< Isaiah 2 >

1 The word that Isaiah the son of Amoz saw concerning Judah and Jerusalem.
Hili ndilo aliloliona Isaya mwana wa Amozi kuhusu Yuda na Yerusalemu:
2 And it shall come to pass in the end of days, that the mountain of the LORD'S house shall be established as the top of the mountains, and shall be exalted above the hills; and all nations shall flow unto it.
Katika siku za mwisho mlima wa Hekalu la Bwana utaimarishwa kama mlima mkuu miongoni mwa milima yote, utainuliwa juu ya vilima, na mataifa yote yatamiminika huko.
3 And many peoples shall go and say: 'Come ye, and let us go up to the mountain of the LORD, to the house of the God of Jacob; and He will teach us of His ways, and we will walk in His paths.' For out of Zion shall go forth the law, and the word of the LORD from Jerusalem.
Mataifa mengi yatakuja na kusema, “Njooni, twendeni mlimani mwa Bwana, kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo. Atatufundisha njia zake, ili tuweze kuenenda katika mapito yake.” Sheria itatoka Sayuni, neno la Bwana litatoka Yerusalemu.
4 And He shall judge between the nations, and shall decide for many peoples; and they shall beat their swords into plowshares, and their spears into pruninghooks; nation shall not lift up sword against nation, neither shall they learn war any more.
Atahukumu kati ya mataifa na ataamua migogoro ya mataifa mengi. Watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao kuwa miundu ya kukata matawi. Taifa halitainua upanga dhidi ya taifa jingine, wala hawatajifunza vita tena.
5 O house of Jacob, come ye, and let us walk in the light of the LORD.
Njooni, enyi nyumba ya Yakobo, tutembeeni katika nuru ya Bwana.
6 For Thou hast forsaken Thy people the house of Jacob; for they are replenished from the east, and with soothsayers like the Philistines, and they please themselves in the brood of aliens.
Umewatelekeza watu wako, nyumba ya Yakobo. Wamejaa ushirikina utokao Mashariki, wanapiga ramli kama Wafilisti na wanashikana mikono na wapagani.
7 Their land also is full of silver and gold, neither is there any end of their treasures; their land also is full of horses, neither is there any end of their chariots.
Nchi yao imejaa fedha na dhahabu, hakuna mwisho wa hazina zao. Nchi yao imejaa farasi, hakuna mwisho wa magari yao.
8 Their land also is full of idols; every one worshippeth the work of his own hands, that which his own fingers have made.
Nchi yao imejaa sanamu, wanasujudia kazi za mikono yao, vitu vile vidole vyao vimevitengeneza.
9 And man boweth down, and man lowereth himself; and Thou canst not bear with them.
Kwa hiyo mwanadamu atashushwa na binadamu atanyenyekezwa: usiwasamehe.
10 Enter into the rock, and hide thee in the dust, from before the terror of the LORD, and from the glory of His majesty.
Ingieni kwenye miamba, jificheni ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake!
11 The lofty looks of man shall be brought low, and the haughtiness of men shall be bowed down, and the LORD alone shall be exalted in that day.
Macho ya mtu mwenye majivuno yatanyenyekezwa na kiburi cha wanadamu kitashushwa, Bwana peke yake ndiye atakayetukuzwa siku hiyo.
12 For the LORD of hosts hath a day upon all that is proud and lofty, and upon all that is lifted up, and it shall be brought low;
Bwana Mwenye Nguvu Zote anayo siku aliyoiweka akiba kwa wote wenye kujivuna na wenye kiburi, kwa wote wanaojikweza (nao watanyenyekezwa),
13 And upon all the cedars of Lebanon that are high and lifted up, and upon all the oaks of Bashan;
kwa mierezi yote ya Lebanoni iliyo mirefu sana, na mialoni yote ya Bashani,
14 And upon all the high mountains, and upon all the hills that are lifted up;
kwa milima yote mirefu na vilima vyote vilivyoinuka,
15 And upon every lofty tower, and upon every fortified wall;
kwa kila mnara ulio mrefu sana na kila ukuta wenye ngome,
16 And upon all the ships of Tarshish, and upon all delightful imagery.
kwa kila meli ya biashara, na kila chombo cha baharini cha fahari.
17 And the loftiness of man shall be bowed down, and the haughtiness of men shall be brought low; and the LORD alone shall be exalted in that day.
Majivuno ya mwanadamu yatashushwa, na kiburi cha wanadamu kitanyenyekezwa, Bwana peke yake ndiye atatukuzwa siku hiyo,
18 And the idols shall utterly pass away.
nazo sanamu zitatoweka kabisa.
19 And men shall go into the caves of the rocks, and into the holes of the earth, from before the terror of the LORD, and from the glory of His majesty, when He ariseth to shake mightily the earth.
Watu watakimbilia kwenye mapango ndani ya miamba, na kwenye mahandaki ardhini kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
20 In that day a man shall cast away his idols of silver, and his idols of gold, which they made for themselves to worship, to the moles and to the bats;
Siku ile, watu watawatupia panya na popo sanamu zao za fedha na za dhahabu, walizozitengeneza ili waziabudu.
21 To go into the clefts of the rocks, and into the crevices of the crags, from before the terror of the LORD, and from the glory of His majesty, when he ariseth to shake mightily the earth.
Watakimbilia kwenye mapango miambani na kwenye nyufa za miamba kutokana na utisho wa Bwana na utukufu wa enzi yake, ainukapo kuitikisa dunia.
22 Cease ye from man, in whose nostrils is a breath; for how little is he to be accounted!
Acheni kumtumainia mwanadamu, ambaye hana kitu ila pumzi katika pua zake. Yeye ana thamani gani?

< Isaiah 2 >