< Ecclesiastes 12 >

1 Remember then thy Creator in the days of thy youth, before the evil days come, and the years draw nigh, when thou shalt say: 'I have no pleasure in them';
Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijaja siku za taabu, wala haijakaribia miaka utakaposema, “Mimi sifurahii hiyo”:
2 Before the sun, and the light, and the moon, and the stars, are darkened, and the clouds return after the rain;
kabla jua na nuru, nao mwezi na nyota havijatiwa giza, kabla ya kurudi mawingu baada ya mvua;
3 In the day when the keepers of the house shall tremble, and the strong men shall bow themselves, and the grinders cease because they are few, and those that look out shall be darkened in the windows,
siku ile walinzi wa nyumba watakapotetemeka, nao watu wenye nguvu watakapojiinamisha, wakati wasagao watakapokoma kwa sababu ya uchache, nao wachunguliao madirishani kutiwa giza;
4 And the doors shall be shut in the street, when the sound of the grinding is low; and one shall start up at the voice of a bird, and all the daughters of music shall be brought low;
wakati milango ya kuingia barabarani itakapofungwa na sauti ya kusaga kufifia; wakati watu wataamshwa kwa sauti ya ndege, lakini nyimbo zao zote zikififia;
5 Also when they shall be afraid of that which is high, and terrors shall be in the way; and the almond-tree shall blossom, and the grasshopper shall drag itself along, and the caperberry shall fail; because man goeth to his long home, and the mourners go about the streets;
wakati watu watakapoogopa kilichoinuka juu na hatari zitakazokuwepo barabarani; wakati mlozi utakapochanua maua na panzi kujikokota nawe usiwe na shauku ya kitu chochote. Ndipo mwanadamu aiendea nyumba yake ya milele nao waombolezaji wakizunguka barabarani.
6 Before the silver cord is snapped asunder, and the golden bowl is shattered, and the pitcher is broken at the fountain, and the wheel falleth shattered, into the pit;
Mkumbuke Muumba wako: kabla haijakatika kamba ya fedha, au bakuli la dhahabu halijavunjika; kabla mtungi kuvunjika kwenye chemchemi, au gurudumu kuvunjika kisimani,
7 And the dust returneth to the earth as it was, and the spirit returneth unto God who gave it.
nayo mavumbi kurudi ardhini yalikotoka, na roho kurudi kwa Mungu aliyeitoa.
8 Vanity of vanities, saith Koheleth; all is vanity.
Mhubiri asema, “Ubatili! Ubatili! Kila kitu ni ubatili!”
9 And besides that Koheleth was wise, he also taught the people knowledge; yea, he pondered, and sought out, and set in order many proverbs.
Mhubiri hakuwa tu na hekima, bali aliwagawia watu maarifa pia. Alitafakari na kutafiti na akaweka katika utaratibu mithali nyingi.
10 Koheleth sought to find out words of delight, and that which was written uprightly, even words of truth.
Mhubiri alitafiti ili kupata maneno sahihi na kila alichoandika kilikuwa sawa na kweli.
11 The words of the wise are as goads, and as nails well fastened are those that are composed in collections; they are given from one shepherd.
Maneno ya wenye hekima ni kama mchokoro, mithali zao zilizokusanywa pamoja ni kama misumari iliyogongomewa ikawa imara, yaliyotolewa na Mchungaji mmoja.
12 And furthermore, my son, be admonished: of making many books there is no end; and much study is a weariness of the flesh.
Tena zaidi ya hayo, mwanangu, kubali maonyo, hakuna mwisho wa kutunga vitabu vingi, nako kusoma sana huuchosha mwili.
13 The end of the matter, all having been heard: fear God, and keep His commandments; for this is the whole man.
Hii ndiyo jumla ya maneno; yote yamekwisha sikiwa: Mche Mungu, nawe uzishike amri zake, maana kwa jumla ndiyo impasayo mtu.
14 For God shall bring every work into the judgment concerning every hidden thing, whether it be good or whether it be evil.
Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la siri, likiwa jema au baya.

< Ecclesiastes 12 >