< Ezekiel 15 >

1 And the word of the LORD came unto me, saying:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 'Son of man, what is the vine-tree more than any tree, the vine branch which grew up among the trees of the forest?
“Mwanadamu, je, ni vipi mti wa mzabibu unaweza kuwa bora zaidi kuliko tawi la mti mwingine wowote ndani ya msitu?
3 Shall wood be taken thereof to make any work? or will men take a pin of it to hang any vessel thereon?
Je, mti wake kamwe huchukuliwa na kutengeneza chochote cha manufaa? Je, watu hutengeneza vigingi vya kuningʼinizia vitu kutokana na huo mti wake?
4 Behold, it is cast into the fire for fuel; the fire hath devoured both the ends of it, and the midst of it is singed; is it profitable for any work?
Nao baada ya kutiwa motoni kama nishati na moto ukateketeza ncha zote mbili na kuunguza sehemu ya kati, je, unafaa kwa lolote?
5 Behold, when it was whole, it was meet for no work; how much less, when the fire hath devoured it, and it is singed, shall it yet be meet for any work?
Kama haukufaa kitu chochote ulipokuwa mzima, je, si zaidi sana sasa ambapo hauwezekani kufanyishwa chochote cha kufaa baada ya moto kuuchoma na kuuunguza?
6 Therefore thus saith the Lord GOD: As the vine-tree among the trees of the forest, which I have given to the fire for fuel, so do I give the inhabitants of Jerusalem.
“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Kama nilivyoutoa mti wa mzabibu miongoni mwa miti ya msituni kuwa nishati kwa ajili ya moto, hivyo ndivyo nitakavyowatendea watu waishio Yerusalemu.
7 And I will set My face against them; out of the fire are they come forth, and the fire shall devour them; and ye shall know that I am the LORD, when I set My face against them.
Nitaukaza uso wangu dhidi yao. Ingawa watakuwa wameokoka kwenye moto, bado moto utawateketeza. Nami nitakapoukaza uso wangu dhidi yao, ninyi mtajua kwamba Mimi ndimi Bwana.
8 And I will make the land desolate, because they have acted treacherously, saith the Lord GOD.'
Nitaifanya nchi kuwa ukiwa kwa sababu wamekuwa si waaminifu, asema Bwana Mwenyezi.”

< Ezekiel 15 >