< Ezekiel 39 >

1 And thou, son of man, prophesy against Gog, and say: Thus saith the Lord GOD: Behold, I am against thee, O Gog, chief prince of Meshech and Tubal;
“Mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali.
2 and I will turn thee about and lead thee on, and will cause thee to come up from the uttermost parts of the north; and I will bring thee upon the mountains of Israel;
Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukuburuta. Nitakuleta kutoka kaskazini ya mbali na kukupeleka wewe dhidi ya milima ya Israeli.
3 and I will smite thy bow out of thy left hand, and will cause thine arrows to fall out of thy right hand.
Kisha nitaupiga upinde wako kutoka mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale ianguke kutoka mkono wako wa kuume.
4 Thou shalt fall upon the mountains of Israel, thou, and all thy bands, and the peoples that are with thee; I will give thee unto the ravenous birds of every sort and to the beasts of the field, to be devoured.
Utaanguka kwenye milima ya Israeli, wewe pamoja na vikosi vyako vyote na yale mataifa yaliyo pamoja nawe. Nitakutoa uwe chakula cha ndege wa aina zote walao nyama na cha wanyama wa mwituni.
5 Thou shalt fall upon the open field; for I have spoken it, saith the Lord GOD.
Utaanguka katika uwanja, kwa kuwa nimenena, asema Bwana Mwenyezi.
6 And I will send a fire on Magog, and on them that dwell safely in the isles; and they shall know that I am the LORD.
Nitatuma moto juu ya Magogu na kwa wale wanaoishi kwa salama huko pwani, nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
7 And My holy name will I make known in the midst of My people Israel; neither will I suffer My holy name to be profaned any more; and the nations shall know that I am the LORD, the Holy One in Israel.
“‘Nitalifanya Jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Israeli. Sitaliacha tena Jina langu takatifu litiwe unajisi, nayo mataifa watajua kuwa Mimi Bwana ndimi Aliye Mtakatifu wa Israeli.
8 Behold, it cometh, and it shall be done, saith the Lord GOD; This is the day whereof I have spoken.
Hili jambo linakuja! Hakika litatokea, asema Bwana Mwenyezi. Hii ndiyo siku ile niliyosema habari zake.
9 And they that dwell in the cities of Israel shall go forth, and shall make fires of the weapons and use them as fuel, both the shields and the bucklers, the bows and the arrows, and the hand-staves, and the spears, and they shall make fires of them seven years;
“‘Ndipo wale wanaoishi katika miji ya Israeli watakapotoka na kutumia hizo silaha kuwashia moto na kuziteketeza, yaani, kigao na ngao, pinde na mishale, rungu za vita na mikuki. Kwa miaka saba watavitumia kama kuni.
10 so that they shall take no wood out of the field, neither cut down any out of the forests, for they shall make fires of the weapons; and they shall spoil those that spoiled them, and rob those that robbed them, saith the Lord GOD.
Hawatahitaji kukusanya kuni kutoka mashambani wala kukata kuni kutoka kwenye misitu, kwa sababu watatumia silaha kuwa kuni. Nao watawateka mateka wale waliowateka na kuchukua nyara mali za wale waliochukua mali zao nyara, asema Bwana Mwenyezi.
11 And it shall come to pass in that day, that I will give unto Gog a place fit for burial in Israel, the valley of them that pass through on the east of the sea; and it shall stop them that pass through; and there shall they bury Gog and all his multitude; and they shall call it the valley of Hamon-gog.
“‘Siku ile nitampa Gogu mahali pa kuzikia katika Israeli, katika bonde la wale wasafirio upande wa mashariki kuelekea baharini. Jambo hili litazuia njia ya wasafiri kwa sababu Gogu na makundi yake yote ya wajeuri watazikwa huko. Kwa hiyo litaitwa Bonde la Hamon-Gogu.
12 And seven months shall the house of Israel be burying them, that they may cleanse the land.
“‘Kwa miezi saba nyumba ya Israeli itakuwa ikiwazika ili kuisafisha nchi.
13 Yea, all the people of the land shall bury them, and it shall be to them a renown; in the day that I shall be glorified, saith the Lord GOD.
Watu wote wa nchi watawazika, nayo siku nitakayotukuzwa itakuwa siku ya kumbukumbu kwa ajili yao, asema Bwana Mwenyezi.
14 And they shall set apart men of continual employment, that shall pass through the land to bury with them that pass through those that remain upon the face of the land, to cleanse it; after the end of seven months shall they search.
“‘Watu wataajiriwa mara kwa mara kuisafisha nchi. Baadhi yao watapita nchini kote na zaidi yao hao wengine, watawazika wale waliosalia juu ya uso wa nchi. Mwisho wa hiyo miezi saba wataanza upekuzi wao.
15 And when they that pass through shall pass through the land, and any seeth a man's bone, then shall he set up a sign by it, till the buriers have buried it in the valley of Hamon-gog.
Wakati wanapopita nchini kote na mmoja wao akaona mfupa wa mwanadamu, ataweka alama kando yake mpaka wachimba kaburi wawe wameuzika katika Bonde la Hamon-Gogu.
16 And Hamonah shall also be the name of a city. Thus shall they cleanse the land.
(Pia mji uitwao Hamona utakuwa humo.) Hivyo ndivyo watakavyoisafisha nchi.’
17 And thou, son of man, thus saith the Lord GOD: Speak unto the birds of every sort, and to every beast of the field: Assemble yourselves, and come; gather yourselves on every side to My feast that I do prepare for you, even a great feast, upon the mountains of Israel, that ye may eat flesh and drink blood.
“Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ita kila aina ya ndege na wanyama wote wa mwituni, waambie: ‘Kusanyikeni mje pamoja kutoka pande zote kwa ajili ya dhabihu ninayowaandalia, dhabihu kuu katika milima ya Israeli. Huko mtakula nyama na kunywa damu.
18 The flesh of the mighty shall ye eat, and the blood of the princes of the earth shall ye drink; rams, lambs, and goats, bullocks, fatlings of Bashan are they all of them.
Mtakula nyama za watu mashujaa na kunywa damu za wakuu wa dunia kana kwamba ni za kondoo dume na kondoo wake, mbuzi na mafahali, wote walionona kutoka Bashani.
19 And ye shall eat fat till ye be full, and drink blood till ye be drunken, of My feast which I have prepared for you.
Katika dhabihu ninayoandaa kwa ajili yenu, mtakula mafuta mpaka mkinai na kunywa damu mpaka mlewe.
20 And ye shall be filled at My table with horses and horsemen, with mighty men, and with all men of war, saith the Lord GOD.
Kwenye meza yangu watajishibisha kwa farasi na wapanda farasi, watu mashujaa na askari wa kila aina,’ asema Bwana Mwenyezi.
21 And I will set My glory among the nations, and all the nations shall see My judgment that I have executed, and My hand that I have laid upon them.
“Nitauonyesha utukufu wangu miongoni mwa mataifa, nayo mataifa yote wataiona adhabu nitakayotoa na mkono wangu nitakaouweka juu yao.
22 So the house of Israel shall know that I am the LORD their God, from that day and forward.
Kuanzia siku ile na kuendelea nyumba ya Israeli itajua kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wao.
23 And the nations shall know that the house of Israel went into captivity for their iniquity, because they broke faith with Me, and I hid My face from them; so I gave them into the hand of their adversaries, and they fell all of them by the sword.
Na mataifa watajua kuwa nyumba ya Israeli walikwenda utumwani kwa ajili ya dhambi yao, kwa sababu hawakuwa waaminifu kwangu. Hivyo niliwaficha uso wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao, nao wote wakaanguka kwa upanga.
24 According to their uncleanness and according to their transgressions did I unto them; and I hid My face from them.
Niliwatendea sawasawa na uchafu wao na makosa yao, nami nikawaficha uso wangu.
25 Therefore thus saith the Lord GOD: Now will I bring back the captivity of Jacob, and have compassion upon the whole house of Israel; and I will be jealous for My holy name.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Sasa nitamrudisha Yakobo kutoka utumwani, nami nitawahurumia watu wote wa Israeli, nami nitakuwa na wivu kwa ajili ya Jina langu takatifu.
26 And they shall bear their shame, and all their breach of faith which they have committed against Me, when they shall dwell safely in their land, and none shall make them afraid;
Wataisahau aibu yao na jinsi walivyoonyesha kutokuwa waaminifu kwangu mimi wakati waliishi salama katika nchi yao, bila kuwa na mtu yeyote wa kuwatia hofu.
27 when I have brought them back from the peoples, and gathered them out of their enemies' lands, and am sanctified in them in the sight of many nations.
Nitakapokuwa nimewarudisha kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka nchi za adui zao, mimi nitajionyesha kuwa mtakatifu kwa kupitia kwao machoni mwa mataifa mengi.
28 And they shall know that I am the LORD their God, in that I caused them to go into captivity among the nations, and have gathered them unto their own land; and I will leave none of them any more there;
Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao, ingawa niliwapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa, nitawakusanya tena katika nchi yao wenyewe, bila kumwacha yeyote nyuma.
29 neither will I hide My face any more from them; for I have poured out My spirit upon the house of Israel, saith the Lord GOD.'
Sitawaficha tena uso wangu, kwa maana nitamimina Roho wangu juu ya nyumba ya Israeli, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ezekiel 39 >