< 1 Chronicles 16 >

1 And they brought in the ark of God, and set it in the midst of the tent that David had pitched for it, and they offered burnt-offerings and peace-offerings before God.
Wakaleta Sanduku la Mungu na kuliweka ndani ya hema ambalo Daudi alikuwa amelisimamisha kwa ajili yake, na wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani mbele za Mungu.
2 And when David had made an end of offering the burnt-offering and the peace-offerings, he blessed the people in the name of the LORD.
Baada ya Daudi kumaliza kutoa hizo sadaka za kuteketezwa na hizo sadaka za amani, akawabariki watu katika jina la Bwana.
3 And he dealt to every one of Israel, both man and woman, to every one a loaf of bread, and a cake made in a pan, and a sweet cake.
Kisha akamgawia kila Mwisraeli mwanaume na mwanamke mkate, andazi la tende na andazi la zabibu kavu.
4 And he appointed certain of the Levites to minister before the ark of the LORD, and to celebrate and to thank and praise the LORD, the God of Israel:
Akawaweka pia baadhi ya Walawi ili wahudumu mbele ya Sanduku la Bwana kufanya maombi, kumshukuru na kumsifu Bwana, Mungu wa Israeli:
5 Asaph the chief, and second to him Zechariah, Jeiel, and Shemiramoth, and Jehiel, and Mattithiah, and Eliab, and Benaiah, and Obed-edom, and Jeiel, with psalteries and with harps; and Asaph with cymbals, sounding aloud;
Asafu ndiye alikuwa mkuu wao, akisaidiwa na Zekaria, Yeieli, Shemiramothi, Yehieli, Matithia, Eliabu, Benaya, Obed-Edomu na Yeieli. Hawa ndio wangepiga zeze na vinubi, Asafu angepiga matoazi,
6 and Benaiah and Jahaziel the priests with trumpets continually, before the ark of the covenant of God.
nao Benaya na Yahazieli makuhani, ndio wangepiga tarumbeta mara kwa mara mbele ya Sanduku la Agano la Mungu.
7 Then on that day did David first ordain to give thanks unto the LORD, by the hand of Asaph and his brethren.
Siku ile, kitu cha kwanza Daudi alichofanya ni kumkabidhi Asafu na wenzake zaburi hii ya shukrani kwa Bwana:
8 O give thanks unto the LORD, call upon His name; make known His doings among the peoples.
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
9 Sing unto Him, sing praises unto Him; speak ye of all His marvellous works.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
10 Glory ye in His holy name; let the heart of them rejoice that seek the LORD.
Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
11 Seek ye the LORD and His strength; seek His face continually.
Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
12 Remember His marvellous works that He hath done, His wonders, and the judgments of His mouth;
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
13 O ye seed of Israel His servant, ye children of Jacob, His chosen ones.
enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14 He is the LORD our God; His judgments are in all the earth.
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
15 Remember His covenant for ever, the word which He commanded to a thousand generations;
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
16 The covenant which He made with Abraham, and His oath unto Isaac;
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
17 And He established it unto Jacob for a statute, to Israel for an everlasting covenant;
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
18 Saying: 'Unto thee will I give the land of Canaan, the lot of your inheritance.'
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
19 When ye were but a few men in number, yea, very few, and sojourners in it,
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
20 And when they went about from nation to nation, and from one kingdom to another people,
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
21 He suffered no man to do them wrong, yea, for their sake He reproved kings:
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
22 'Touch not Mine anointed ones, and do My prophets no harm.'
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
23 Sing unto the LORD, all the earth; proclaim His salvation from day to day.
Mwimbieni Bwana dunia yote; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.
24 Declare His glory among the nations, His marvellous works among all the peoples.
Tangazeni utukufu wake katikati ya mataifa, matendo yake ya ajabu miongoni mwa mataifa yote.
25 For great is the LORD, and highly to be praised; He also is to be feared above all gods.
Kwa kuwa Bwana ni mkuu, mwenye kustahili kusifiwa kuliko wote; yeye ni wa kuogopwa kuliko miungu yote.
26 For all the gods of the peoples are things of nought; but the LORD made the heavens.
Kwa maana miungu yote ya mataifa ni sanamu, lakini Bwana aliziumba mbingu.
27 Honour and majesty are before Him; strength and gladness are in His place.
Fahari na enzi viko mbele yake; nguvu na utukufu vimo patakatifu pake.
28 Ascribe unto the LORD, ye kindreds of the peoples, ascribe unto the LORD glory and strength.
Mpeni Bwana, enyi jamaa za mataifa, mpeni Bwana utukufu na nguvu,
29 Ascribe unto the LORD the glory due unto His name; bring an offering, and come before Him; worship the LORD in the beauty of holiness.
mpeni Bwana utukufu unaostahili jina lake. Leteni sadaka na mje katika nyua zake; mwabuduni Bwana katika uzuri wa utakatifu wake.
30 Tremble before Him, all the earth; the world also is established that it cannot be moved.
Dunia yote na itetemeke mbele zake! Ulimwengu ameuweka imara; hauwezi kusogezwa.
31 Let the heavens be glad, and let the earth rejoice; and let them say among the nations: 'The LORD reigneth.'
Mbingu na zishangilie, nchi na ifurahi; semeni katikati ya mataifa, “Bwana anatawala!”
32 Let the sea roar, and the fulness thereof; let the field exult, and all that is therein;
Bahari na ivume, na vyote vilivyomo ndani yake; mashamba na yashangilie, na vyote vilivyomo ndani yake.
33 Then shall the trees of the wood sing for joy, before the LORD, for He is come to judge the earth.
Kisha miti ya msituni itaimba, itaimba kwa furaha mbele za Bwana, kwa maana anakuja kuihukumu dunia.
34 O give thanks unto the LORD; for He is good; for His mercy endureth for ever.
Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema; upendo wake wadumu milele.
35 And say ye: 'Save us, O God of our salvation, and gather us together and deliver us from the nations, that we may give thanks unto Thy holy name, that we may triumph in Thy praise.'
Mlilieni, “Ee Mungu Mwokozi wetu, tuokoe. Tukusanye tena na utukomboe kutoka kwa mataifa, ili tuweze kulishukuru jina lako takatifu, na kushangilia katika sifa zako.”
36 Blessed be the LORD, the God of Israel, from everlasting even to everlasting. And all the people said: 'Amen,' and praised the LORD.
Atukuzwe Bwana, Mungu wa Israeli, tangu milele na hata milele. Nao watu wote wakasema, “Amen,” na “Msifuni Bwana.”
37 So he left there, before the ark of the covenant of the LORD, Asaph and his brethren, to minister before the ark continually, as every day's work required;
Daudi akamwacha Asafu na wenzake mbele ya Sanduku la Agano la Bwana ili wahudumu humo mara kwa mara, kulingana na mahitaji ya kila siku.
38 and Obed-edom with their brethren, threescore and eight; Obed-edom also the son of Jedithun and Hosah to be door-keepers;
Pia akamwacha Obed-Edomu pamoja na wenzake sitini na wanane wahudumu pamoja nao. Obed-Edomu mwana wa Yeduthuni na pia Hosa walikuwa mabawabu wa lango.
39 and Zadok the priest, and his brethren the priests, before the tabernacle of the LORD in the high place that was at Gibeon,
Daudi akamwacha kuhani Sadoki pamoja na makuhani wenzake mbele ya hema ya ibada ya Bwana katika mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni
40 to offer burnt-offerings unto the LORD upon the altar of burnt-offering continually morning and evening, even according to all that is written in the Law of the LORD, which He commanded unto Israel;
ili kutoa sadaka za kuteketezwa kwa Bwana kwenye madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa mara kwa mara, asubuhi na jioni, sawasawa na kila kitu kilichoandikwa katika sheria ya Bwana ambayo alikuwa amempa Israeli.
41 and with them Heman and Jeduthun, and the rest that were chosen, who were mentioned by name, to give thanks to the LORD, because His mercy endureth for ever;
Waliohudumu pamoja nao walikuwa Hemani, Yeduthuni na wale wote waliochaguliwa na kutajwa kwa jina kumpa Bwana shukrani, “Kwa maana fadhili zake zadumu milele.”
42 and with them Heman and Jeduthun, to sound aloud with trumpets and cymbals, and with instruments for the songs of God; and the sons of Jeduthun to be at the gate.
Hemani na Yeduthuni walikuwa na wajibu wa kupiga tarumbeta, matoazi na kutumia vyombo vingine kwa ajili ya nyimbo za sifa kwa Mungu. Wana wa Yeduthuni waliwekwa langoni.
43 And all the people departed every man to his house; and David returned to bless his house.
Kisha watu wote wakaondoka, kila mmoja akarudi nyumbani kwake, naye Daudi akarudi nyumbani kuibariki jamaa yake.

< 1 Chronicles 16 >