< 2 Chronicles 12 >

1 And it came to pass, when the kingdom of Rehoboam was established, and he was strong, that he forsook the law of the LORD, and all Israel with him.
Baada ya nafasi ya Rehoboamu kuimarika na kuwa na nguvu, yeye na Israeli yote waliiacha sheria ya Bwana Mungu.
2 And it came to pass in the fifth year of king Rehoboam, that Shishak king of Egypt came up against Jerusalem, because they had dealt treacherously with the LORD,
Kwa sababu hawakuwa waaminifu kwa Bwana, Shishaki mfalme wa Misri akashambulia Yerusalemu katika mwaka wa tano wa utawala wa Mfalme Rehoboamu.
3 with twelve hundred chariots, and threescore thousand horsemen; and the people were without number that came with him out of Egypt; the Lubim, the Sukkiim, and the Ethiopians.
Akiwa na magari ya vita 1,200 na wapanda farasi 60,000 na idadi isiyohesabika ya majeshi ya Walibia, Wasukii na Wakushi yaliyokuja pamoja naye kutoka Misri.
4 And he took the fortified cities which pertained to Judah, and came unto Jerusalem.
Akateka miji ya Yuda yenye ngome akaendelea mpaka Yerusalemu.
5 Now Shemaiah the prophet came to Rehoboam, and to the princes of Judah, that were gathered together to Jerusalem because of Shishak, and said unto them: 'Thus saith the LORD: Ye have forsaken Me, therefore have I also left you in the hand of Shishak.'
Ndipo nabii Shemaya akaja kwa Rehoboamu na kwa viongozi wa Yuda waliokuwa wamekusanyika huko Yerusalemu kwa ajili ya hofu ya Shishaki naye akawaambia, “Hivi ndivyo asemavyo Bwana, ‘Ninyi mmeniacha mimi, kwa hiyo, mimi nami sasa ninawaacha ninyi mkononi mwa Shishaki.’”
6 Then the princes of Israel and the king humbled themselves; and they said: 'The LORD is righteous.'
Viongozi wa Israeli na mfalme wakajinyenyekeza na kusema, “Bwana Mungu ni mwenye haki.”
7 And when the LORD saw that they humbled themselves, the word of the LORD came to Shemaiah, saying: 'They have humbled themselves; I will not destroy them; but I will grant them some deliverance, and My wrath shall not be poured out upon Jerusalem by the hand of Shishak.
Bwana Mungu alipoona kwamba wamejinyenyekeza, neno hili la Bwana likamjia Shemaya: “Maadamu wamejinyenyekeza, sitawaangamiza bali hivi karibuni nitawapatia wokovu. Ghadhabu yangu haitamwagwa juu ya Yerusalemu kwa kupitia Shishaki.
8 Nevertheless they shall be his servants; that they may know My service, and the service of the kingdoms of the countries.'
Hata hivyo, watamtumikia Shishaki ili wapate kujifunza tofauti kati ya kunitumikia mimi na kuwatumikia wafalme wa nchi nyingine.”
9 So Shishak king of Egypt came up against Jerusalem, and took away the treasures of the house of the LORD, and the treasures of the king's house; he took all away; he took away also the shields of gold which Solomon had made.
Shishaki mfalme wa Misri alipoishambulia Yerusalemu, alichukua hazina za Hekalu la Bwana na hazina za jumba la kifalme. Akachukua kila kitu, pamoja na zile ngao za dhahabu ambazo Solomoni alikuwa amezitengeneza.
10 And king Rehoboam made in their stead shields of brass, and committed them to the hands of the captains of the guard, that kept the door of the king's house.
Kwa hiyo Mfalme Rehoboamu akatengeneza ngao za shaba badala ya zile za dhahabu na kuzikabidhi kwa majemadari wa ulinzi wa zamu kwenye ingilio la jumba la mfalme.
11 And it was so, that as oft as the king entered into the house of the LORD, the guard came and bore them, and brought them back into the guard-chamber.
Kila wakati mfalme alipokwenda katika Hekalu la Bwana walinzi walikwenda pamoja naye wakiwa wamebeba hizo ngao na baadaye walizirudisha kwenye chumba cha ulinzi.
12 And when he humbled himself, the anger of the LORD turned from him, that He would not destroy him altogether; and moreover in Judah there were good things found.
Kwa sababu Rehoboamu alijinyenyekeza, hasira ya Bwana ikageukia mbali naye, hakuangamizwa kabisa. Kukawa na hali nzuri katika Yuda.
13 So king Rehoboam strengthened himself in Jerusalem, and reigned; for Rehoboam was forty and one years old when he began to reign, and he reigned seventeen years in Jerusalem, the city which the LORD had chosen out of all the tribes of Israel, to put His name there; and his mother's name was Naamah the Ammonitess.
Mfalme Rehoboamu akajiweka imara katika Yerusalemu na akaendelea kuwa mfalme. Alikuwa na umri wa miaka arobaini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na saba, mji ambao Bwana alikuwa ameuchagua miongoni mwa makabila yote ya Israeli ili aliweke Jina lake humo. Mama yake aliitwa Naama, alikuwa Mwamoni.
14 And he did that which was evil, because he set not his heart to seek the LORD.
Rehoboamu akatenda maovu kwa sababu hakuuelekeza moyo wake katika kumtafuta Bwana Mungu.
15 Now the acts of Rehoboam, first and last, are they not written in the histories of Shemaiah the prophet and of Iddo the seer, after the manner of genealogies? And there were wars between Rehoboam and Jeroboam continually.
Kwa habari ya matukio katika utawala wa Rehoboamu, tangu mwanzo mpaka mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Shemaya na mwonaji Ido zinazohusiana na vizazi? Kulikuwako na vita mara kwa mara kati ya Rehoboamu na Yeroboamu.
16 And Rehoboam slept with his fathers, and was buried in the city of David; and Abijah his son reigned in his stead.
Rehoboamu akalala na baba zake, akazikwa katika Mji wa Daudi. Naye Abiya mwanawe akawa mfalme baada yake.

< 2 Chronicles 12 >