< Luke 3 >

1 And in the fifteenth year in the reign of Tiberius Caesar, Pontius Pilate being governor of Judea, and Herod being tetrarch of Galilee, and Philip his brother, tetrarch of Ituria and the Trachonitis country, and Lusanius tetrarch of Abilene, during the high-priesthood of Annas
Sasa, katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberia, wakati Pontio Pilato alikuwa gavana wa Uyahudi, Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo ndugu yake alikuwa mkuu wa mkoa wa Iturea na Trakoniti, na Lisania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
2 and Caiaphas, the word of God came to John the son of Zacharias in the wilderness.
na wakati wa ukuhani mkuu wa Anasi na Kayafa, Neno la Mungu lilimjia Yohana mwana wa Zakaria, jangwani.
3 And he came into all the region round about the Jordan preaching the baptism of repentance unto the remissions of sins,
Alisafiri katika mkoa wote kuzunguka Mto Yordani, akihubiri ubatizo wa toba kwa ajili ya msamaha wa dhambi
4 as has been written in the book of Isaiah the prophet, saying; The voice of one roaring in the wilderness; Prepare ye the way of the Lord, make straight His paths.
Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha maneno ya Isaya nabii, “sauti ya mtu aliaye nyikani, “Itengenezeni tayari njia ya Bwana, yatengenezeni mapito yake yaliyoonyoka.
5 Every valley shall be filled up and every mountain and hill shall be cut down; and the crooked places shall be straight and the rough ways smooth.
Kila bonde litajazwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa, barabara zilizopinda zitanyoshwa, na njia zilizoparaza zitalainishwa.
6 And all flesh shall see the salvation of God.
Watu wote watauona wokovu wa Mungu.”
7 Then he said unto the multitudes coming out to be baptized by him; O generations of vipers, who hath warned you to flee from the wrath to come?
Hivyo, Yohana akawaambia makutano makubwa ya watu waliomjia wapate kubatizwa na yeye, “Ninyi uzao wa nyoka wenye sumu, nani aliwaonya kuikimbia gadhabu inayokuja?
8 Bring forth therefore fruits worthy of repentance, and do not begin to say among yourselves; We have Abraham our father.
Zaeni matunda yanayoedana na toba, na msianze kusema ndani yenu, “Tunaye Ibarahimu ambaye ni baba yetu; kwa sababu nawaambia ya kwamba, Mungu anaweza kumwinulia Ibrahimu watoto hata kutokana na mawe haya.
9 But truly the ax is laid to the root of the trees; Therefore every tree not producing good fruit is hewn down, and cast into the fire.
Tayari shoka limeshawekwa kwenye mzizi wa miti. Hivyo, kila mti usiozaa matunda mema, hukatwa na kutupwa motoni.
10 And the multitudes asked him, saying; What then shall we do?
Kisha watu katika makutano walimuuliza wakisema, “Sasa tunatakiwa tufanyeje?”
11 And responding he says to them, Let the one having two coats, give to him having none, and let the one having food do likewise.
Alijibu na kuwaambia, “kama mtu ana kanzu mbili anatakiwa atoe kanzu moja kwa mwingine ambaye hana kabisa, na ambaye ana chakula na afanye vivyo hivyo.”
12 And the publicans came also to be baptized, and said to him; Teacher, what shall we do!
Kisha baadhi ya watoza ushuru walikuja pia kubatizwa, na wakamwambia, “Mwalimu, tunatakiwa kufanya nini?
13 And he said to them, Exact no more than that which has been appointed unto you.
Akawaambia, “Msikusanye fedha zaidi kuliko mnachotakiwa kukusanya.”
14 And the soldiers were asking him saying; And what shall we do? And he said to them; Oppress no one, neither defraud; and be content with your wages.
Baadhi ya maaskari pia wakamuuliza wakisema, “Na sisi je? Tunatakiwa tufanye nini?” Akawambia, “Msichukue fedha kwa mtu yeyote kwa nguvu, na msimtuhumu mtu yeyote kwa uongo. Ridhikeni na mishahara yenu.”
15 And the people waiting and all reasoning in their hearts concerning John, lest he might be the Christ.
Sasa, kwa kuwa watu walikuwa na shauku ya kumngojea Kristo atakaye kuja, kila mmoja alikuwa anawaza moyoni mwake kuhusu Yohana kama yeye ndiye Kristo.
16 John responded to all, saying; I indeed baptize you with water; but there cometh One more powerful than I, the latchet of His sandals I am not worthy to loose; He will baptize you with the Holy Ghost and fire.
Yohana akajibu kwa kuwaambia wote, “Mimi nawabatiza ninyi kwa maji, lakini kuna mmoja ajaye ambaye ana nguvu kuliko mimi, na sisitahili hata kufungua kamba za viatu vyake. Atawabatiza ninyi kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
17 Whose fan is in His hand, and He will thoroughly purify His threshing-floor, and gather the wheat into His garner, and will burn up the chaff with unquenchable fire.
Pepeto lake liko mkononi mwake ili kusafisha vizuri uwanda wake wa kupepetea ngano na kuikusanya ngano ghalani mwake. Lakini, atayateketeza makapi kwa moto ambao hauwezi kuzimika.
18 Then indeed exhorting them as to many other things he continued to preach the gospel to the people.
Kwa maonyo mengine mengi pia, alihubiri habari njema kwa watu.
19 And Herod the tetrarch, being convicted by him concerning Herodias, the wife of his brother Philip, and concerning the wickedness which Herod did,
Yohana alimkemea pia Herode mkuu wa mkoa kwa kumuoa Herodia, mke wa ndugu yake na kwa maovu mengine mengi ambayo Herode alikuwa ameyatenda.
20 added also this to all, and shut up John in prison.
Lakini baadaye Herode alifanya uovu mwingine mbaya sana. Alimfunga Yohana gerezani.
21 And it came to pass while all the people were being baptized, and Jesus having been baptized, and praying, the heaven was opened,
Kisha ilitokea kwamba, wakati watu wote walipokuwa wakibatizwa na Yohana, naye Yesu alibatizwa pia. Wakati alipokuwa akiomba, mbingu zikafunguka.
22 and the Holy Spirit in bodily appearance like a dove descended on Him; and there was a voice from heaven, saying; Thou art my beloved Son, I am delighted in Thee.
Roho Mtakatifu akashuka juu yake kwa mfano wa kiwiliwili kama njiwa, wakati huo huo sauti ikaja kutoka mbinguni ikisema, “Wewe ni Mwanangu mpendwa. Ninapendezwa sana na wewe.”
23 And Jesus was beginning to be about thirty years old, being as was supposed, the son of Joseph, the son of Eli,
Sasa Yesu mwenyewe, alipoanza kufundisha, alikuwa na umri upatao miaka thelathini. Alikuwa ni mwana (kama ilivyotadhaniwa) wa Yusufu, mwana wa Eli,
24 Matthat, Levi, Melchi, Janna, Joseph:
mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yana, mwana wa Yusufu,
25 Mattathios, Amos, Naum, Esli, Naggai,
mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Esli, mwana wa Nagai,
26 Mattathios, Semei, Josech, Joda,
mwana wa Maati, mwana wa Matathia, mwana wa Semeini, mwana wa Yusufu, mwana wa Yuda,
27 Joanna, Resa, Zorababbel, Salithiel, Neri,
mwana wa Yoanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
28 Melchi, Addi, Cosam, Elmodam, Er,
mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
29 Joses, Eliezer, Jorim, Matthat, Levi,
mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Matathi, mwana wa Lawi,
30 Simeon, Judah, Joseph, Jonan, Eliakim,
mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yusufu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliyakimu,
31 Melea, Mainan, Mattatha, Nathan, David,
mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
32 Jesse, Obed, Booz, Salmon, Naasson,
mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
33 Aminadab, Aram, Esrom, Phares, Judah,
mwana wa Abinadabu, mwana wa Aramu, mwana wa Hesroni, mwana wa Peresi, mwana wa Yuda,
34 Jacob, Isaac, Abraham, Thara, Nachor, Serouch, Ragau,
mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Ibrahimu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
35 Phalek, Heber, Sala,
mwana wa Seruig, mwana wa Ragau, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
36 Cainan, Arphaxad, Shem, Noah, Lamech,
mwana wa Kenani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Nuhu, mwana wa Lameki,
37 of Methusalah, Enoch, Jared, of Mahalaleel, Cainan,
mwana wa Methusela, mwana wa Henoko, mwana wa Yaredi, mwana Mahalalei, mwana wa Kenani,
38 of Enos, Seth, Adam, the Son of God.
mwana wa Enoshi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, mwana wa Mungu.

< Luke 3 >