< Exodus 26 >

1 Moreover thou shalt make the tabernacle with ten curtains: of fine twined linen, and blue, and purple, and scarlet, with cherubim the work of the skilful workman shalt thou make them.
“Tengeneza maskani kwa mapazia kumi ya kitani iliyosokotwa vizuri na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, naye fundi stadi atatarizi makerubi kwenye mapazia hayo.
2 The length of each curtain shall be eight and twenty cubits, and the breadth of each curtain four cubits; all the curtains shall have one measure.
Mapazia yote yatatoshana kwa ukubwa: kila moja litakuwa na urefu wa dhiraa ishirini na nane, na upana wa dhiraa nne
3 Five curtains shall be coupled together one to another; and the other five curtains shall be coupled one to another.
Unganisha mapazia matano pamoja; fanya vivyo hivyo kwa hayo mengine matano.
4 And thou shalt make loops of blue upon the edge of the one curtain that is outmost in the first set; and likewise shalt thou make in the edge of the curtain that is outmost in the second set.
Tengeneza vitanzi vya kitambaa cha buluu kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu la kwanza, na ufanye vivyo hivyo na pazia la fungu la mwisho.
5 Fifty loops shalt thou make in the one curtain, and fifty loops shalt thou make in the edge of the curtain that is in the second set; the loops shall be opposite one to another.
Fanya vitanzi hamsini katika pazia mmoja, na vitanzi vingine hamsini kwenye pazia la mwisho la fungu hilo lingine, nazo vitanzi vyote vielekeane.
6 And thou shalt make fifty clasps of gold, and couple the curtains one to another with the clasps, that the tabernacle may be one whole.
Kisha tengeneza vifungo hamsini vya dhahabu ili vitumike kufunga na kuunganisha mapazia pamoja kufanya Hema liwe kitu kimoja.
7 And thou shalt make curtains of goats' hair for a tent over the tabernacle; eleven curtains shalt thou make them.
“Tengeneza mapazia kumi na moja ya singa za mbuzi kwa ajili ya kufunika maskani.
8 The length of each curtain shall be thirty cubits, and the breadth of each curtain four cubits; the eleven curtains shall have one measure.
Mapazia hayo kumi na moja yatakuwa na kipimo kimoja, yaani urefu wa dhiraa thelathini, na upana wa dhiraa nne.
9 And thou shalt couple five curtains by themselves, and six curtains by themselves, and shalt double over the sixth curtain in the forefront of the tent.
Unganisha hayo mapazia matano yawe fungu moja, na hayo mengine sita yawe fungu lingine. Kunja hilo pazia la sita mara mbili mbele ya maskani.
10 And thou shalt make fifty loops on the edge of the one curtain that is outmost in the first set, and fifty loops upon the edge of the curtain which is outmost in the second set.
Tengeneza vitanzi hamsini kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu moja, na vivyo hivyo kwenye upindo wa pazia la mwisho la fungu hilo lingine.
11 And thou shalt make fifty clasps of brass, and put the clasps into the loops, and couple the tent together, that it may be one.
Kisha tengeneza vifungo hamsini vya shaba, uviingize katika vile vitanzi ili kukaza hema pamoja kuwa kitu kimoja.
12 And as for the overhanging part that remaineth of the curtains of the tent, the half curtain that remaineth over shall hang over the back of the tabernacle.
Kuhusu kile kipande cha ziada cha pazia la Hema, nusu ya hilo pazia lililobaki litaningʼinizwa upande wa nyuma wa Hema.
13 And the cubit on the one side, and the cubit on the other side, of that which remaineth over in the length of the curtains of the tent, shall hang over the sides of the tabernacle on this side and on that side, to cover it.
Mapazia ya hema yatakuwa na urefu wa dhiraa moja zaidi pande zote, sehemu itakayobaki itaningʼinia pande zote za Hema ili kuifunika.
14 And thou shalt make a covering for the tent of rams' skins dyed red and a covering of sealskins above.
Tengeneza kifuniko cha hema kwa ngozi za kondoo dume zilizotiwa rangi nyekundu, na juu yake kifuniko cha ngozi za pomboo.
15 And thou shalt make the boards for the tabernacle of acacia-wood, standing up.
“Tengeneza mihimili ya kusimamisha ya mti wa mshita kwa ajili ya maskani.
16 Ten cubits shall be the length of a board, and a cubit and a half the breadth of each board.
Kila mhimili uwe na urefu wa dhiraa kumi na upana wa dhiraa moja na nusu,
17 Two tenons shall there be in each board, joined one to another; thus shalt thou make for all the boards of the tabernacle.
zikiwa na ndimi mbili zilizo sambamba kila mmoja na mwingine. Tengeneza mihimili yote ya maskani jinsi hii.
18 And thou shalt make the boards for the tabernacle, twenty boards for the south side southward:
Tengeneza mihimili ishirini kwa ajili ya upande wa kusini wa maskani,
19 And thou shalt make forty sockets of silver under the twenty boards: two sockets under one board for its two tenons, and two sockets under another board for its two tenons;
kisha tengeneza vitako arobaini vya fedha vya kuweka chini ya hiyo mihimili, vitako viwili kwa kila mhimili, kimoja chini ya kila ulimi.
20 and for the second side of the tabernacle, on the north side, twenty boards.
Kuhusu upande wa kaskazini wa maskani, tengeneza mihimili ishirini
21 And their forty sockets of silver: two sockets under one board, and two sockets under another board.
na vitako arobaini vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
22 And for the hinder part of the tabernacle westward thou shalt make six boards.
Kisha tengeneza mihimili sita kwa mwisho ulio mbali, yaani upande wa magharibi wa maskani,
23 And two boards shalt thou make for the corners of the tabernacle in the hinder part.
na pia utengeneze mihimili miwili ya pembe za upande ulio mbali.
24 And they shall be double beneath, and in like manner they shall be complete unto the top thereof unto the first ring; thus shall it be for them both; they shall be for the two corners.
Katika pembe hizi mbili ni lazima mihimili yake iwe miwili kuanzia chini mpaka juu, na iingizwe kwenye pete moja; mihimili ya pembe hizi mbili itafanana.
25 Thus there shall be eight boards, and their sockets of silver, sixteen sockets: two sockets under one board, and two sockets under another board.
Kwa hiyo itakuwepo mihimili minane, na vitako kumi na sita vya fedha, viwili chini ya kila mhimili.
26 And thou shalt make bars of acacia-wood: five for the boards of the one side of the tabernacle,
“Pia tengeneza mataruma ya mti wa mshita: matano kwa ajili ya mihimili ya upande mmoja wa maskani,
27 and five bars for the boards of the other side of the tabernacle, and five bars for the boards of the side of the tabernacle, for the hinder part westward;
matano kwa ajili ya mihimili ya upande mwingine, na matano kwa ajili ya mihimili ya upande wa magharibi, mwisho kabisa mwa maskani.
28 and the middle bar in the midst of the boards, which shall pass through from end to end.
Taruma la katikati litapenya katikati ya mihimili kutoka mwisho mmoja hadi mwisho mwingine.
29 And thou shalt overlay the boards with gold, and make their rings of gold for holders for the bars; and thou shalt overlay the bars with gold.
Funika hiyo mihimili kwa dhahabu, kisha tengeneza pete za dhahabu ambazo zitashikilia hayo mataruma. Pia funika hayo mataruma kwa dhahabu.
30 And thou shalt rear up the tabernacle according to the fashion thereof which hath been shown thee in the mount.
“Simamisha Hema sawasawa na mfano ulioonyeshwa kule mlimani.
31 And thou shalt make a veil of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen; with cherubim the work of the skilful workman shall it be made.
“Tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, naye fundi stadi atirizi makerubi kwenye hilo pazia.
32 And thou shalt hang it upon four pillars of acacia overlaid with gold, their hooks being of gold, upon four sockets of silver.
Litundike kwa kulabu za dhahabu kwenye nguzo nne za mti wa mshita ambazo zimefunikwa kwa dhahabu, zikiwa zimesimamishwa kwenye vitako vinne vya fedha.
33 And thou shalt hang up the veil under the clasps, and shalt bring in thither within the veil the ark of the testimony; and the veil shall divide unto you between the holy place and the most holy.
Ningʼiniza pazia hilo kwenye vifungo, kisha weka Sanduku la Ushuhuda nyuma ya pazia. Pazia litatenganisha Mahali Patakatifu kutoka Patakatifu pa Patakatifu.
34 And thou shalt put the ark-cover upon the ark of the testimony in the most holy place.
Weka kifuniko cha kiti cha rehema juu ya Sanduku la Ushuhuda ndani ya Patakatifu pa Patakatifu.
35 And thou shalt set the table without the veil, and the candlestick over against the table on the side of the tabernacle toward the south; and thou shalt put the table on the north side.
Weka meza nje ya pazia upande wa kaskazini wa Hema, kisha weka kinara cha taa upande wa kusini wa Hema.
36 And thou shalt make a screen for the door of the Tent, of blue, and purple, and scarlet, and fine twined linen, the work of the weaver in colours.
“Kwa ajili ya ingilio la hema, tengeneza pazia la nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi iliyosokotwa vizuri, kazi ya mtarizi.
37 And thou shalt make for the screen five pillars of acacia, and overlay them with gold; their hooks shall be of gold; and thou shalt cast five sockets of brass for them.
Tengeneza kulabu za dhahabu kwa ajili ya hilo pazia, na nguzo tano za mshita zilizofunikwa kwa dhahabu. Kisha mimina vitako vitano vya shaba kwa ajili yake.

< Exodus 26 >