< 1 Kings 22 >

1 And they continued three years without war between Aram and Israel.
Kwa miaka mitatu hapakuwa na vita kati ya Aramu na Israeli.
2 And it came to pass in the third year, that Jehoshaphat the king of Judah came down to the king of Israel.
Lakini katika mwaka wa tatu Yehoshafati mfalme wa Yuda akashuka kwenda kumwona mfalme wa Israeli.
3 And the king of Israel said unto his servants: 'Know ye that Ramoth-gilead is ours, and we are still, and take it not out of the hand of the king of Aram?'
Mfalme wa Israeli alikuwa amewaambia maafisa wake, “Je, hamjui Ramoth-Gileadi ni mali yetu na bado hatufanyi chochote kuirudisha kwetu kutoka kwa mfalme wa Aramu?”
4 And he said unto Jehoshaphat: 'Wilt thou go with me to battle to Ramoth-gilead?' And Jehoshaphat said to the king of Israel: 'I am as thou art, my people as thy people, my horses as thy horses.'
Kwa hiyo akamuuliza Yehoshafati, “Je, utakwenda pamoja nami kupigana dhidi ya Ramoth-Gileadi?” Yehoshafati akamjibu mfalme wa Israeli, “Mimi ni kama wewe, watu wangu ni kama watu wako, farasi wangu ni kama farasi wako.”
5 And Jehoshaphat said unto the king of Israel: 'Inquire, I pray thee, at the word of the LORD today.'
Lakini Yehoshafati pia akamwambia mfalme wa Israeli, “Kwanza tafuta shauri la Bwana.”
6 Then the king of Israel gathered the prophets together, about four hundred men, and said unto them: 'Shall I go against Ramoth-gilead to battle, or shall I forbear?' And they said: 'Go up; for the LORD will deliver it into the hand of the king.'
Kwa hiyo mfalme wa Israeli akawaleta pamoja manabii wanaume wapatao mia nne, akawauliza, “Je, niende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi, au niache?” Wakajibu, “Naam, nenda, kwa kuwa Bwana ataiweka Ramoth-Gileadi mkononi mwa mfalme.”
7 But Jehoshaphat said: 'Is there not here besides a prophet of the LORD, that we might inquire of him?'
Lakini Yehoshafati akauliza, “Je, hayuko nabii wa Bwana hapa ambaye tunaweza kumuuliza?”
8 And the king of Israel said unto Jehoshaphat: 'There is yet one man by whom we may inquire of the LORD, Micaiah the son of Imlah; but I hate him; for he doth not prophesy good concerning me, but evil.' And Jehoshaphat said: 'Let not the king say so.'
Mfalme wa Israeli akamjibu Yehoshafati, “Bado yupo mtu mmoja ambaye kupitia yeye twaweza kumuuliza shauri la Bwana, lakini namchukia kwa sababu huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu mimi, lakini kila mara hunitabiria mabaya tu. Yeye ni Mikaya mwana wa Imla.” Yehoshafati akajibu, “Mfalme hapaswi kusema hivyo.”
9 Then the king of Israel called an officer, and said: 'Fetch quickly Micaiah the son of Imlah.'
Kwa hiyo mfalme wa Israeli akamwita mmoja wa maafisa wake na kusema, “Mlete Mikaya mwana wa Imla mara moja.”
10 Now the king of Israel and Jehoshaphat the king of Judah sat each on his throne, arrayed in their robes, in a threshing-floor, at the entrance of the gate of Samaria; and all the prophets prophesied before them.
Wakiwa wamevalia majoho yao ya kifalme, mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda walikuwa wameketi juu ya viti vyao vya kifalme katika sakafu ya kupuria, kwenye ingilio la lango la Samaria, pamoja na manabii wote wakiwa wakitabiri mbele yao.
11 And Zedekiah the son of Chenaanah made him horns of iron, and said: 'Thus saith the LORD: With these shalt thou gore the Arameans, until they be consumed.'
Wakati huu Sedekia mwana wa Kenaana alikuwa ametengeneza pembe za chuma, akatangaza, “Hivi ndivyo Bwana asemavyo, ‘Kwa hizi pembe utawapiga na kuwarudisha Waaramu nyuma mpaka wameangamizwa.’”
12 And all the prophets prophesied so, saying: 'Go up to Ramoth-gilead, and prosper; for the LORD will deliver it into the hand of the king.'
Manabii wengine wote walikuwa wanatabiri kitu hicho hicho wakisema, “Ishambulie Ramoth-Gileadi na uwe mshindi. Kwa kuwa Bwana ataitia mkononi mwa mfalme.”
13 And the messenger that went to call Micaiah spoke unto him, saying: 'Behold now, the words of the prophets declare good unto the king with one mouth, let thy word, I pray thee, be like the word of one of them, and speak thou good.'
Mjumbe aliyekuwa amekwenda kumwita Mikaya akamwambia, “Tazama, manabii wote kama mtu mmoja wanatabiri ushindi kwa mfalme. Neno lako na likubaliane na lao, nawe unene mema kuhusu mfalme.”
14 And Micaiah said: 'As the LORD liveth, what the LORD saith unto me, that will I speak.'
Lakini Mikaya akasema, “Hakika kama Bwana aishivyo, nitamwambia kile tu Bwana atakachoniambia.”
15 And when he was come to the king, the king said unto him: 'Micaiah, shall we go to Ramoth-gilead to battle, or shall we forbear?' And he answered him: 'Go up, and prosper; and the LORD will deliver it into the hand of the king.'
Alipofika, mfalme akamuuliza, “Mikaya, je, twende vitani dhidi ya Ramoth-Gileadi au niache?” Akamjibu, “Shambulia na ushinde, kwa kuwa Bwana atawatia mkononi mwa mfalme.”
16 And the king said unto him: 'How many times shall I adjure thee that thou speak unto me nothing but the truth in the name of the LORD?'
Mfalme akamwambia, “Je, ni mara ngapi nitakuapisha ili usiniambie kitu chochote ila kweli tu kwa jina la Bwana?”
17 And he said: 'I saw all Israel scattered upon the mountains, as sheep that have no shepherd; and the LORD said: These have no master; let them return every man to his house in peace.'
Ndipo Mikaya akajibu, “Niliona Israeli wote wametawanyika vilimani kama kondoo wasio na mchungaji, naye Bwana akasema, ‘Watu hawa hawana bwana. Mwache kila mmoja aende nyumbani kwa amani.’”
18 And the king of Israel said to Jehoshaphat: 'Did I not tell thee that he would not prophesy good concerning me, but evil?'
Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Sikukuambia kwamba huwa hatabiri jambo lolote jema kunihusu, bali mabaya tu?”
19 And he said: 'Therefore hear thou the word of the LORD. I saw the LORD sitting on His throne, and all the host of heaven standing by Him on His right hand and on his left.
Mikaya akaendelea, “Kwa hiyo lisikie neno la Bwana: Nilimwona Bwana ameketi juu ya kiti chake cha enzi pamoja na jeshi lote la mbinguni likiwa limesimama kumzunguka upande wa kulia na wa kushoto.
20 And the LORD said: Who shall entice Ahab, that he may go up and fall at Ramoth-gilead. And one said: On this manner; and another said: On that manner.
Naye Bwana akasema, ‘Ni nani atakayemshawishi Ahabu ili aishambulie Ramoth-Gileadi na kukiendea kifo chake huko?’ “Mmoja akapendekeza hili na mwingine lile.
21 And there came forth the spirit, and stood before the LORD, and said: I will entice him.
Mwishoni, pepo mchafu akajitokeza, akasimama mbele za Bwana na kusema, ‘Nitamshawishi.’
22 And the LORD said unto him: Wherewith? And he said: I will go forth, and will be a lying spirit in the mouth of all his prophets. And He said: Thou shalt entice him, and shalt prevail also; go forth, and do so.
“Bwana akauliza, ‘Kwa njia gani?’ “Akasema, ‘Nitakwenda na kuwa roho ya uongo katika vinywa vya manabii wake wote.’ “Bwana akasema, ‘Utafanikiwa katika kumshawishi. Nenda ukafanye hivyo.’
23 Now therefore, behold, the LORD hath put a lying spirit in the mouth of all these thy prophets; and the LORD hath spoken evil concerning thee.'
“Kwa hiyo sasa Bwana ameweka roho ya kudanganya ndani ya vinywa vya hawa manabii wako wote. Bwana ameamuru maafa kwa ajili yako.”
24 Then Zedekiah the son of Chenaanah came near, and smote Micaiah on the check, and said: 'Which way went the spirit of the LORD from me to speak unto thee?'
Kisha Sedekia mwana wa Kenaana akatoka na kumpiga Mikaya kofi usoni. Akauliza, “Huyo Roho kutoka kwa Bwana alipita njia gani alipotoka kwangu ili kusema nawe?”
25 And Micaiah said: 'Behold, thou shalt see on that day, when thou shalt go into an inner chamber to hide thyself.'
Mikaya akajibu, “Utagundua siku hiyo utakapokwenda kujificha kwenye chumba cha ndani.”
26 And the king of Israel said: 'Take Micaiah, and carry him back unto Amon the governor of the city, and to Joash the king's son;
Kisha mfalme wa Israeli akaagiza, “Mchukueni na mkamrudishe kwa Amoni mtawala wa mji na kwa Yoashi mwana wa mfalme.
27 and say: Thus saith the king: Put this fellow in the prison, and feed him with scant bread and with scant water, until I come in peace.'
Mkaseme, ‘Hivi ndivyo asemavyo mfalme: Mwekeni mtu huyu gerezani na asipewe chochote ila mkate na maji mpaka nitakaporudi salama.’”
28 And Micaiah said: 'If thou return at all in peace, the LORD hath not spoken by me.' And he said: 'Hear, ye peoples, all of you.'
Mikaya akasema, “Kama utarudi salama, basi Bwana hajanena kupitia kwangu.” Kisha akaongeza kusema, “Zingatieni maneno yangu, enyi watu wote!”
29 So the king of Israel and Jehoshaphat the king of Judah went up to Ramoth-gilead.
Basi mfalme wa Israeli na Yehoshafati mfalme wa Yuda wakaenda Ramoth-Gileadi.
30 And the king of Israel said unto Jehoshaphat: 'I will disguise myself, and go into the battle; but put thou on thy robes.' And the king of Israel disguised himself, and went into the battle.
Mfalme wa Israeli akamwambia Yehoshafati, “Nitaingia vitani nikiwa nimejibadilisha, lakini wewe uvae majoho yako ya kifalme.” Kwa hiyo mfalme wa Israeli akajibadilisha na kwenda vitani.
31 Now the king of Aram had commanded the thirty and two captains of his chariots, saying: 'Fight neither with small nor great, save only with the king of Israel.'
Wakati huu, mfalme wa Aramu alikuwa amewaagiza majemadari thelathini na wawili wa magari ya vita, “Msipigane na yeyote, mdogo au mkubwa, isipokuwa mfalme wa Israeli.”
32 And it came to pass, when the captains of the chariots saw Jehoshaphat, that they said: 'Surely it is the king of Israel'; and they turned aside to fight against him; and Jehoshaphat cried out.
Wakati wale majemadari wa magari ya vita walipomwona Yehoshafati wakafikiri, “Hakika huyu ndiye mfalme wa Israeli.” Kwa hiyo wakageuka ili wamshambulie, lakini Yehoshafati akapiga kelele,
33 And it came to pass, when the captains of the chariots saw that it was not the king of Israel, that they turned back from pursuing him.
wale majemadari wakaona kwamba hakuwa mfalme wa Israeli, nao wakaacha kumfuatilia.
34 And a certain man drew his bow at a venture, and smote the king of Israel between the lower armour and the breastplate; wherefore he said unto the driver of his chariot: 'Turn thy hand, and carry me out of the host; for I am sore wounded.'
Lakini mtu fulani akavuta upinde pasipo lengo na kumpiga mfalme wa Israeli katikati ya kiungio cha mavazi yake ya chuma. Mfalme akamwambia mwendesha gari lake, “Geuza gari na uniondoe mimi katika mapigano, nimejeruhiwa.”
35 And the battle increased that day; and the king was stayed up in his chariot against the Arameans, and died at even; and the blood ran out of the wound into the bottom of the chariot.
Vita vikaendelea mchana kutwa, naye Mfalme Ahabu akategemezwa ndani ya gari kuelekea Waaramu. Damu kutoka kwenye jeraha lake ikachuruzika ndani ya gari na jioni yake akafa.
36 And there went a cry throughout the host about the going down of the sun, saying: 'Every man to his city, and every man to his country.'
Jua lilipokuwa linazama, mbiu ikaenea katika jeshi lote: “Kila mtu aende mjini kwake, na kila mtu shambani kwake!”
37 So the king died, and was brought to Samaria; and they buried the king in Samaria.
Basi mfalme akafa na akaletwa Samaria, nao wakamzika huko.
38 And they washed the chariot by the pool of Samaria; and the dogs licked up his blood; the harlots also washed themselves there; according unto the word of the LORD which He spoke.
Wakasafisha lile gari la vita katika bwawa la Samaria (mahali makahaba walipooga), na mbwa wakaramba damu yake, sawasawa na neno la Bwana lilivyokuwa limesema.
39 Now the rest of the acts of Ahab, and all that he did, and the ivory house which he built, and all the cities that he built, are they not written in the book of the chronicles of the kings of Israel?
Kwa matukio mengine ya utawala wa Ahabu, pamoja na yote aliyoyafanya, jumba la kifalme alilojenga na kupambwa kwa pembe za ndovu, nayo miji aliyoijengea maboma, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Israeli?
40 So Ahab slept with his fathers; and Ahaziah his son reigned in his stead.
Ahabu akalala pamoja na baba zake. Naye Ahazia mwanawe akawa mfalme baada yake.
41 And Jehoshaphat the son of Asa began to reign over Judah in the fourth year of Ahab king of Israel.
Yehoshafati mwana wa Asa akawa mfalme wa Yuda katika mwaka wa nne wa Ahabu mfalme wa Israeli.
42 Jehoshaphat was thirty and five years old when he began to reign; and he reigned twenty and five years in Jerusalem. And his mother's name was Azubah the daughter of Shilhi.
Yehoshafati alikuwa na umri wa miaka thelathini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka ishirini na mitano. Jina la mama yake aliitwa Azuba binti Shilhi.
43 And he walked in all the way of Asa his father; he turned not aside from it, doing that which was right in the eyes of the LORD; howbeit the high places were not taken away; the people still sacrificed and offered in the high places.
Katika kila jambo alitembea katika njia za Asa baba yake wala hakwenda kinyume chake. Alifanya yaliyo mema machoni pa Bwana. Hata hivyo mahali pa juu pa kuabudia hapakuondolewa. Watu waliendelea kutoa kafara na kufukiza uvumba huko.
44 And Jehoshaphat made peace with the king of Israel.
Yehoshafati pia alikuwa na amani na mfalme wa Israeli.
45 Now the rest of the acts of Jehoshaphat, and his might that he showed, and how he warred, are they not written in the book of the chronicles of the kings of Judah?
Kwa habari ya matukio mengine ya utawala wa Yehoshafati, mafanikio aliyokuwa nayo na uhodari wake katika vita, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
46 And the remnant of the sodomites that remained in the days of his father Asa, he put away out of the land.
Aliondolea mbali katika nchi mahanithi wa mahali pa kuabudia miungu waliobaki huko hata baada ya utawala wa baba yake Asa.
47 And there was no king in Edom: a deputy was king.
Tangu hapo hapakuwepo na mfalme katika Edomu, naibu ndiye alitawala.
48 Jehoshaphat made ships of Tarshish to go to Ophir for gold; but they went not; for the ships were broken at Ezion-geber.
Wakati huu Yehoshafati akaunda merikebu nyingi za biashara ili kwenda Ofiri kuchukua dhahabu, lakini kamwe hazikusafiri, kwa maana zilivunjika huko Esion-Geberi.
49 Then said Ahaziah the son of Ahab unto Jehoshaphat: 'Let my servants go with thy servants in the ships.' But Jehoshaphat would not.
Wakati ule, Ahazia mwana wa Ahabu akamwambia Yehoshafati, “Waache watu wangu wasafiri baharini pamoja na watu wako,” lakini Yehoshafati akakataa.
50 And Jehoshaphat slept with his fathers, and was buried with his fathers in the city of David his father; and Jehoram his son reigned in his stead.
Kisha Yehoshafati akalala na baba zake, akazikwa pamoja nao katika mji wa Daudi baba yake. Mwanawe Yehoramu akawa mfalme baada yake.
51 Ahaziah the son of Ahab began to reign over Israel in Samaria in the seventeenth year of Jehoshaphat king of Judah, and he reigned two years over Israel.
Ahazia mwana wa Ahabu akawa mfalme wa Israeli huko Samaria katika mwaka wa kumi na saba wa Yehoshafati mfalme wa Yuda, naye alitawala katika Israeli kwa miaka miwili.
52 And he did that which was evil in the sight of the LORD, and walked in the way of his father, and in the way of his mother, and in the way of Jeroboam the son of Nebat, wherein he made Israel to sin.
Akafanya maovu machoni mwa Bwana kwa sababu alienenda katika njia za baba yake na mama yake na katika njia za Yeroboamu mwana wa Nebati, ambaye alisababisha Israeli itende dhambi.
53 And he served Baal, and worshipped him, and provoked the LORD, the God of Israel, according to all that his father had done.
Alimtumikia na kumwabudu Baali na kumghadhibisha Bwana, Mungu wa Israeli, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.

< 1 Kings 22 >