< Zechariah 3 >

1 And he shewed mee Iehoshua the hie Priest, standing before the Angel of the Lord, and Satan stoode at his right hand to resist him.
Kisha akanionyesha Yoshua, kuhani mkuu, akiwa amesimama mbele ya malaika wa Bwana, naye Shetani amesimama upande wake wa kuume ili amshtaki.
2 And the Lord said vnto Satan, The Lord reprooue thee, O Satan: euen the Lord that hath chosen Ierusalem, reprooue thee. Is not this a brand taken out of the fire?
Bwana akamwambia Shetani, “Bwana akukemee Shetani! Bwana, ambaye ameichagua Yerusalemu, akukemee! Je, mtu huyu siyo kijinga kinachowaka kilichonyakuliwa kwenye moto?”
3 Nowe Iehoshua was clothed with filthie garments, and stoode before the Angel.
Wakati huu, Yoshua alikuwa amevaa nguo chafu alipokuwa amesimama mbele ya malaika.
4 And he answered and spake vnto those that stoode before him, saying, Take away the filthie garments from him. And vnto him hee saide, Behold, I haue caused thine iniquitie to depart from thee, and I wil clothe thee with change of raiment.
Malaika akawaambia wale waliokuwa wamesimama mbele yake, “Mvueni hizo nguo zake chafu.” Kisha akamwambia Yoshua, “Tazama, nimeiondoa dhambi yako, nami nitakuvika mavazi ya kitajiri.”
5 And I saide, Let them set a faire diademe vpon his head. So they set a faire diademe vpon his head, and clothed him with garments, and the Angel of the Lord stoode by.
Kisha nikasema, “Mvike kilemba kilicho safi kichwani mwake.” Kwa hiyo wakamvika kilemba safi kichwani na kumvika yale mavazi mengine, wakati malaika wa Bwana akiwa amesimama karibu.
6 And the Angel of the Lord testified vnto Iehoshua, saying,
Malaika wa Bwana akamwamuru Yoshua:
7 Thus saith the Lord of hostes, If thou wilt walke in my wayes, and keepe my watch, thou shalt also iudge mine House, and shalt also keepe my courtes, and I will giue thee place among these that stand by.
“Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: ‘Ikiwa utakwenda katika njia zangu na kushika masharti yangu, basi utaitawala nyumba yangu na kuwa na amri juu ya nyua zangu, nami nitakupa nafasi miongoni mwa hawa wasimamao hapa.
8 Heare now, O Iehoshua the hie Priest, thou and thy fellowes that sit before thee: for they are monstruous persons: but behold, I wil bring forth the Branche my seruant.
“‘Sikiliza, ee Yoshua kuhani mkuu, pamoja na wenzako walioketi mbele yako, ambao ni watu walio ishara ya mambo yatakayokuja: Ninakwenda kumleta mtumishi wangu, Tawi.
9 For loe, the stone that I haue layd before Iehoshua: vpon one stone shalbe seuen eyes: beholde, I will cut out the grauing thereof, saith the Lord of hostes, and I will take away the iniquitie of this land in one day.
Tazama, jiwe nililoliweka mbele ya Yoshua! Kuna macho saba juu ya jiwe lile moja, nami nitachora maandishi juu yake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote, ‘nami nitaiondoa dhambi ya nchi hii kwa siku moja.
10 In that day, saith the Lord of hostes, shall ye call euery man his neighbour vnder the vine, and vnder the figge tree.
“‘Katika siku hiyo kila mmoja wenu atamwalika jirani yake akae chini ya mzabibu wake na mtini wake,’ asema Bwana Mwenye Nguvu Zote.”

< Zechariah 3 >