< Exodus 33 >

1 And the LORD spoke unto Moses: 'Depart, go up hence, thou and the people that thou hast brought up out of the land of Egypt, unto the land of which I swore unto Abraham, to Isaac, and to Jacob, saying: Unto thy seed will I give it —
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Ondoka mahali hapa, wewe pamoja na hao watu uliowapandisha kutoka Misri, mpande mpaka nchi niliyomwahidi Abrahamu, Isaki na Yakobo kwa kiapo, nikisema, ‘Nitawapa wazao wenu nchi hii.’
2 and I will send an angel before thee; and I will drive out the Canaanite, the Amorite, and the Hittite, and the Perizzite, the Hivite, and the Jebusite —
Nitamtuma malaika mbele yenu, naye atawafukuza Wakanaani, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.
3 unto a land flowing with milk and honey; for I will not go up in the midst of thee; for thou art a stiffnecked people; lest I consume thee in the way.'
Pandeni mwende katika nchi itiririkayo maziwa na asali. Lakini mimi sitakwenda pamoja nanyi, kwa sababu ninyi ni watu wenye shingo ngumu, nisije nikawaangamiza njiani.”
4 And when the people heard these evil tidings, they mourned; and no man did put on him his ornaments.
Watu waliposikia habari hizo za huzuni, wakaanza kuomboleza wala hakuna mtu aliyevaa mapambo yoyote.
5 And the LORD said unto Moses: 'Say unto the children of Israel: Ye are a stiffnecked people; if I go up into the midst of thee for one moment, I shall consume thee; therefore now put off thy ornaments from thee, that I may know what to do unto thee.'
Kwa kuwa Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Waambie Waisraeli, ‘Ninyi ni watu wenye shingo ngumu. Kama ningefuatana nanyi hata kwa muda mfupi, ningewaangamiza. Sasa vueni mapambo yenu, nami nitaamua nitakalowatendea.’”
6 And the children of Israel stripped themselves of their ornaments from mount Horeb onward.
Hivyo Waisraeli wakavua mapambo yao katika Mlima wa Horebu.
7 Now Moses used to take the tent and to pitch it without the camp, afar off from the camp; and he called it The tent of meeting. And it came to pass, that every one that sought the LORD went out unto the tent of meeting, which was without the camp.
Basi Mose alikuwa na desturi ya kuchukua hema na kuliweka wakfu nje ya kambi umbali kiasi, akaliita “Hema la Kukutania.” Kila aliyekuwa akiulizia shauri kwa Bwana, angelikwenda katika Hema la Kukutania nje ya kambi.
8 And it came to pass, when Moses went out unto the Tent, that all the people rose up, and stood, every man at his tent door, and looked after Moses, until he was gone into the Tent.
Wakati wowote Mose alipokwenda kwenye Hema, watu wote waliinuka na kusimama kwenye maingilio ya mahema yao, wakimwangalia Mose mpaka aingie kwenye Hema.
9 And it came to pass, when Moses entered into the Tent, the pillar of cloud descended, and stood at the door of the Tent; and the LORD spoke with Moses.
Kila mara Mose alipoingia ndani ya hema, nguzo ya wingu ingeshuka chini na kukaa kwenye ingilio, wakati Mungu akizungumza na Mose.
10 And when all the people saw the pillar of cloud stand at the door of the Tent, all the people rose up and worshipped, every man at his tent door.
Kila mara watu walipoona hiyo nguzo ya wingu ikiwa imesimama kwenye ingilio la hema, wote walisimama wakaabudu, kila mmoja kwenye ingilio la hema lake.
11 And the LORD spoke unto Moses face to face, as a man speaketh unto his friend. And he would return into the camp; but his minister Joshua, the son of Nun, a young man, departed not out of the Tent.
Bwana angezungumza na Mose uso kwa uso, kama vile mtu azungumzavyo na rafiki yake. Kisha Mose angerudi kambini, lakini msaidizi wake kijana Yoshua mwana wa Nuni hakuondoka mle Hemani.
12 And Moses said unto the LORD: 'See, Thou sayest unto me: Bring up this people; and Thou hast not let me know whom Thou wilt send with me. Yet Thou hast said: I know thee by name, and thou hast also found grace in My sight.
Mose akamwambia Bwana, “Umekuwa ukiniambia, ‘Ongoza watu hawa,’ lakini hujanifahamisha ni nani utakayemtuma pamoja nami. Umesema, ‘Ninakujua wewe kwa jina lako, nawe umepata kibali mbele zangu.’
13 Now therefore, I pray Thee, if I have found grace in Thy sight, show me now Thy ways, that I may know Thee, to the end that I may find grace in Thy sight; and consider that this nation is Thy people.'
Ikiwa umependezwa nami, nifundishe njia zako ili nipate kukujua, nami nizidi kupata kibali mbele zako. Kumbuka kuwa taifa hili ni watu wako.”
14 And He said: 'My presence shall go with thee, and I will give thee rest.'
Bwana akajibu, “Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.”
15 And he said unto Him: 'If Thy presence go not with me, carry us not up hence.
Kisha Mose akamwambia, “Kama Uso wako hauendi pamoja nasi, usituondoe hapa.
16 For wherein now shall it be known that I have found grace in Thy sight, I and Thy people? is it not in that Thou goest with us, so that we are distinguished, I and Thy people, from all the people that are upon the face of the earth?'
Mtu yeyote atajuaje kuwa mimi pamoja na watu wako tumepata kibali mbele zako, usipokwenda pamoja nasi? Ni nini kingine kitakachoweza kututofautisha mimi na watu wako miongoni mwa watu wengine wote walio katika uso wa dunia?”
17 And the LORD said unto Moses: 'I will do this thing also that thou hast spoken, for thou hast found grace in My sight, and I know thee by name.'
Bwana akamwambia Mose, “Nitakufanyia jambo lile uliloomba, kwa sababu ninapendezwa nawe, nami ninakujua kwa jina lako.”
18 And he said: 'Show me, I pray Thee, Thy glory.'
Kisha Mose akasema, “Basi nionyeshe utukufu wako.”
19 And He said: 'I will make all My goodness pass before thee, and will proclaim the name of the LORD before thee; and I will be gracious to whom I will be gracious, and will show mercy on whom I will show mercy.'
Ndipo Bwana akasema, “Nitapitisha wema wangu wote mbele yako, nami nitalitangaza Jina langu, Bwana, mbele ya uso wako. Nitamrehemu yeye nimrehemuye, na pia nitamhurumia yeye nimhurumiaye.”
20 And He said: 'Thou canst not see My face, for man shall not see Me and live.'
Lakini Mungu akasema, “Hutaweza kuuona uso wangu, kwa kuwa hakuna mtu yeyote awezaye kuniona akaishi.”
21 And the LORD said: 'Behold, there is a place by Me, and thou shalt stand upon the rock.
Kisha Bwana akasema, “Kuna mahali karibu nami ambapo unaweza kusimama juu ya mwamba.
22 And it shall come to pass, while My glory passeth by, that I will put thee in a cleft of the rock, and will cover thee with My hand until I have passed by.
Utukufu wangu unapopita, nitakuweka gengeni kwenye mwamba na kukufunika kwa mkono wangu mpaka nitakapokwisha kupita.
23 And I will take away My hand, and thou shalt see My back; but My face shall not be seen.'
Kisha nitaondoa mkono wangu nawe utaona mgongo wangu; lakini kamwe uso wangu hautaonekana.”

< Exodus 33 >