< Luke 3 >

1 NOW in the fifteenth year of the reign of Tiberius Caesar, Pontius Pilate being governor of Judea, and Herod tetrarch of Galilee, and Philip his brother tetrarch of Iturea and the region of Trachonitis, and Lysanias tetrarch of Abilene:
Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato akiwa mtawala wa Uyahudi, Herode akiwa mfalme wa Galilaya, Filipo ndugu yake akiwa mfalme wa Iturea na nchi ya Trakoniti, na Lisania akiwa mfalme wa Abilene,
2 when Annas and Caiaphas were high-priests, the word of God came to John the son of Zacharias in the wilderness;
nao Anasi na Kayafa wakiwa makuhani wakuu, neno la Mungu likamjia Yohana, mwana wa Zekaria huko jangwani.
3 and he came into all the country on the confines of Jordan, preaching the baptism of repentance for the remission of sins;
Akaenda katika nchi yote kandokando ya Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi.
4 as it is written in the book of the words of the prophet Isaiah, saying, “The voice of one crying in the wilderness, Prepare ye the way of the Lord, make his paths strait:
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu aliaye nyikani, ‘Itengenezeni njia ya Bwana, yanyoosheni mapito yake.
5 every valley shall be filled up, and every mountain and hill shall be levelled, and the crooked ways made strait, and the rough roads smooth:
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitashushwa. Njia zilizopinda zitanyooshwa, na zilizoparuza zitasawazishwa.
6 and all flesh shall see the salvation of God.”
Nao watu wote watauona wokovu wa Mungu.’”
7 He said, therefore, to the multitudes who came out to be baptised by him, Ye broods of vipers, who hath warned you to fly from the approaching wrath?
Yohana akauambia ule umati wa watu uliokuwa unakuja ili kubatizwa naye, “Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
8 Produce then fruits worthy of repentance, and begin not to say in yourselves, We have a father, even Abraham; for I say unto you, That God is able out of these stones to raise up children to Abraham.
Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. Wala msianze kusema mioyoni mwenu kuwa, ‘Sisi tunaye Abrahamu, baba yetu.’ Kwa maana nawaambia kuwa Mungu anaweza kumwinulia Abrahamu watoto kutoka mawe haya.
9 But now is the ax laid even to the root of the trees; every tree therefore that produceth not good fruit, is cut down and cast into the fire.
Hata sasa shoka limeshawekwa tayari kwenye shina la kila mti. Basi kila mti usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa motoni.”
10 And the multitudes asked him, saying, What then shall we do?
Ule umati wa watu ukamuuliza, “Inatupasa tufanyeje basi?”
11 And he answering said to them, He that hath two coats, let him give to him that hath none; and he that hath provisions, let him do in like manner.
Yohana akawaambia, “Aliye na kanzu mbili amgawie asiye nayo, naye aliye na chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 Then came also the farmers of the taxes to be baptised, and they said unto him, Master, what shall we do?
Watoza ushuru nao wakaja ili wabatizwe, wakamuuliza, “Bwana na sisi inatupasa tufanyeje?”
13 He said unto them, Exact nothing more than is appointed for you.
Akawaambia, “Msichukue zaidi ya kiwango mlichopangiwa.”
14 And the military men also asked him, And what shall we do? And he said unto them, Extort nothing by force; nor turn informers; and be content with your pay.
Askari nao wakamuuliza, “Je, nasi inatupasa tufanye nini?” Akawaambia, “Msimdhulumu mtu wala msimshtaki mtu kwa uongo, bali mridhike na mishahara yenu.”
15 Now when the people were in expectation, and many reasoned in their hearts respecting John, whether he were the Messiah,
Watu walikuwa na matazamio makubwa. Wakawa wanajiuliza mioyoni mwao iwapo Yohana angeweza kuwa ndiye Kristo.
16 John addressed himself to them all, saying, I indeed baptise you with water; but one mightier than I is coming, the thong of whose sandals I am not worthy to untie: he shall baptise you with the Holy Ghost and with fire;
Yohana akawajibu akawaambia, “Mimi nawabatiza kwa maji. Lakini atakuja aliye na nguvu kuniliko mimi, ambaye sistahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 whose winnowing fan is in his hand, and he will thoroughly cleanse his threshing-floor, and collect the wheat into his granary; but the chaff he will burn with fire unquenchable.
Pepeto lake liko mkononi, tayari kusafisha sakafu yake ya kupuria na kuikusanya ngano ghalani, lakini makapi atayateketeza kwa moto usiozimika.”
18 Thus in many and various discourses exhorting them, he preached the glad tidings of the gospel to the people.
Basi, kwa maonyo mengine mengi Yohana aliwasihi na kuwahubiria watu Habari Njema.
19 Now Herod the tetrarch, being reproved by him, on account of Herodias his brother Philip’s wife, and for all the other wicked actions which he had done,
Lakini Yohana alipomkemea Mfalme Herode kuhusu uhusiano wake na Herodia, mke wa ndugu yake, na maovu mengine aliyokuwa amefanya,
20 added this also to all the rest, and shut up John in prison.
Herode aliongezea jambo hili kwa hayo mengine yote: alimfunga Yohana gerezani.
21 Now it came to pass, at the time when John was baptising all the people, that Jesus also was baptised, and as he prayed, the heaven was opened,
Baada ya watu wote kubatizwa, Yesu naye akabatizwa. Naye alipokuwa akiomba, mbingu zilifunguka.
22 and the Holy Ghost descended in a bodily form, like a dove, upon him, and a voice came from heaven, saying, Thou art my beloved Son, in thee I am well pleased.
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa umbo kama la hua, nayo sauti kutoka mbinguni ikasema: “Wewe ni Mwanangu mpendwa; nami nimependezwa nawe sana.”
23 And Jesus himself was about thirty years of age when he began his ministry, being (as was supposed the son of Joseph) of Heli,
Yesu alikuwa na umri wa miaka thelathini alipoanza huduma yake. Alikuwa akidhaniwa kuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Eli,
24 of Matthat, of Levi, of Melchi, of Janna, of Joseph,
Eli alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi, Lawi alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Yanai, Yanai alikuwa mwana wa Yosefu,
25 of Mattathias, of Amos, of Naum, of Esli, of Nagge,
Yosefu alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Amosi, Amosi alikuwa mwana wa Nahumu, Nahumu alikuwa mwana wa Esli, Esli alikuwa mwana wa Nagai,
26 of Maath, of Mattathias, of Semei, of Joseph, of Juda,
Nagai alikuwa mwana wa Maathi, Maathi alikuwa mwana wa Matathia, Matathia alikuwa mwana wa Semeini, Semeini alikuwa mwana wa Yoseki, Yoseki alikuwa mwana wa Yoda,
27 of Joanna, of Rhesa, of Zerubbabel, of Salathiel, of Neri,
Yoda alikuwa mwana wa Yoanani, Yoanani alikuwa mwana wa Resa, Resa alikuwa mwana wa Zerubabeli, Zerubabeli alikuwa mwana wa Shealtieli, Shealtieli alikuwa mwana wa Neri,
28 of Melchi, of Addi, of Cosam, of Elmodam, of Er,
Neri alikuwa mwana wa Melki, Melki alikuwa mwana wa Adi, Adi alikuwa mwana wa Kosamu, Kosamu alikuwa mwana wa Elmadamu, Elmadamu alikuwa mwana wa Eri,
29 of Jose, of Eliezer, of Jorim, of Matthat, of Levi,
Eri alikuwa mwana wa Yoshua, Yoshua alikuwa mwana wa Eliezeri, Eliezeri alikuwa mwana wa Yorimu, Yorimu alikuwa mwana wa Mathati, Mathati alikuwa mwana wa Lawi,
30 of Simeon, of Judah, of Joseph, of Jonan, of Eliakim,
Lawi alikuwa mwana wa Simeoni, Simeoni alikuwa mwana wa Yuda, Yuda alikuwa mwana wa Yosefu, Yosefu alikuwa mwana wa Yonamu, Yonamu alikuwa mwana wa Eliakimu, Eliakimu alikuwa mwana wa Melea,
31 of Melea, of Menan, of Mattatha, of Nathan, of David,
Melea alikuwa mwana wa Mena, Mena alikuwa mwana wa Matatha, Matatha alikuwa mwana wa Nathani, Nathani alikuwa mwana wa Daudi,
32 of Jesse, of Obed, of Booz, of Salmon, of Naasson,
Daudi alikuwa mwana wa Yese, Yese alikuwa mwana wa Obedi, Obedi alikuwa mwana wa Boazi, Boazi alikuwa mwana wa Salmoni, Salmoni alikuwa mwana wa Nashoni,
33 of Aminadab, of Aram, of Esrom, of Phares, of Judah,
Nashoni alikuwa mwana wa Aminadabu, Aminadabu alikuwa mwana wa Aramu, Aramu alikuwa mwana wa Hesroni, Hesroni alikuwa mwana wa Peresi, Peresi alikuwa mwana wa Yuda,
34 of Jacob, of Isaac, of Abraham, of Terah, of Nachor,
Yuda alikuwa mwana wa Yakobo, Yakobo alikuwa mwana wa Isaki, Isaki alikuwa mwana wa Abrahamu, Abrahamu alikuwa mwana wa Tera, Tera alikuwa mwana wa Nahori,
35 of Saruch, of Ragau, of Phalec, of Heber, of Sala,
Nahori alikuwa mwana wa Serugi, Serugi alikuwa mwana wa Reu, Reu alikuwa mwana wa Pelegi, Pelegi alikuwa mwana wa Eberi, Eberi alikuwa mwana wa Sala,
36 of Cainan, of Arphaxad, of Sem, of Noe, of Lamech,
Sala alikuwa mwana wa Kenani, Kenani alikuwa mwana wa Arfaksadi, Arfaksadi alikuwa mwana wa Shemu, Shemu alikuwa mwana wa Noa, Noa alikuwa mwana wa Lameki,
37 of Methusaleh, of Enoch, of Jared, of Maleleel, of Cainan,
Lameki alikuwa mwana wa Methusela, Methusela alikuwa mwana wa Enoki, Enoki alikuwa mwana wa Yaredi, Yaredi alikuwa mwana wa Mahalaleli, Mahalaleli alikuwa mwana wa Kenani,
38 of Enos, of Seth, of Adam, the son of God.
Kenani alikuwa mwana wa Enoshi, Enoshi alikuwa mwana wa Sethi, Sethi alikuwa mwana wa Adamu, Adamu alikuwa mwana wa Mungu.

< Luke 3 >