< 1 Chronicles 21 >

1 And Satan stood up against Israel, and moved David to number Israel.
Shetani akainuka dhidi ya Israeli na kumshawishi Daudi ahesabu watu wa Israeli.
2 And David said to Joab and to the princes of the people: 'Go, number Israel from Beersheba even to Dan; and bring me word, that I may know the sum of them.'
Kwa hiyo Daudi akamwambia Yoabu na majemadari wa jeshi, “Nendeni mkawahesabu Waisraeli kuanzia Beer-Sheba mpaka Dani. Kisha nileteeni taarifa ili kwamba niweze kufahamu wako wangapi.”
3 And Joab said: 'The LORD make His people a hundred times so many more as they are; but, my lord the king, are they not all my lord's servants? why doth my lord require this thing? why will he be a cause of guilt unto Israel?'
Yoabu akajibu, “Bwana na aongeze jeshi lake mara mia na zaidi. Mfalme bwana wangu, kwani hawa wote si raiya wa bwana wangu? Kwa nini bwana wangu unataka kufanya hivi? Kwa nini kuleta hatia juu ya Israeli?”
4 Nevertheless the king's word prevailed against Joab. Wherefore Joab departed and went throughout all Israel, and came to Jerusalem.
Hata hivyo, neno la mfalme likawa na nguvu juu ya Yoabu; kwa hiyo Yoabu akaondoka na kuzunguka Israeli yote kisha akarudi Yerusalemu.
5 And Joab gave up the sum of the numbering of the people unto David. And all they of Israel were a thousand thousand and a hundred thousand men that drew sword; and Judah was four hundred three-score and ten thousand men that drew sword.
Yoabu akampa Daudi jumla ya idadi ya watu wanaoweza kupigana. Katika Israeli kulikuwa na watu 1,100,000 ambao wangeweza kutumia upanga na katika Yuda watu 470,000.
6 But Levi and Benjamin he did not number among them; for the king's word was abominable to Joab.
Lakini Yoabu hakuwahesabu Walawi na Wabenyamini, kwa sababu alichukizwa sana na amri ya mfalme.
7 And God was displeased with this thing; therefore He smote Israel.
Amri hii ilikuwa mbaya machoni pa Mungu pia; hivyo akaiadhibu Israeli.
8 And David said unto God: 'I have sinned greatly, in that I have done this thing; but now, put away, I beseech Thee, the iniquity of Thy servant; for I have done very foolishly.'
Kisha Daudi akamwambia Mungu, “Nimetenda dhambi kubwa kwa kufanya jambo hili. Sasa, ninakusihi, ondoa hatia ya mtumishi wako. Nimefanya jambo la kipumbavu sana.”
9 And the LORD spoke unto Gad, David's seer, saying:
Bwana akamwambia Gadi, mwonaji wa Daudi,
10 'Go and speak unto David, saying: Thus saith the LORD: I offer thee three things; choose thee one of them, that I may do it unto thee.'
“Nenda ukamwambie Daudi, hivi ndivyo asemavyo Bwana: ‘Ninakupa wewe uchaguzi wa mambo matatu. Nichagulie mojawapo nitakalotenda dhidi yako.’”
11 So Gad came to David, and said unto him: 'Thus saith the LORD: Take which thou wilt:
Kwa hiyo Gadi akamwendea Daudi akamwambia, “Hili ndilo Bwana asemalo: ‘Chagua:
12 either three years of famine; or three months to be swept away before thy foes, while the sword of thine enemies overtaketh thee; or else three days the sword of the LORD, even pestilence in the land, and the angel of the LORD destroying throughout all the borders of Israel. Now therefore consider what answer I shall return to Him that sent me.'
miaka mitatu ya njaa, au miezi mitatu ya kushindwa na adui zako, ukipatwa na upanga wao, au siku tatu za upanga wa Bwana, yaani, siku tatu za tauni katika nchi na malaika wa Bwana akiangamiza kila mahali katika Israeli.’ Sasa basi, amua jinsi nitakavyomjibu yeye aliyenituma.”
13 And David said unto Gad: 'I am in a great strait; let me fall now into the hand of the LORD, for very great are His mercies; and let me not fall into the hand of man.'
Daudi akamwambia Gadi, “Ninayo mahangaiko makubwa. Mimi na nianguke mikononi mwa Bwana kwa maana rehema zake ni kuu mno, lakini usiniache niangukie mikononi mwa wanadamu.”
14 So the LORD sent a pestilence upon Israel; and there fell of Israel seventy thousand men.
Basi Bwana akatuma tauni katika Israeli, watu 70,000 wa Israeli wakafa.
15 And God sent an angel unto Jerusalem to destroy it; and as he was about to destroy, the LORD beheld, and He repented Him of the evil, and said to the destroying angel: 'It is enough; now stay thy hand.' And the angel of the LORD was standing by the threshing-floor of Ornan the Jebusite.
Mungu akapeleka malaika kuangamiza Yerusalemu. Lakini malaika alipokuwa akifanya hivyo, Bwana akaona na akahuzunika kwa sababu ya maafa, akamwambia yule malaika aliyekuwa anaangamiza watu, “Yatosha! Rudisha mkono wako.” Wakati huo malaika wa Bwana alikuwa amesimama katika sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
16 And David lifted up his eyes, and saw the angel of the LORD standing between the earth and the heaven, having a drawn sword in his hand stretched out over Jerusalem. Then David and the elders, clothed in sackcloth, fell upon their faces.
Daudi akayainua macho yake akamwona huyo malaika wa Bwana akiwa amesimama katikati ya mbingu na dunia, naye ameunyoosha upanga wake juu ya Yerusalemu tayari kuangamiza. Kisha Daudi na wazee, waliokuwa wamevaa nguo za gunia, wakaanguka kifudifudi.
17 And David said unto God: 'Is it not I that commanded the people to be numbered? even I it is that have sinned and done very wickedly; but these sheep, what have they done? let Thy hand, I pray Thee, O LORD my God, be against me, and against my father's house; but not against Thy people, that they should be plagued.'
Daudi akamwambia Mungu, “Je, si mimi ndiye niliyeamuru watu wahesabiwe? Mimi ndiye niliyetenda dhambi na kukosa. Hawa ni kondoo tu. Wamefanya nini? Ee Bwana, Mungu wangu, mkono wako na uwe juu yangu mimi na jamaa yangu, lakini usiache tauni hii iendelee juu ya watu wako.”
18 Then the angel of the LORD commanded Gad to say to David, that David should go up, and rear an altar unto the LORD in the threshing-floor of Ornan the Jebusite.
Kisha malaika wa Bwana akamwamuru Gadi amwambie Daudi apande na kumjengea Bwana madhabahu kwenye sakafu ya kupuria nafaka ya Arauna Myebusi.
19 And David went up at the saying of Gad, which he spoke in the name of the LORD.
Kwa hiyo Daudi akakwea, akalitii lile neno ambalo Gadi alikuwa amelisema katika jina la Bwana.
20 And Ornan turned back, and saw the angel; and his four sons that were with him hid themselves. Now Ornan was threshing wheat.
Arauna alipokuwa akipura ngano, akageuka akamwona yule malaika. Wanawe wanne waliokuwa pamoja naye wakajificha, yeye akaendelea kupura ngano.
21 And as David came to Ornan, Ornan looked and saw David, and went out of the threshing-floor, and bowed down to David with his face to the ground.
Kisha Daudi akakaribia, Arauna alipotazama na kumwona, akaondoka kwenye uwanja wa kupuria nafaka akamsujudia Daudi akiuinamisha uso wake ardhini.
22 Then David said to Ornan: 'Give me the place of this threshing-floor, that I may build thereon an altar unto the LORD; for the full price shalt thou give it me; that the plague may be stayed from the people.'
Daudi akamwambia, “Nipatie huu uwanja wako wa kupuria nafaka ili niweze kujenga madhabahu ya Bwana tauni ipate kukomeshwa katika watu. Niuzie kwa bei yake kamili.”
23 And Ornan said unto David: 'Take it to thee, and let my lord the king do that which is good in his eyes; lo, I give thee the oxen for burnt-offerings, and the threshing-instruments for wood, and the wheat for the meal-offering; I give it all'
Arauna akamwambia Daudi, “Uchukue huo uwanja. Mfalme bwana wangu na afanye lolote analopenda. Tazama, nitatoa maksai kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, vifaa vya kupuria kuwa kuni, pamoja na ngano kwa ajili ya dhabihu ya nafaka. Natoa hivi vyote.”
24 And king David said to Ornan: 'Nay, but I will verily buy it for the full price; for I will not take that which is thine for the LORD, nor offer a burnt-offering without cost.'
Lakini Mfalme Daudi akamjibu Arauna, “La hasha! Lakini ninasisitiza kwamba nitalipa bei yake kamili. Sitachukua kilicho chako kwa ajili ya Bwana au kutoa sadaka ya kuteketezwa ambayo hainigharimu chochote.”
25 So David gave to Ornan for the place six hundred shekels of gold by weight.
Basi Daudi akamlipa Arauna shekeli za dhahabu 600 kwa ajili ya ule uwanja.
26 And David built there an altar unto the LORD, and offered burnt-offerings and peace-offerings, and called upon the LORD; and He answered him from heaven by fire upon the altar of burnt-offering.
Kisha Daudi akamjengea Bwana madhabahu mahali hapo, na kutoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Akamwita Bwana naye Bwana akajibu maombi yake kwa moto toka mbinguni juu ya madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa.
27 And the LORD commanded the angel; and he put up his sword back into the sheath thereof.
Kisha Bwana akanena na yule malaika, naye akarudisha upanga wake katika ala yake.
28 At that time, when David saw that the LORD had answered him in the threshing-floor of Ornan the Jebusite, then he sacrificed there.
Wakati huo, Daudi alipoona kwamba Bwana amemjibu kule kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Arauna Myebusi, akatoa dhabihu huko.
29 For the tabernacle of the LORD, which Moses made in the wilderness, and the altar of burnt-offering, were at that time in the high place at Gibeon.
Maskani ya Bwana ambayo Mose aliitengeneza kule jangwani, pamoja na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa kwa wakati huo vilikuwa viko mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni.
30 But David could not go before it to inquire of God; for he was terrified because of the sword of the angel of the LORD.
Lakini Daudi hakuthubutu kuisogelea ili kumuuliza Mungu, kwa sababu aliuogopa upanga wa yule malaika wa Bwana.

< 1 Chronicles 21 >