< Exodus 37 >

1 And Bezalel made the ark of acacia-wood: two cubits and a half was the length of it, and a cubit and a half the breadth of it, and a cubit and a half the height of it.
Bezaleli akatengeneza Sanduku la mbao za mshita: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, upana wake dhiraa moja na nusu, na kimo chake dhiraa moja na nusu.
2 And he overlaid it with pure gold within and without, and made a crown of gold to it round about.
Akalifunika kwa dhahabu safi ndani na nje, na kulizungushia ukingo wa dhahabu.
3 And he cast for it four rings of gold, in the four feet thereof: even two rings on the one side of it, and two rings on the other side of it.
Akasubu pete nne za dhahabu na kuzifungia kwenye miguu yake minne, pete mbili kwa upande mmoja na pete mbili kwa upande mwingine.
4 And he made staves of acacia-wood, and overlaid them with gold.
Kisha akatengeneza mipiko ya mti wa mshita na kuzifunika kwa dhahabu.
5 And he put the staves into the rings on the sides of the ark, to bear the ark.
Akaiingiza hiyo mipiko kwenye zile pete katika pande mbili za Sanduku ili kulibeba.
6 And he made an ark-cover of pure gold: two cubits and a half was the length thereof, and a cubit and a half the breadth thereof.
Akatengeneza kifuniko cha upatanisho kwa dhahabu safi: urefu wake ulikuwa dhiraa mbili na nusu, na upana wake dhiraa moja na nusu.
7 And he made two cherubim of gold: of beaten work made he them, at the two ends of the ark-cover:
Kisha akatengeneza makerubi wawili wa dhahabu iliyofuliwa katika miisho ya hicho kifuniko.
8 one cherub at the one end, and one cherub at the other end; of one piece with the ark-cover made he the cherubim at the two ends thereof.
Akatengeneza kerubi mmoja kwenye mwisho mmoja, na kerubi mwingine kwenye mwisho mwingine; akawatengeneza kuwa kitu kimoja na hicho kifuniko katika miisho hiyo miwili.
9 And the cherubim spread out their wings on high, screening the ark-cover with their wings, with their faces one to another; toward the ark-cover were the faces of the cherubim.
Makerubi hao walikuwa wametandaza mabawa kuelekea juu, wakitia kivuli hicho kifuniko. Makerubi hao walielekeana, wakitazama hicho kifuniko.
10 And he made the table of acacia-wood: two cubits was the length thereof, and a cubit the breadth thereof, and a cubit and a half the height thereof.
Akatengeneza meza ya mbao za mshita yenye urefu wa dhiraa mbili, upana wa dhiraa moja, na kimo cha dhiraa moja na nusu.
11 And he overlaid it with pure gold, and made thereto a crown of gold round about.
Kisha akaifunika kwa dhahabu safi, na kuitengenezea ukingo wa dhahabu kuizunguka pande zote.
12 And he made unto it a border of a hand-breadth round about, and made a golden crown to the border thereof round about.
Pia akatengeneza upapi wenye upana wa nyanda nne, na kuufanyia ule upapi ukingo wa dhahabu kuuzunguka pande zote.
13 And he cast for it four rings of gold, and put the rings in the four corners that were on the four feet thereof.
Akasubu pete nne za dhahabu kwa ajili ya meza hiyo, na kuzifungia kwenye pembe nne, pale penye miguu yake minne.
14 Close by the border were the rings, the holders for the staves to bear the table.
Pete hizo ziliwekwa karibu na ukingo ule ili kuishikilia ile mipiko iliyotumika kuibebea hiyo meza.
15 And he made the staves of acacia-wood, and overlaid them with gold, to bear the table.
Mipiko hiyo ya kubebea meza ilitengenezwa kwa mti wa mshita, na ilikuwa imefunikwa kwa dhahabu.
16 And he made the vessels which were upon the table, the dishes thereof, and the pans thereof, and the bowls thereof, and the jars thereof, wherewith to pour out, of pure gold.
Vyombo vyote vya mezani vilitengenezwa kwa dhahabu safi: yaani sahani zake, masinia, na bakuli na bilauri zake kwa ajili ya kumiminia sadaka za vinywaji.
17 And he made the candlestick of pure gold: of beaten work made he the candlestick, even its base, and its shaft; its cups, its knops, and its flowers, were of one piece with it.
Akatengeneza kinara cha taa cha dhahabu safi iliyofuliwa vizuri katika kitako chake na ufito wake; vikombe vyake vilivyofanana na ua, matovu na maua vilikuwa kitu kimoja.
18 And there were six branches going out of the sides thereof: three branches of the candlestick out of the one side thereof, and three branches of the candlestick out of the other side thereof;
Matawi sita yalitokeza kuanzia ule ufito wa katikati wa kinara cha taa: matawi matatu upande mmoja na matatu upande mwingine.
19 three cups made like almond-blossoms in one branch, a knop and a flower; and three cups made like almond-blossoms in the other branch, a knop and a flower. So for the six branches going out of the candlestick.
Vikombe vitatu vya mfano wa maua ya mlozi yenye matovu na maua vilikuwa katika tawi moja, vikombe vitatu katika tawi jingine, na vivyo hivyo kwa matawi yote sita yaliyotokeza kwenye kile kinara cha taa.
20 And in the candlestick were four cups made like almond-blossoms, the knops thereof, and the flowers thereof;
Juu ya kinara chenyewe kulikuwepo na vikombe vinne vya mfano wa maua ya mlozi yakiwa na matovu yake na maua yake.
21 and a knop under two branches of one piece with it, and a knop under two branches of one piece with it, and a knop under two branches of one piece with it, for the six branches going out of it.
Tovu moja lilikuwa chini ya jozi ya kwanza ya matawi yaliyotokeza kwenye kinara cha taa, tovu la pili chini ya jozi ya pili, nalo tovu la tatu chini ya jozi ya tatu, yaani, matawi sita kwa jumla.
22 Their knops and their branches were of one piece with it; the whole of it was one beaten work of pure gold.
Matovu na matawi yote yalikuwa kitu kimoja na kile kinara cha taa, yakiwa yamefuliwa kwa dhahabu safi.
23 And he made the lamps thereof, seven, and the tongs thereof, and the snuffdishes thereof, of pure gold.
Akatengeneza taa zake saba, na pia mikasi ya kusawazishia tambi, pamoja na masinia, zote kwa dhahabu safi.
24 Of a talent of pure gold made he it, and all the vessels thereof.
Akatengeneza kinara hicho cha taa pamoja na vifaa vyake vyote kutumia talanta moja ya dhahabu safi.
25 And he made the altar of incense of acacia-wood: a cubit was the length thereof, and a cubit the breadth thereof, four-square; and two cubits was the height thereof; the horns thereof were of one piece with it.
Akatengeneza madhabahu ya kufukizia uvumba kwa mbao za mshita. Ilikuwa ya mraba, urefu na upana wake dhiraa moja, na kimo cha dhiraa mbili, nazo pembe zake zilikuwa kitu kimoja nayo.
26 And he overlaid it with pure gold, the top thereof, and the sides thereof round about, and the horns of it; and he made unto it a crown of gold round about.
Akafunika hayo madhabahu juu na pande zote na pia zile pembe zake kwa dhahabu safi, na akayafanyizia ukingo wa dhahabu kuizunguka.
27 And he made for it two golden rings under the crown thereof, upon the two ribs thereof, upon the two sides of it, for holders for staves wherewith to bear it.
Akatengeneza pete mbili za dhahabu kwa ajili ya madhabahu chini ya huo ukingo, zikiwa mbili kila upande, za kushikilia hiyo mipiko iliyotumika kuyabebea madhabahu.
28 And he made the staves of acacia-wood, and overlaid them with gold.
Akatengeneza mipiko kwa miti ya mshita na kuifunika kwa dhahabu.
29 And he made the holy anointing oil, and the pure incense of sweet spices, after the art of the perfumer.
Pia akatengeneza mafuta matakatifu ya upako, na uvumba safi wenye harufu nzuri, kazi ya mtengeneza manukato.

< Exodus 37 >