people to forget My name by their dreams which they tell every man to his neighbour, as their fathers forgot My name for Baal.
Wanadhani ndoto wanazoambiana wao kwa wao zitawafanya watu wangu walisahau jina langu, kama baba zao walivyolisahau jina langu kwa kumwabudu Baali.
28 The prophet that hath a dream, let him tell a dream; and he that hath My word; let him speak My word faithfully. What hath the straw to do with the wheat? saith the LORD.
Mwache nabii aliye na ndoto aseme ndoto yake, lakini yule aliye na neno langu na aliseme kwa uaminifu. Kwa maana jani kavu lina uhusiano gani na ngano?” asema Bwana.
29 Is not My word like as fire? saith the LORD; and like a hammer that breaketh the rock in pieces?
“Je, neno langu si kama moto,” asema Bwana, “na kama nyundo ivunjayo mwamba vipande vipande?
30 Therefore, behold, I am against the prophets, saith the LORD, that steal My words every one from his neighbour.
“Kwa hiyo, niko kinyume na manabii wanaoibiana maneno kana kwamba ni yangu,” asema Bwana.
31 Behold, I am against the prophets, saith the LORD, that use their tongues and say: 'He saith.'
“Naam, mimi niko kinyume na manabii wanaotikisa ndimi zao wenyewe na kusema, ‘Bwana asema.’
32 Behold, I am against them that prophesy lying dreams, saith the LORD, and do tell them, and cause My people to err by their lies, and by their wantonness; yet I sent them not, nor commanded them; neither can they profit this people at all, saith the LORD.
Kweli, niko kinyume na hao wanaotabiri ndoto za uongo,” asema Bwana. “Wanazisimulia na kuwapotosha watu wangu kwa uongo wao bila kujali, lakini sikuwatuma wala sikuwaamuru. Hawawafaidi watu hawa hata kidogo,” asema Bwana.
33 And when this people, or the prophet, or a priest, shall ask thee, saying: 'What is the burden of the LORD?' then shalt thou say unto them: 'What burden! I will cast you off, saith the LORD.'
“Wakati watu hawa, au nabii, au kuhani watakapokuuliza, ‘Mzigo wa Bwana ni nini?’ wewe utawaambia, ‘Ninyi ndio mzigo. Nami nitawavua kama vazi, asema Bwana.’
34 And as for the prophet, and the priest, and the people, that shall say: 'The burden of the LORD', I will even punish that man and his house.
Nabii, kuhani, au mtu yeyote akisema, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ nitamwadhibu huyo na nyumba yake.
35 Thus shall ye say every one to his neighbour, and every one to his brother: 'What hath the LORD answered?' and: 'What hath the LORD spoken?'
Hivyo mnaambiana kila mmoja na mwenzake, au kwa mtu wa nyumba yao: ‘Bwana amejibu nini?’ au ‘Bwana amesema nini?’
36 And the burden of the LORD shall ye mention no more; for every man's own word shall be his burden; and would ye pervert the words of the living God, of the LORD of hosts our God?
Lakini kamwe msiseme tena, ‘Nina mzigo wa Bwana,’ kwa sababu kila neno la mtu binafsi linakuwa mzigo wake mwenyewe, na hivyo kupotosha maneno ya Mungu aliye hai, Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wetu.
37 Thus shalt thou say to the prophet: 'What hath the LORD answered thee?' and: 'What hath the LORD spoken?'
Hivi ndivyo utakavyoendelea kumuuliza nabii: ‘Bwana amekujibu nini?’ au ‘Je, Bwana amesema nini?’
38 But if ye say: 'The burden of the LORD'; therefore thus saith the LORD: Because ye say this word: 'The burden of the LORD', and I have sent unto you, saying: 'Ye shall not say: The burden of the LORD';
Ingawa unadai, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hili ndilo Bwana asemalo: Ulitumia maneno, ‘Huu ndio mzigo wa Bwana,’ hata ingawa nilikuambia kuwa kamwe usiseme, ‘Huu ni mzigo wa Bwana.’
39 therefore, behold, I will utterly tear you out, and I will cast you off, and the city that I gave unto you and to your fathers, away from My presence;
Kwa hiyo, hakika nitakusahau na kukutupa mbali na uso wangu pamoja na mji niliowapa ninyi na baba zenu.
40 and I will bring an everlasting reproach upon you, and a perpetual shame, which shall not be forgotten.
Nitaleta juu yako fedheha ya kudumu: yaani aibu ya kudumu ambayo haitasahaulika.”

< Jeremiah 23 >