< Ezra 8 >

1 Now these are the heads of their fathers' houses, and this is the genealogy of them that went up with me from Babylon, in the reign of Artaxerxes the king.
Hawa ndio viongozi wa jamaa pamoja na wale walioandikwa ambao walikuja pamoja nami kutoka Babeli wakati wa utawala wa Mfalme Artashasta:
2 Of the sons of Phinehas, Gershom; of the sons of Ithamar, Daniel; of the sons of David, Hattush.
wa wazao wa Finehasi, alikuwa Gershoni; wa wazao wa Ithamari, alikuwa Danieli; wa wazao wa Daudi, alikuwa Hatushi
3 Of the sons of Shecaniah: of the sons of Parosh, Zechariah; and with him were reckoned by genealogy of the males a hundred and fifty.
wa wazao wa Shekania; wa wazao wa Paroshi, alikuwa Zekaria, na watu 150 walioandikishwa pamoja naye;
4 Of the sons of Pahath-moab, Eliehoenai the son of Zerahiah; and with him two hundred males.
wa wazao wa Pahath-Moabu, alikuwa Eliehoenai mwana wa Zerahia na wanaume 200 pamoja naye;
5 Of the sons of Shechaniah, the son of Jahaziel; and with him three hundred males.
wa wazao wa Zatu, alikuwa Shekania mwana wa Yahazieli na wanaume 300 pamoja naye;
6 And of the sons of Adin, Ebed the son of Jonathan; and with him fifty males.
wa wazao wa Adini, alikuwa Ebedi mwana wa Yonathani na wanaume 50 pamoja naye;
7 And of the sons of Elam, Jeshaiah the son of Athaliah; and with him seventy males.
wa wazao wa Elamu, alikuwa Yeshaya mwana wa Athalia, na wanaume 70 pamoja naye;
8 And of the sons of Shephatiah, Zebadiah the son of Michael; and with him fourscore males.
wa wazao wa Shefatia, alikuwa Zebadia mwana wa Mikaeli na wanaume 80 pamoja naye;
9 Of the sons of Joab, Obadiah the son of Jehiel; and with him two hundred and eighteen males.
wa wazao wa Yoabu, alikuwa Obadia mwana wa Yehieli na wanaume 218 pamoja naye;
10 And of the sons of Shelomith, the son of Josiphiah; and with him a hundred and threescore males.
wa wazao wa Bani, alikuwa Shelomithi mwana wa Yosifia na wanaume 160 pamoja naye;
11 And of the sons of Bebai, Zechariah the son of Bebai; and with him twenty and eight males.
wa wazao wa Bebai, alikuwa Zekaria mwana wa Bebai na wanaume 28 pamoja naye;
12 And of the sons of Azgad, Johanan the son of Hakkatan; and with him a hundred and ten males.
wa wazao wa Azgadi, alikuwa Yohanani mwana wa Hakatani na wanaume 110 pamoja naye;
13 And of the sons of Adonikam, that were the last; and these are their names, Eliphelet, Jeiel, and Shemaiah; and with them threescore males.
wa wazao wa Adonikamu, hawa walikuwa wa mwisho ambao majina yao ni Elifeleti, Yeueli, Shemaya na wanaume 60 pamoja nao;
14 And of the sons of Bigvai, Uthai and Zaccur; and with him seventy males.
wa wazao wa Bigwai, walikuwa Uthai na Zakuri na wanaume 70 pamoja nao.
15 And I gathered them together to the river that runneth to Ahava; and there we encamped three days; and I viewed the people, and the priests, and found there none of the sons of Levi.
Niliwakusanya kwenye mto utiririkao kuelekea Ahava, nasi tukapiga kambi pale siku tatu. Wakati nilipokagua kati ya watu na makuhani, sikuwapata Walawi.
16 Then sent I for Eliezer, for Ariel, for Shemaiah, and for Elnathan, and for Jarib, and for Elnathan, and for Nathan, and for Zechariah, and for Meshullam, chief men; also for Joiarib, and for Elnathan, teachers.
Basi niliwaita Eliezeri, Arieli, Shemaya, Elnathani, Yaribu, Elnathani, Nathani, Zekaria na Meshulamu waliokuwa viongozi na Yoyaribu na Elnathani waliokuwa wasomi,
17 And I gave them commandment unto Iddo the chief at the place Casiphia; and I told them what they should say unto Iddo and his brother, who were set over the place Casiphia, that they should bring unto us ministers for the house of our God.
nikawatuma kwa Ido kiongozi huko Kasifia. Niliwaambia watakayomwambia Ido na ndugu zake, watumishi wa Hekalu huko Kasifia, ili waweze kutuletea wahudumu kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
18 And according to the good hand of our God upon us they brought us a man of discretion, of the sons of Mahli, the son of Levi, the son of Israel; and Sherebiah, with his sons and his brethren, eighteen;
Kwa sababu mkono wa neema wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, walituletea Sherebia, mtu mwenye uwezo kutoka wazao wa Mahli mwana wa Lawi, mwana wa Israeli, na wana wa Sherebia pamoja na ndugu zao wanaume kumi na wanane.
19 and Hashabiah, and with him Jeshaiah of the sons of Merari, his brethren and their sons, twenty;
Naye Hashabia, pamoja na Yeshaya kutoka wazao wa Merari na ndugu zake na wapwa wake wanaume ishirini.
20 and of the Nethinim, whom David and the princes had given for the service of the Levites, two hundred and twenty Nethinim; all of them were mentioned by name.
Vilevile walileta watumishi wa Hekalu 220, kikundi ambacho Daudi na maafisa walikuwa wamekiweka kusaidia Walawi. Wote walikuwa wameorodheshwa kwa majina.
21 Then I proclaimed a fast there, at the river Ahava, that we might humble ourselves before our God, to seek of Him a straight way, for us, and for our little ones, and for all our substance.
Kando ya Mto Ahava, hapo nilitangaza kufunga, ili tujinyenyekeshe mbele za Mungu wetu na kumwomba kwa ajili ya kutujalia safari ya amani sisi na watoto wetu, pamoja na mali zetu zote.
22 For I was ashamed to ask of the king a band of soldiers and horsemen to help us against the enemy in the way; because we had spoken unto the king, saying: 'The hand of our God is upon all them that seek Him, for good; but His power and His wrath is against all them that forsake Him.'
Niliona aibu kumwomba mfalme askari na wapanda farasi wa kutulinda njiani kutokana na adui zetu, kwa sababu tulikwisha kumwambia mfalme, “Mkono wa neema wa Mungu wetu uko juu ya kila mmoja anayemtafuta, lakini hasira yake kubwa ni dhidi ya wote wamwachao.”
23 So we fasted and besought our God for this; and He was entreated of us.
Kwa hiyo tulifunga na kumwomba Mungu wetu kuhusu jambo hili, naye akajibu maombi yetu.
24 Then I separated twelve of the chiefs of the priests, besides Sherebiah, Hashabiah, and ten of their brethren with them,
Kisha niliwatenga viongozi wa makuhani kumi na wawili, pamoja na Sherebia, Hashabia na ndugu zao kumi,
25 and weighed unto them the silver, and the gold, and the vessels, even the offering for the house of our God, which the king, and his counsellors, and his princes, and all Israel there present, had offered;
nami nikawapimia fedha, dhahabu na vifaa ambavyo mfalme, washauri wake, maafisa wake na Israeli wote waliokuwepo walikuwa wamevitoa sadaka kwa ajili ya nyumba ya Mungu wetu.
26 I even weighed into their hand six hundred and fifty talents of silver, and silver vessels a hundred talents; of gold a hundred talents;
Niliwapimia talanta 650 za fedha, vifaa vingine vya fedha vya uzito wa talanta mia moja, talanta mia moja za dhahabu,
27 and twenty bowels of gold, of a thousand darics; and two vessels of fine bright brass, precious as gold.
mabakuli ishirini ya dhahabu ya thamani ya darkoni elfu moja, na vyombo viwili vya shaba iliyosuguliwa, ya thamani kama dhahabu.
28 And I said unto them: 'Ye are holy unto the LORD, and the vessels are holy; and the silver and the gold are a freewill-offering unto the LORD, the God of your fathers.
Niliwaambia, “Ninyi pamoja na vyombo hivi ni wakfu kwa Bwana. Fedha na dhahabu ni sadaka ya hiari kwa Bwana, Mungu wa baba zenu.
29 Watch ye, and keep them, until ye weigh them before the chiefs of the priests and the Levites, and the princes of the fathers' houses of Israel, at Jerusalem, in the chambers of the house of the LORD.'
Vilindeni kwa uangalifu mpaka mtakapovipima ndani ya vyumba vya nyumba ya Bwana katika Yerusalemu mbele ya makuhani, viongozi na Walawi pamoja na wakuu wa jamaa za Israeli.”
30 So the priests and the Levites received the weight of the silver and the gold, and the vessels, to bring them to Jerusalem unto the house of our God.
Ndipo makuhani na Walawi wakapokea fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu ambavyo vilipimwa na kupelekwa katika nyumba ya Mungu wetu mjini Yerusalemu.
31 Then we departed from the river of Ahava on the twelfth day of the first month, to go unto Jerusalem; and the hand of our God was upon us, and He delivered us from the hand of the enemy and lier-in-wait by the way.
Tulianza safari kutoka Mto Ahava kwenda Yerusalemu kwenye siku ya kumi na mbili ya mwezi wa kwanza. Mkono wa Mungu wetu ulikuwa juu yetu, naye njiani alitulinda dhidi ya adui na wanyangʼanyi.
32 And we came to Jerusalem, and abode there three days.
Kwa hiyo tuliwasili Yerusalemu ambapo tulipumzika kwa siku tatu.
33 And on the fourth day was the silver and the gold and the vessels weighed in the house of our God into the hand of Meremoth the son of Uriah the priest; and with him was Eleazar the son of Phinehas; and with them was Jozabad the son of Jeshua, and Noadiah the son of Binnui, the Levites;
Katika siku ya nne, ndani ya nyumba ya Mungu wetu, tulipima fedha, dhahabu na vyombo vilivyowekwa wakfu, tukakabidhi mikononi mwa kuhani Meremothi mwana wa Uria. Eleazari mwana wa Finehasi alikuwa pamoja naye, pia walikuwako Walawi wawili, Yozabadi mwana wa Yeshua na Noadia mwana wa Binui.
34 the whole by number and by weight; and all the weight was written at that time.
Kila kitu kilihesabiwa kwa idadi na kupimwa kwa uzito, nao uzito wote uliandikwa wakati ule.
35 The children of the captivity, that were come out of exile, offered burnt-offerings unto the God of Israel, twelve bullocks for all Israel, ninety and six rams, seventy and seven lambs, twelve he-goats for a sin-offering; all this was a burnt-offering unto the LORD.
Kisha mateka waliokuwa wamerudi kutoka utumwani wakatoa sadaka za kuteketezwa kwa moto kwa Mungu wa Israeli: mafahali kumi na wawili kwa ajili ya Israeli wote, kondoo dume tisini na sita, wana-kondoo sabini na saba na mbuzi dume kumi na wawili kuwa sadaka ya dhambi. Hii yote ilikuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto kwa Bwana.
36 And they delivered the king's commissions unto the king's satraps, and to the governors beyond the River; and they furthered the people and the house of God.
Pia walikabidhi manaibu wa mfalme na watawala wa Ngʼambo ya Mto Frati maagizo ya mfalme, ambao baadaye walitoa msaada kwa watu na kwa nyumba ya Mungu.

< Ezra 8 >