< 1 Chronicles 13 >

1 And David consulted with the captains of thousands and of hundreds, even with every leader.
Daudi alishauriana na kila afisa wake, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia.
2 And David said unto all the assembly of Israel: 'If it seem good unto you, and if it be of the LORD our God, let us send abroad everywhere unto our brethren that are left in all the land of Israel, and with them to the priests and Levites that are in their cities that have open land about them, that they may gather themselves unto us;
Ndipo Daudi akaliambia kusanyiko lote la Israeli, “Kama mkiona ni vyema, na kama ni mapenzi ya Bwana Mungu wetu, tupeleke ujumbe kwa ndugu zetu wengine walio mbali na walio karibu katika nchi yote ya Israeli, pia kwa makuhani na Walawi walio pamoja nao katika miji yao na katika sehemu zao za malisho yao, waje waungane na sisi.
3 and let us bring back the ark of our God to us; for we sought not unto it in the days of Saul.'
Sisi na tulirudishe Sanduku la Mungu wetu kwetu kwa maana hatukujali wakati wa utawala wa Sauli.”
4 And all the assembly said that they would do so; for the thing was right in the eyes of all the people.
Kusanyiko lote likakubaliana kufanya hivyo, kwa sababu ilionekana vyema kwa watu wote.
5 So David assembled all Israel together, from Shihor the brook of Egypt even unto the entrance of Hamath, to bring the ark of God from Kiriath-jearim.
Basi Daudi akawakusanya Waisraeli wote, kuanzia Mto Shihori ulioko Misri hadi Lebo-Hamathi, ili kulileta Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu.
6 And David went up, and all Israel, to Baalah, that is, to Kiriath-jearim, which belonged to Judah, to bring up from thence the ark of God, the LORD that sitteth upon the cherubim, whereon is called the Name.
Daudi akiwa pamoja na Waisraeli wote wakaenda Baala ya Yuda (yaani Kiriath-Yearimu) kulipandisha Sanduku la Mungu Bwana, yeye anayeketi katika kiti cha enzi kati ya makerubi: Sanduku linaloitwa kwa Jina lake, kutoka huko.
7 And they set the ark of God upon a new cart, and brought it out of the house of Abinadab; and Uzza and Ahio drove the cart.
Wakalisafirisha Sanduku la Mungu kwa gari jipya la kukokotwa na maksai kutoka nyumba ya Abinadabu, Uza na Ahio wakiliongoza gari hilo.
8 And David and all Israel played before God with all their might; even with songs, and with harps, and with psalteries, and with timbrels, and with cymbals, and with trumpets.
Daudi pamoja na Waisraeli wote walikuwa wanasifu kwa nguvu zao zote mbele za Mungu, kwa nyimbo na kwa vinubi, zeze, matari, matoazi na tarumbeta.
9 And when they came unto the threshing-floor of Chidon, Uzza put forth his hand to hold the ark; for the oxen stumbled.
Walipofika kwenye uwanja wa kupuria nafaka wa Kidoni, Uza akaunyoosha mkono wake ili kulizuia Sanduku, kwa sababu maksai walijikwaa.
10 And the anger of the LORD was kindled against Uzza, and He smote him, because he put forth his hand to the ark; and there he died before God.
Hasira ya Bwana ikawaka dhidi ya Uza, akampiga kwa sababu aliuweka mkono wake kwenye Sanduku. Kwa hiyo akafa pale mbele za Mungu.
11 And David was displeased, because the LORD had broken forth upon Uzza; and that place was called Perez-uzza unto this day.
Ndipo Daudi akakasirika kwa sababu ghadhabu ya Bwana ilifurika dhidi ya Uza, mahali pale pakaitwa Peres-Uza hadi leo.
12 And David was afraid of God that day, saying: 'How shall I bring the ark of God home to me?'
Siku ile Daudi akamwogopa Mungu naye akauliza. “Nitawezaje kulichukua Sanduku la Mungu kwangu?”
13 So David removed not the ark unto him into the city of David, but carried it aside into the house of Obed-edom the Gittite.
Hakulichukua hilo Sanduku akae nalo katika Mji wa Daudi. Badala yake, akalipeleka nyumbani kwa Obed-Edomu, Mgiti.
14 And the ark of God remained with the family of Obed-edom in his house three months; and the LORD blessed the house of Obed-edom, and all that he had.
Sanduku la Mungu likabaki pamoja na jamaa ya Obed-Edomu, nyumbani kwake kwa miezi mitatu, naye Bwana akaibariki nyumba yake pamoja na kila kitu alichokuwa nacho.

< 1 Chronicles 13 >