< Deuteronomy 14 >

1 Ye are the children of the LORD your God: ye shall not cut yourselves, nor make any baldness between your eyes for the dead.
Ninyi ni watoto wa Bwana Mungu wenu. Msijichanje ama kujinyoa upara kwenye paji la uso kwa ajili ya aliyekufa,
2 For thou art a holy people unto the LORD thy God, and the LORD hath chosen thee to be His own treasure out of all peoples that are upon the face of the earth.
kwa maana ninyi ni taifa takatifu kwa Bwana Mungu wenu. Bwana amewachagua ninyi kuwa taifa la kipekee kutoka mataifa yote juu ya uso wa dunia, mwe tunu yake.
3 Thou shalt not eat any abominable thing.
Msile kitu chochote ambacho ni machukizo.
4 These are the beasts which ye may eat: the ox, the sheep, and the goat,
Hawa ndio wanyama mtakaokula: ngʼombe, kondoo, mbuzi,
5 the hart, and the gazelle, and the roebuck, and the wild goat, and the pygarg, and the antelope, and the mountain-sheep.
kulungu, paa, kongoni, paa mweupe, mbuzi-mwitu, pofu na kondoo wa mlimani.
6 And every beast that parteth the hoof, and hath the hoof wholly cloven in two, and cheweth the cud, among the beasts, that ye may eat.
Mnaweza kumla mnyama yeyote mwenye kwato zilizogawanyika mara mbili, pia yule anayecheua.
7 Nevertheless these ye shall not eat of them that only chew the cud, or of them that only have the hoof cloven: the camel, and the hare, and the rock-badger, because they chew the cud but part not the hoof, they are unclean unto you;
Hata hivyo, miongoni mwa wale wanaocheua au wale walio na kwato zilizogawanyika kamwe msile ngamia, sungura na pelele. Iwapo wanacheua, lakini hawana kwato zilizogawanyika; ni najisi kwenu kwa taratibu za kiibada.
8 and the swine, because he parteth the hoof but cheweth not the cud, he is unclean unto you; of their flesh ye shall not eat, and their carcasses ye shall not touch.
Nguruwe pia ni najisi; ingawa ana kwato zilizogawanyika, hacheui. Msile nyama yake wala kugusa mzoga wake.
9 These ye may eat of all that are in the waters: whatsoever hath fins and scales may ye eat;
Katika viumbe hai vyote viishivyo kwenye maji, mnaweza kula yeyote aliye na mapezi na magamba.
10 and whatsoever hath not fins and scales ye shall not eat; it is unclean unto you.
Lakini chochote kisicho na mapezi na magamba msile; kwenu ni najisi.
11 Of all clean birds ye may eat.
Mnaweza kula ndege yeyote aliye safi.
12 But these are they of which ye shall not eat: the great vulture, and the bearded vulture, and the ospray;
Lakini wafuatao msiwale: tai, furukombe, kipungu,
13 and the glede, and the falcon, and the kite after its kinds;
kengewa mwekundu, kengewa mweusi, mwewe wa aina yoyote,
14 and every raven after its kinds;
kunguru wa aina yoyote,
15 and the ostrich, and the night-hawk, and the sea-mew, and the hawk after its kinds;
mbuni, kiruka-njia, dudumizi, kipanga wa aina yoyote,
16 the little owl, and the great owl, and the horned owl;
bundi, mumbi, bundi mkubwa,
17 and the pelican, and the carrion-vulture, and the cormorant;
mwari, nderi, mnandi,
18 and the stork, and the heron after its kinds, and the hoopoe, and the bat.
korongo, koikoi wa aina yoyote, hudihudi na popo.
19 And all winged swarming things are unclean unto you; they shall not be eaten.
Wadudu wote warukao kwa makundi ni najisi kwenu, msiwale.
20 Of all clean winged things ye may eat.
Lakini viumbe vyote vyenye mabawa vilivyo safi mwaweza kula.
21 Ye shall not eat of any thing that dieth of itself; thou mayest give it unto the stranger that is within thy gates, that he may eat it; or thou mayest sell it unto a foreigner; for thou art a holy people unto the LORD thy God. Thou shalt not seethe a kid in its mother's milk.
Msile kitu chochote mtakachokuta kimekufa. Mnaweza kumpa mgeni yeyote anayeishi katika mojawapo ya miji yenu, naye anaweza kula au mnaweza kumuuzia mtu wa nchi nyingine. Lakini ninyi ni watu watakatifu kwa Bwana Mungu wenu. Msitokose mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.
22 Thou shalt surely tithe all the increase of thy seed, that which is brought forth in the field year by year.
Hakikisheni mmetenga sehemu ya kumi ya mazao yote ya mashamba yenu kila mwaka.
23 And thou shalt eat before the LORD thy God, in the place which He shall choose to cause His name to dwell there, the tithe of thy corn, of thy wine, and of thine oil, and the firstlings of thy herd and of thy flock; that thou mayest learn to fear the LORD thy God always.
Mtakula zaka za nafaka yenu, divai mpya, mafuta na wazaliwa wa kwanza wa makundi yenu ya ngʼombe na ya kondoo na mbuzi mbele za Bwana Mungu wenu pale mahali atakapopachagua kama maskani kwa ajili ya Jina lake, ili kwamba mpate kujifunza kumheshimu Bwana Mungu wenu daima.
24 And if the way be too long for thee, so that thou art not able to carry it, because the place is too far from thee, which the LORD thy God shall choose to set His name there, when the LORD thy God shall bless thee;
Lakini ikiwa mahali pale ni mbali sana nanyi mmebarikiwa na Bwana Mungu wenu na hamwezi kubeba zaka yenu (kwa sababu mahali pale Bwana atakapopachagua kuliweka Jina lake ni mbali sana),
25 then shalt thou turn it into money, and bind up the money in thy hand, and shalt go unto the place which the LORD thy God shall choose.
basi badilisheni zaka yenu kuwa fedha, mkaichukue hiyo fedha mwende nayo mahali Bwana Mungu wenu atakapopachagua.
26 And thou shalt bestow the money for whatsoever thy soul desireth, for oxen, or for sheep, or for wine, or for strong drink, or for whatsoever thy soul asketh of thee; and thou shalt eat there before the LORD thy God, and thou shalt rejoice, thou and thy household.
Tumieni hiyo fedha kununua chochote ukitakacho: ngʼombe, kondoo, divai au kinywaji chochote chenye chachu au chochote mnachotaka. Kisha ninyi na wa nyumbani mwenu mtaila mbele za Bwana Mungu wenu na kufurahi.
27 And the Levite that is within thy gates, thou shalt not forsake him; for he hath no portion nor inheritance with thee.
Msiache kuwajali Walawi waishio katika miji yenu, kwa kuwa hao hawana shamba wala urithi wao wenyewe.
28 At the end of every three years, even in the same year, thou shalt bring forth all the tithe of thine increase, and shall lay it up within thy gates.
Mwishoni mwa kila mwaka wa tatu, leteni zaka zote za mazao ya miaka ile na uyahifadhi kwenye miji yenu,
29 And the Levite, because he hath no portion nor inheritance with thee, and the stranger, and the fatherless, and the widow, that are within thy gates, shall come, and shall eat and be satisfied; that the LORD thy God may bless thee in all the work of thy hand which thou doest.
ili Walawi (ambao hawana mashamba wala urithi wao wenyewe) na wageni, yatima na wajane wanaoishi kwenye miji yenu wapate kuja kula na kushiba, ili Bwana Mungu wenu apate kuwabariki ninyi katika kazi zote za mikono yenu.

< Deuteronomy 14 >