< Hosea 11 >

1 When Israel was a child, then I loved him, and out of Egypt I called My son.
“Wakati Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda, nilimwita mwanangu kutoka Misri.
2 The more they called them, the more they went from them; they sacrificed unto the Baalim, and offered to graven images.
Lakini kadiri nilivyomwita Israeli, ndivyo walivyokwenda mbali nami. Walitoa dhabihu kwa Mabaali na kufukiza uvumba kwa vinyago.
3 And I, I taught Ephraim to walk, taking them by their arms; but they knew not that I healed them.
Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea, nikiwashika mikono; lakini hawakutambua kuwa ni mimi niliyewaponya.
4 I drew them with cords of a man, with bands of love; and I was to them as they that take off the yoke on their jaws, and I fed them gently.
Niliwaongoza kwa kamba za huruma ya kibinadamu, kwa vifungo vya upendo; niliondoa nira shingoni mwao nami nikainama kuwalisha.
5 He shall not return into the land of Egypt, but the Assyrian shall be his king, because they refused to return.
“Je, hawatarudi Misri, nayo Ashuru haitawatawala kwa sababu wamekataa kutubu?
6 And the sword shall fall upon his cities, and shall consume his bars, and devour them, because of their own counsels.
Panga zitametameta katika miji yao, zitaharibu makomeo ya malango yao na kukomesha mipango yao.
7 And My people are in suspense about returning to Me; and though they call them upwards, none at all will lift himself up.
Watu wangu wamedhamiria kuniacha. Hata kama wakimwita Yeye Aliye Juu Sana, kwa vyovyote hatawainua.
8 How shall I give thee up, Ephraim? How shall I surrender thee, Israel? How shall I make thee as Admah? How shall I set thee as Zeboim? My heart is turned within Me, My compassions are kindled together.
“Efraimu, ninawezaje kukuacha? Ee Israeli, ninawezaje kukutoa? Nitawezaje kukutendea kama Adma? Nitawezaje kukufanya kama Seboimu? Moyo wangu umegeuka ndani yangu, huruma zangu zote zimeamshwa.
9 I will not execute the fierceness of Mine anger, I will not return to destroy Ephraim; for I am God, and not man, the Holy One in the midst of thee; and I will not come in fury.
Sitatimiza hasira yangu kali, wala sitageuka na kumharibu Efraimu. Kwa kuwa mimi ndimi Mungu, wala si mwanadamu, Aliye Mtakatifu miongoni mwenu. Sitakuja kwa ghadhabu.
10 They shall walk after the LORD, who shall roar like a lion; for He shall roar, and the children shall come trembling from the west.
Watamfuata Bwana; atanguruma kama simba. Wakati angurumapo, watoto wake watakuja wakitetemeka kutoka magharibi.
11 They shall come trembling as a bird out of Egypt, and as a dove out of the land of Assyria; and I will make them to dwell in their houses, saith the LORD.
Watakuja wakitetemeka kama ndege wakitoka Misri, kama hua wakitoka Ashuru. Nitawakalisha katika nyumba zao,” asema Bwana.
12 Ephraim compasseth Me about with lies, and the house of Israel with deceit; and Judah is yet wayward towards God, and towards the Holy One who is faithful.
Efraimu amenizunguka kwa uongo, nyumba ya Israeli kwa udanganyifu. Naye Yuda ni mkaidi dhidi ya Mungu, hata kinyume cha yule mwaminifu Aliye Mtakatifu.

< Hosea 11 >