< 2 Chronicles 6 >

1 Then spoke Solomon: The LORD hath said that He would dwell in the thick darkness.
Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene.
2 But I have built Thee a house of habitation, and a place for Thee to dwell in for ever.
Nimejenga Hekalu zuri kwa ajili yako, mahali pako pa kukaa milele.”
3 And the king turned his face, and blessed all the congregation of Israel; and all the congregation of Israel stood.
Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
4 And he said: 'Blessed be the LORD, the God of Israel, who spoke with His mouth unto David my father, and hath with His hands fulfilled it, saying:
Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mikono yake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
5 Since the day that I brought forth My people out of the land of Egypt, I chose no city out of all the tribes of Israel to build a house in, that My name might be there; neither chose I any man to be prince over My people Israel;
‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, wala sikumchagua mtu yeyote kuwa kiongozi wa watu wangu Israeli.
6 but I have chosen Jerusalem, that My name might be there; and have chosen David to be over My people Israel.
Lakini sasa nimeuchagua Yerusalemu ili Jina langu lipate kuwamo humo, na nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
7 Now it was in the heart of David my father to build a house for the name of the LORD, the God of Israel.
“Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
8 But the LORD said unto David my father: Whereas it was in thy heart to build a house for My name, thou didst well that it was in thy heart;
Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
9 nevertheless thou shalt not build the house, but thy son that shall come forth out of thy loins, he shall build the house for My name.
Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea Hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
10 And the LORD hath established His word that He spoke; for I am risen up in the room of David my father, and sit on the throne of Israel, as the LORD promised, and have built the house for the name of the LORD, the God of Israel.
“Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
11 And there have I set the ark, wherein is the covenant of the LORD, which He made with the children of Israel.'
Nimeliweka humo Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na watu wa Israeli.”
12 And he stood before the altar of the LORD in the presence of all the congregation of Israel, and spread forth his hands —
Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, naye akakunjua mikono yake.
13 for Solomon had made a brazen scaffold, of five cubits long, and five cubits broad, and three cubits high, and had set it in the midst of the court; and upon it he stood, and kneeled down upon his knees before all the congregation of Israel, and spread forth his hands toward heaven —
Basi Solomoni alikuwa ametengeneza jukwaa la shaba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano na kimo chake dhiraa tatu, naye akaliweka katikati ya ukumbi wa nje. Akapanda juu ya hilo jukwaa kisha akapiga magoti mbele ya kusanyiko lote la Israeli, akanyoosha mikono yake kwelekea mbinguni.
14 and he said: 'O LORD, the God of Israel, there is no God like Thee, in the heaven, or in the earth; who keepest covenant and mercy with Thy servants, that walk before Thee with all their heart;
Akasema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
15 who hast kept with Thy servant David my father that which Thou didst promise him; yea, Thou spokest with Thy mouth, and hast fulfilled it with Thy hand, as it is this day.
Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
16 Now therefore, O LORD, the God of Israel, keep with Thy servant David my father that which Thou hast promised him, saying: There shall not fail thee a man in My sight to sit on the throne of Israel; if only thy children take heed to their way, to walk in My law as thou hast walked before Me.
“Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
17 Now therefore, O LORD, the God of Israel, let Thy word be verified, which Thou spokest unto Thy servant David.
Sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
18 But will God in very truth dwell with men on the earth? behold, heaven and the heaven of heavens cannot contain Thee; how much less this house which I have builded!
“Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani na wanadamu? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
19 Yet have Thou respect unto the prayer of Thy servant, and to his supplication, O LORD my God, to hearken unto the cry and to the prayer which Thy servant prayeth before Thee;
Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
20 that Thine eyes may be open toward this house day and night, even toward the place whereof Thou hast said that thou wouldest put Thy name there; to hearken unto the prayer which Thy servant shall pray toward this place.
Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
21 And hearken Thou to the supplications of Thy servant, and of Thy people Israel, when they shall pray toward this place; yea, hear Thou from Thy dwelling-place, even from heaven; and when Thou hearest, forgive.
Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
22 If a man sin against his neighbour, and an oath be exacted of him to cause him to swear, and he come and swear before Thine altar in this house;
“Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
23 then hear Thou from heaven, and do, and judge Thy servants, requiting the wicked, to bring his way upon his own head; and justifying the righteous, to give him according to his righteousness.
basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimwadhibu yule mwenye hatia kwa kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
24 And if Thy people Israel be smitten down before the enemy, when they sin against Thee, and shall turn again and confess Thy name, and pray and make supplication before Thee in this house;
“Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
25 then hear Thou from heaven, and forgive the sin of Thy people Israel, and bring them back unto the land which Thou gavest to them and to their fathers.
basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
26 When the heaven is shut up, and there is no rain, when they sin against Thee; if they pray toward this place, and confess Thy name, turning from their sin, when Thou dost afflict them;
“Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
27 then hear Thou in heaven, and forgive the sin of Thy servants, and of Thy people Israel, when Thou dost direct them on the good way wherein they should walk; and send rain upon Thy land, which Thou hast given to Thy people for an inheritance.
basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
28 If there be in the land famine, if there be pestilence, if there be blasting or mildew, locust or caterpillar; if their enemies besiege them in the land of their cities; whatsoever plague or whatsoever sickness there be;
“Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
29 what prayer and supplication soever be made by any man, or by all Thy people Israel, who shall know every man his own plague and his own pain, and shall spread forth his hands toward this house;
wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu zake na uchungu wake, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili,
30 then hear Thou from heaven Thy dwelling-place, and forgive, and render unto every man according to all his ways, whose heart Thou knowest — for Thou, even Thou only, knowest the hearts of the children of men —
basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
31 that they may fear Thee, to walk in Thy ways, all the days that they live in the land which Thou gavest unto our fathers.
ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
32 Moreover concerning the stranger, that is not of Thy people Israel, when be shall come out of a far country for Thy great name's sake, and Thy mighty hand, and Thine outstretched arm; when they shall come and pray toward this house;
“Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako kuu na mkono wako wenye nguvu ulionyooshwa, atakapokuja kuomba kuelekea Hekalu hili,
33 then hear Thou from heaven, even from Thy dwelling-place, and do according to all that the stranger calleth to Thee for; that all the peoples of the earth may know Thy name, and fear Thee, as doth Thy people Israel, and that they may know that Thy name is called upon this house which I have built.
basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
34 If Thy people go out to battle against their enemies, by whatsoever way Thou shalt send them, and they pray unto Thee toward this city which Thou hast chosen, and the house which I have built for Thy name;
“Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
35 then hear Thou from heaven their prayer and their supplication, and maintain their cause.
basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
36 If they sin against Thee — for there is no man that sinneth not — and Thou be angry with them, and deliver them to the enemy, so that they carry them away captive unto a land far off or near;
“Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi iliyo mbali au karibu
37 yet if they shall bethink themselves in the land whither they are carried captive, and turn, and make supplication unto Thee in the land of their captivity, saying: We have sinned, we have done iniquitously, and have dealt wickedly;
na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya utumwa na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa na tumetenda uovu’;
38 if they return unto Thee with all their heart and with all their soul in the land of their captivity, whither they have carried them captive, and pray toward their land, which Thou gavest unto their fathers, and the city which Thou hast chosen, and toward the house which I have built for Thy name;
kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
39 then hear Thou from heaven, even from Thy dwelling-place, their prayer and their supplications, and maintain their cause; and forgive Thy people who have sinned against Thee.
basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao. Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako.
40 Now, O my God, let, I beseech Thee, Thine eyes be open, and let Thine ears be attent, unto the prayer that is made in this place.
“Sasa, Mungu wangu, macho yako na yafumbuke na masikio yako yasikie maombi yaombwayo mahali hapa.
41 Now therefore arise, O LORD God, into Thy resting-place, Thou, and the ark of Thy strength; let Thy priests, O LORD God, be clothed with salvation, and let Thy saints rejoice in good.
“Sasa inuka, Ee Bwana Mungu,
42 O LORD God, turn not away the face of Thine anointed; remember the good deeds of David Thy servant.'
Ee Bwana Mungu, usimkatae

< 2 Chronicles 6 >