< Exodus 2 >

1 And there went a man of the house of Levi, and took to wife a daughter of Levi.
Sasa mwanamme wa kabila la Lawi alimuoa mwanamke Mlawi.
2 And the woman conceived, and bore a son; and when she saw him that he was a goodly child, she hid him three months.
Yule mwanamke akapata mimba na kuzaa mtoto wa kiume. Alipoona ya kuwa alikuwa mtoto mwenye afaya, alimficha kwa miezi mitatu.
3 And when she could not longer hide him, she took for him an ark of bulrushes, and daubed it with slime and with pitch; and she put the child therein, and laid it in the flags by the river's brink.
Lakini alipokuwa hawezi kuendelea kumficha tena, alichukua kikapu cha manyasi akakipaka sifa na lami. Akamtia mtoto ndani yake na kukiweka juu ya maji katika majani kando ya mto.
4 And his sister stood afar off, to know what would be done to him.
Dada yake akasimama kwa mbali ili ajue yatakayompata.
5 And the daughter of Pharaoh came down to bathe in the river; and her maidens walked along by the river-side; and she saw the ark among the flags, and sent her handmaid to fetch it.
Binti Farao akashuka kuoga mtoni wakati vijakazi wake wakitembea kando ya mto. Naye akaona kile kikapu katika majani na akamtuma kijakazi wake kwenda kukileta.
6 And she opened it, and saw it, even the child; and behold a boy that wept. And she had compassion on him, and said: 'This is one of the Hebrews' children.'
Alipokifungua, aliomwona mtoto. Tazama, mtoto alikuwa analia. Alimhurumia na kusema, “Bila shaka huyu ni mmoja wapo wa watoto wa Waebrania.”
7 Then said his sister to Pharaoh's daughter: 'Shall I go and call thee a nurse of the Hebrew women, that she may nurse the child for thee?'
Basi dada wa yule mtoto akamwambia binti Farao, “Je naweza kwenda kukutafutia mwanamke wa Kiebrania aje akulele mtoto kwa ajili yako?”
8 And Pharaoh's daughter said to her: 'Go.' And the maiden went and called the child's mother.
Binti Farao akamwambia, “Nenda.” Hivyo yule binti akaenda na kumwita mama yake yule mtoto.
9 And Pharaoh's daughter said unto her: 'Take this child away, and nurse it for me, and I will give thee thy wages.' And the woman took the child, and nursed it.
Binti Farao akamwambia mama yake yule mtoto, “Mchukue mtoto huyu ukaninyonyeshee, nami nitakupa posho.” Hivyo yule mwanamke akamchukua mtoto na kumnyonyesha.
10 And the child grew, and she brought him unto Pharaoh's daughter, and he became her son. And she called his name Moses, and said: 'Because I drew him out of the water.'
Mtoto alipokuwa mkubwa, akamleta kwa binti Farao, na akawa mtoto wake. Akamwita jina lake Musa akisema, “Kwa sababu nilimtoa katika maji.”
11 And it came to pass in those days, when Moses was grown up, that he went out unto his brethren, and looked on their burdens; and he saw an Egyptian smiting a Hebrew, one of his brethren.
Musa alipokuwa mtu mzima, alienda kwa watu wake na kuona kazi ngumu walizokuwa wanafanya. Alimuona Mmisri akimpiga Mwebrania, mmoja wa watu wa jamii yake.
12 And he looked this way and that way, and when he saw that there was no man, he smote the Egyptian, and hid him in the sand.
Aliangalia huku na kule, na alipoona ya kuwa hakuna mtu, alimuua yule mmisri na kuuficha mwili wake katika mchanga.
13 And he went out the second day, and, behold, two men of the Hebrews were striving together; and he said to him that did the wrong: 'Wherefore smitest thou thy fellow?'
Alienda tena siku iliyofuata, na tazama, Waebrania wawili walikuwa wanapigana. Alimwambia yule aliyekuwa na makosa, “Kwa nini unampigia mwenzako?”
14 And he said: 'Who made thee a ruler and a judge over us? thinkest thou to kill me, as thou didst kill the Egyptian?' And Moses feared, and said: 'Surely the thing is known.'
Lakini yule mtu alisema, “Ni nani aliyekuweka wewe kuwa kiongozi na mwamuzi juu yetu? Unataka kuniua na mimi kama ulivyomuua yule mmisri?” Ndipo Musa akaogopa na kusema, “Hakika niliyoyafanya yamejulikana.”
15 Now when Pharaoh heard this thing, he sought to slay Moses. But Moses fled from the face of Pharaoh, and dwelt in the land of Midian; and he sat down by a well.
Farao aliposikia habari hizi, alijaribu kumuua Musa. Lakini Musa alikimbia na kwenda kuishi katika nchi ya Wamidiani. Kule alikaa chini kando ya mto.
16 Now the priest of Midian had seven daughters; and they came and drew water, and filled the troughs to water their father's flock.
Wakati huo kuhani wa Midiani alikuwa na mabinti saba. Walikuja mtoni kuchota maji na kujaza vyombo vyao ili wawanyweshe mifuko ya baba yao.
17 And the shepherds came and drove them away; but Moses stood up and helped them, and watered their flock.
Wachungaji walikuja na kutaka kuwafukuza, lakini Musa alienda kuwasaidia. Kisha akawanywesha mifugo wao.
18 And when they came to Reuel their father, he said: 'How is it that ye are come so soon to-day?'
Wale mabinti walipoenda kwa Reueli baba yao, aliwauliza, “Kwa nini mmerudi nyumbani mapema hivi leo?”
19 And they said: 'An Egyptian delivered us out of the hand of the shepherds, and moreover he drew water for us, and watered the flock.'
Wakamwambia, “Mmisri mmoja alituokoa dhidi ya wachungaji. Pia alichota maji na kuwanywesha mifugo wetu.”
20 And he said unto his daughters: 'And where is he? Why is it that ye have left the man? call him, that he may eat bread.'
Kisha akawauliza binti zake, “Yu wapi sasa? Kwa nini mlimwacha? Mwiteni ili apate kula chakula pamoja nasi.”
21 And Moses was content to dwell with the man; and he gave Moses Zipporah his daughter.
Musa akakubali kukaa na yule mtu ambaye pia alimpa binti yake Zipora ili amuoe.
22 And she bore a son, and he called his name Gershom; for he said: 'I have been a stranger in a strange land.'
Alizaa mtoto wa kiume, na Musa akamwita jina lake Geshomu; akisema; “Nimekuwa mkazi katika nchi ya ugeni.”
23 And it came to pass in the course of those many days that the king of Egypt died; and the children of Israel sighed by reason of the bondage, and they cried, and their cry came up unto God by reason of the bondage.
Muda mrefu baadaye, mfalme wa Misri akafa. Waisraeli walilalamika kwa sababu ya kazi za utumwa. Walilia kutafuta msaada, na maombi yao yakamfikia Mungu kwa sababu ya mateso yao.
24 And God heard their groaning, and God remembered His covenant with Abraham, with Isaac, and with Jacob.
Mungu aliposikia malalamiko yao, Mungu alikumbuka agano lake na Abrahamu, na Isaka, na Yakobo.
25 And God saw the children of Israel, and God took cognizance of them.
Mungu aliwaona Waisraeli na akaielewa hali yao.

< Exodus 2 >