< Genesis 41 >

1 And it came to pass at the end of two full years, that Pharaoh dreamed: and, behold, he stood by the river.
Baada ya miaka miwili kamili kupita, Farao aliota ndoto: Tazama alikuwa amesimama kando ya Mto Naili,
2 And, behold, there came up out of the river seven kine, well-favoured and fat-fleshed; and they fed in the reed-grass.
wakati ngʼombe saba, wazuri na wanono, walitokea mtoni wakajilisha kwenye matete.
3 And, behold, seven other kine came up after them out of the river, ill favoured and lean-fleshed; and stood by the other kine upon the brink of the river.
Baada yao ngʼombe wengine saba, wabaya na waliokonda, wakatokea mtoni Naili wakasimama kando ya wale wanono ukingoni mwa mto.
4 And the ill-favoured and lean-fleshed kine did eat up the seven well-favoured and fat kine. So Pharaoh awoke.
Wale ngʼombe wabaya na waliokonda wakawala wale saba wazuri na wanono. Kisha Farao akaamka.
5 And he slept and dreamed a second time: and, behold, seven ears of corn came up upon one stalk, rank and good.
Farao akaingia usingizini tena akaota ndoto ya pili: Akaona masuke saba ya nafaka, yenye afya na mazuri, yanakua katika bua moja.
6 And, behold, seven ears, thin and blasted with the east wind, sprung up after them.
Baadaye, masuke mengine saba yakachipua, yakiwa membamba yaliyonyaushwa na upepo wa mashariki.
7 And the thin ears swallowed up the seven rank and full ears. And Pharaoh awoke, and, behold, it was a dream.
Masuke yale membamba yakameza yale masuke saba yenye afya na yaliyojaa. Basi Farao akaamka kutoka usingizini, kumbe ilikuwa ndoto.
8 And it came to pass in the morning that his spirit was troubled; and he sent and called for all the magicians of Egypt, and all the wise men thereof; and Pharaoh told them his dream; but there was none that could interpret them unto Pharaoh.
Asubuhi yake, alifadhaika akilini, hivyo akawaita waaguzi wote pamoja na watu wenye busara wa Misri. Walipokuja, Farao akawaeleza ndoto zake, lakini hakuna hata mmoja aliyeweza kumfasiria.
9 Then spoke the chief butler unto Pharaoh, saying: 'I make mention of my faults this day:
Ndipo mnyweshaji mkuu alipomwambia Farao, “Leo nimekumbushwa kuhusu kosa langu.
10 Pharaoh was wroth with his servants, and put me in the ward of the house of the captain of the guard, me and the chief baker.
Wakati fulani Farao aliwakasirikia watumishi wake, akanifunga mimi na mwokaji mkuu katika nyumba ya mkuu wa ulinzi.
11 And we dreamed a dream in one night, I and he; we dreamed each man according to the interpretation of his dream.
Kila mmoja wetu aliota ndoto katika usiku mmoja na kila ndoto ilikuwa na maana yake tofauti.
12 And there was with us there a young man, a Hebrew, servant to the captain of the guard; and we told him, and he interpreted to us our dreams; to each man according to his dream he did interpret.
Basi kijana wa Kiebrania aliyekuwa pamoja nasi huko, alikuwa mtumishi wa mkuu wa kikosi cha ulinzi. Tulimweleza ndoto zetu, naye akatufasiria, akitupa kila mtu tafsiri ya ndoto yake.
13 And it came to pass, as he interpreted to us, so it was: I was restored unto mine office, and he was hanged.'
Nayo mambo yakawa sawa kabisa na jinsi alivyotufasiria ndoto zetu: Mimi nilirudishwa kazini mwangu na huyo mtu mwingine akaangikwa.”
14 Then Pharaoh sent and called Joseph, and they brought him hastily out of the dungeon. And he shaved himself, and changed his raiment, and came in unto Pharaoh.
Basi, Farao akatuma Yosefu aitwe, naye akatolewa kifungoni haraka. Baada ya kunyoa na kubadilisha nguo zake akaenda mbele ya Farao.
15 And Pharaoh said unto Joseph: 'I have dreamed a dream, and there is none that can interpret it; and I have heard say of thee, that when thou hearest a dream thou canst interpret it.'
Farao akamwambia Yosefu, “Nimeota ndoto, wala hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuifasiri. Lakini nimesikia ikisemwa kwa habari yako kwamba unapoelezwa ndoto waweza kuifasiri.”
16 And Joseph answered Pharaoh, saying: 'It is not in me; God will give Pharaoh an answer of peace.'
Yosefu akamjibu Farao, “Siwezi kuifasiri, lakini Mungu atampa Farao jibu analolihitaji.”
17 And Pharaoh spoke unto Joseph: 'In my dream, behold, I stood upon the brink of the river.
Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Katika ndoto yangu nilikuwa nimesimama ukingoni mwa Mto Naili,
18 And, behold, there came up out of the river seven kine, fat-fleshed and well-favoured; and they fed in the reed-grass.
nikawaona ngʼombe saba, wazuri na wanono, wakijitokeza kutoka mtoni wakaja kujilisha kwenye matete.
19 And, behold, seven other kine came up after them, poor and very ill-favoured and lean-fleshed, such as I never saw in all the land of Egypt for badness.
Baada ya hao, ngʼombe wengine saba wadhaifu wakatokea, wabaya sana na waliokonda. Kamwe sikuwahi kuona ngʼombe wabaya jinsi hiyo katika nchi yote ya Misri.
20 And the lean and ill-favoured kine did eat up the first seven fat kine.
Hao ngʼombe waliokonda na wabaya sana wakawala wale ngʼombe saba walionona waliojitokeza kwanza.
21 And when they had eaten them up, it could not be known that they had eaten them; but they were still ill-favoured as at the beginning. So I awoke.
Lakini hata baada ya kuwala, hakuna mtu ambaye angeweza kusema kwamba wamekula, bado walionekana wabaya kama mwanzoni. Kisha nikaamka kutoka usingizini.
22 And I saw in my dream, and, behold, seven ears came up upon one stalk, full and good.
“Pia katika ndoto zangu niliona masuke saba ya nafaka, yamejaa na mazuri, yanakua katika bua moja.
23 And, behold, seven ears, withered, thin, and blasted with the east wind, sprung up after them.
Baada ya hayo masuke mengine saba yakachipua, yaliyonyauka, membamba na yamekaushwa na upepo wa mashariki.
24 And the thin ears swallowed up the seven good ears. And I told it unto the magicians; but there was none that could declare it to me.'
Yale masuke membamba ya nafaka yakayameza yale masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka. Nimewaeleza waaguzi, wala hakuna yeyote aliyeweza kunifasiria.”
25 And Joseph said unto Pharaoh: 'The dream of Pharaoh is one; what God is about to do He hath declared unto Pharaoh.
Ndipo Yosefu akamwambia Farao, “Ndoto za Farao ni ndoto iyo hiyo moja. Mungu amemfunulia Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
26 The seven good kine are seven years; and the seven good ears are seven years: the dream is one.
Ngʼombe saba wazuri ni miaka saba, nayo masuke saba mazuri yaliyojaa nafaka ni miaka saba, ni ndoto iyo hiyo moja.
27 And the seven lean and ill-favoured kine that came up after them are seven years, and also the seven empty ears blasted with the east wind; they shall be seven years of famine.
Ngʼombe saba waliokonda na wabaya wale waliojitokeza baadaye ni miaka saba, vivyo hivyo masuke saba ya ngano yaliyodhoofika na kukaushwa na upepo wa mashariki, ni miaka saba ya njaa.
28 That is the thing which I spoke unto Pharaoh: what God is about to do He hath shown unto Pharaoh.
“Ni kama vile nilivyomwambia Farao: Mungu amemwonyesha Farao jambo analokusudia kufanya karibuni.
29 Behold, there come seven years of great plenty throughout all the land of Egypt.
Miaka saba ya neema inakuja katika nchi yote ya Misri,
30 And there shall arise after them seven years of famine; and all the plenty shall be forgotten in the land of Egypt; and the famine shall consume the land;
lakini itafuata miaka saba ya njaa. Ndipo neema yote ya Misri itasahaulika na njaa itaikumba nchi.
31 and the plenty shall not be known in the land by reason of that famine which followeth; for it shall be very grievous.
“Neema iliyokuwa katika nchi haitakumbukwa, kwa sababu njaa itakayofuata itakuwa kali mno.
32 And for that the dream was doubled unto Pharaoh twice, it is because the thing is established by God, and God will shortly bring it to pass.
Sababu ya ndoto kumjia Farao kwa namna mbili ni kwamba jambo hilo Mungu ameshaamua kwa hakika, naye Mungu atalifanya karibuni.
33 Now therefore let Pharaoh look out a man discreet and wise, and set him over the land of Egypt.
“Basi sasa Farao na atafute mtu mwenye akili na hekima ili amweke kuwa msimamizi wa nchi ya Misri.
34 Let Pharaoh do this, and let him appoint overseers over the land, and take up the fifth part of the land of Egypt in the seven years of plenty.
Farao na aweke wenye amri nchini kote wakusanye sehemu ya tano ya mavuno ya Misri katika miaka hii saba ya neema.
35 And let them gather all the food of these good years that come, and lay up corn under the hand of Pharaoh for food in the cities, and let them keep it.
Wakusanye chakula chote katika miaka hii saba ya neema inayokuja na kuhifadhi nafaka chini ya mamlaka ya Farao, iwe akiba ya chakula katika miji.
36 And the food shall be for a store to the land against the seven years of famine, which shall be in the land of Egypt; that the land perish not through the famine.'
Chakula hiki kitakuwa akiba ya tahadhari kwa ajili ya nchi, ili kitumike katika ile miaka saba ya njaa itakayokuja Misri, ili nchi isiharibiwe na njaa.”
37 And the thing was good in the eyes of Pharaoh, and in the eyes of all his servants.
Mpango huu ulionekana mzuri kwa Farao na kwa maafisa wake wote.
38 And Pharaoh said unto his servants: 'Can we find such a one as this, a man in whom the spirit of God is?'
Hivyo Farao akawauliza, “Je tunaweza kumpata yeyote kama mtu huyu, ambaye Roho wa Mungu yumo ndani yake?”
39 And Pharaoh said unto Joseph: 'Forasmuch as God hath shown thee all this, there is none so discreet and wise as thou.
Ndipo Farao akamwambia Yosefu, “Maadamu Mungu amekufunulia yote haya, hakuna mwingine yeyote mwenye akili na hekima kama wewe.
40 Thou shalt be over my house, and according unto thy word shall all my people be ruled; only in the throne will I be greater than thou.'
Wewe utakuwa msimamizi wa jumba langu la kifalme, na watu wangu wote watatii amri zako. Ni kuhusu kiti cha ufalme tu nitakuwa mkuu kuliko wewe.”
41 And Pharaoh said unto Joseph: 'See, I have set thee over all the land of Egypt.'
Kwa hiyo Farao akamwambia Yosefu, “Sasa nakuweka uwe msimamizi wa nchi yote ya Misri.”
42 And Pharaoh took off his signet ring from his hand, and put it upon Joseph's hand, and arrayed him in vestures of fine linen, and put a gold chain about his neck.
Ndipo Farao akaivua pete yake ya muhuri kutoka kidoleni mwake na kuivalisha katika kidole cha Yosefu. Akamvika majoho mazuri ya kitani safi na mkufu wa dhahabu shingoni mwake.
43 And he made him to ride in the second chariot which he had; and they cried before him: 'Abrech'; and he set him over all the land of Egypt.
Akampandisha katika gari lake la farasi kama msaidizi wake, watu wakatangulia wakishangilia, wakisema, “Fungueni njia!” Ndivyo Farao alivyomweka Yosefu kuwa msimamizi wa nchi yote ya Misri.
44 And Pharaoh said unto Joseph: 'I am Pharaoh, and without thee shall no man lift up his hand or his foot in all the land of Egypt.'
Kisha Farao akamwambia Yosefu, “Mimi ni Farao, lakini pasipo neno lako, hakuna mtu mwenye ruhusa kuinua mkono au mguu katika nchi yote ya Misri.”
45 And Pharaoh called Joseph's name Zaphenath-paneah; and he gave him to wife Asenath the daughter of Poti-phera priest of On. And Joseph went out over the land of Egypt. —
Farao akamwita Yosefu Safenath-Panea, pia akampa Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, kuwa mke wake. Ndipo Yosefu akaitembelea nchi yote ya Misri.
46 And Joseph was thirty years old when he stood before Pharaoh king of Egypt. — And Joseph went out from the presence of Pharaoh, and went throughout all the land of Egypt.
Yosefu alikuwa na miaka thelathini alipoingia katika utumishi wa Farao mfalme wa Misri. Naye Yosefu akatoka mbele ya Farao akasafiri katika nchi yote ya Misri.
47 And in the seven years of plenty the earth brought forth in heaps.
Katika ile miaka saba ya neema nchi ilizaa mazao kwa wingi sana.
48 And he gathered up all the food of the seven years which were in the land of Egypt, and laid up the food in the cities; the food of the field, which was round about every city, laid he up in the same.
Yosefu akakusanya chakula chote kilichozalishwa katika ile miaka saba ya neema nchini Misri, akakihifadhi katika ghala za miji. Katika kila mji kulihifadhiwa chakula kilichozalishwa katika mashamba yaliyouzunguka mji huo.
49 And Joseph laid up corn as the sand of the sea, very much, until they left off numbering; for it was without number.
Yosefu alihifadhi nafaka nyingi, mfano wa mchanga wa bahari, ilikuwa nyingi mno kiasi kwamba walishindwa kuweka kumbukumbu kwa sababu akiba ilizidi sana kupita kipimo.
50 And unto Joseph were born two sons before the year of famine came, whom Asenath the daughter of Poti-phera priest of On bore unto him.
Kabla ya miaka ya njaa kuanza, Asenathi binti Potifera, kuhani wa mji wa Oni, alikuwa amemzalia Yosefu wana wawili wa kiume.
51 And Joseph called the name of the first-born Manasseh: 'for God hath made me forget all my toil, and all my father's house.'
Yosefu akamwita mzaliwa wake wa kwanza Manase, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenifanya nisahau taabu zangu zote pamoja na jamaa yote ya nyumba ya baba yangu.”
52 And the name of the second called he Ephraim: 'for God hath made me fruitful in the land of my affliction.'
Mwana wa pili akamwita Efraimu, akisema, “Ni kwa sababu Mungu amenistawisha katika nchi ya mateso yangu.”
53 And the seven years of plenty, that was in the land of Egypt, came to an end.
Ile miaka saba ya neema huko Misri ikaisha,
54 And the seven years of famine began to come, according as Joseph had said; and there was famine in all lands; but in all the land of Egypt there was bread.
nayo miaka ile saba ya njaa ikaanza, sawasawa na alivyosema Yosefu. Kulikuwa na njaa katika nchi nyingine zote, bali katika nchi yote ya Misri kulikuwa na chakula.
55 And when all the land of Egypt was famished, the people cried to Pharaoh for bread; and Pharaoh said unto all the Egyptians: 'Go unto Joseph; what he saith to you, do.'
Wakati nchi yote ya Misri ilipopatwa na njaa, watu wakamlilia Farao ili awape chakula. Ndipo Farao alipowaagiza Wamisri wote, akisema, “Nendeni kwa Yosefu, nanyi mfanye anachowaambia.”
56 And the famine was over all the face of the earth; and Joseph opened all the storehouses, and sold unto the Egyptians; and the famine was sore in the land of Egypt.
Wakati njaa ilipokuwa imeenea katika nchi yote, Yosefu akafungua ghala za vyakula na kuwauzia Wamisri nafaka, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno katika nchi yote ya Misri.
57 And all countries came into Egypt to Joseph to buy corn; because the famine was sore in all the earth.
Pia nchi nyingine zote zilikuja Misri kununua nafaka kutoka kwa Yosefu, kwa sababu njaa ilikuwa kali mno duniani kote.

< Genesis 41 >