< Ruth 1 >

1 In the time that the Iudges ruled, there was a dearth in the lande, and a man of Beth-lehem Iudah went for to soiourne in the countrey of Moab, he, and his wife, and his two sonnes.
Ilitokea katika siku za utawala wa majaji kuwa kulikuwa na njaa katika nchi, na mtu mmoja wa Bethelehemu ya Yuda alikwenda katika nchi ya Moabu pamoja na mke wake na watoto wake walili wa kiume.
2 And the name of the man was Elimelech, and the name of his wife, Naomi: and the names of his two sonnes, Mahlon, and Chilion, Ephrathites of Beth-lehem Iudah: and when they came into the land of Moab, they continued there.
Jina la mtu huyo lilikuwa Elimeleki, na jina la mke wake lilikuwa Naomi. Majina ya watoto wake wawili wa kiume waliitwa Mahiloni na Kileoni, ambao walikuwa Waefraimu wa Betherehemu ya Yuda. Waliwasili katika nchi ya Moabu na kuishi hapo.
3 Then Elimelech the husband of Naomi died, and she remayned with her two sonnes,
Ndipo Elimeleki, mume wa Naomi, alikufa, na Naomi aliachwa na watoto wake wa kiume wawili.
4 Which tooke them wiues of the Moabites: the ones name was Orpah, and the name of ye other Ruth: and they dwelled there about ten yeeres.
Watoto hawa walioa wanawake wa Moabu; jina la mmoja lilikuwa Oripa, na jina la mwingine lilikuwa Ruth. waliishi huko kwa takribani miaka kumi.
5 And Mahlon and Chilion dyed also both twaine: so the woman was left destitute of her two sonnes, and of her husband.
Kisha wote Mahiloni na Kileoni walikufa, na kumuacha Naomi bila mme wake na bila watoto wake wawili.
6 Then she arose with her daughters in law, and returned from the countrey of Moab: for she had heard say in the countrey of Moab, that the Lord had visited his people, and giuen them bread.
Ndipo Naomi aliamua kuondoka Moabu pamoja na wake wa watoto wake na kurudi Yuda kwa sababu alikuwa amesikia katika mkoa wa Moabu kuwa Yahweh amewasaidia watu wake katika uhitaji na amewapa chakula.
7 Wherefore shee departed out of the place where she was, and her two daughters in law with her, and they went on their way to returne vnto the land of Iudah.
Hivyo aliondoka sehemu aliyokuwa pamoja na wake wa watoto wake wawili, walitelemka njia kurudi kwenye nchi ya Yuda.
8 Then Naomi saide vnto her two daughters in lawe, Goe, returne eche of you vnto her owne mothers house: the Lord shew fauour vnto you, as ye haue done with the dead, and with me.
Naomi aliwaambia wake wa watoto wake, “Nendeni, mrudi, kila mmoja wenu, kwenye nyumba ya mama yake. na Mungu aonyeshe wema juu yenu, kama mlivyo onyesha wema kwao waliokufa na kwangu.
9 The Lord graunt you, that you may finde rest, either of you in the house of her husband. And when she kissed them, they lift vp their voice and wept.
Mungu awajalie ninyi kupata pumziko, kila mmoja wenu katika nyumba ya mme mwingine.” Kisha akawabusu, na wakapaza sauti zao na kulia.
10 And they saide vnto her, Surely we will returne with thee vnto thy people.
Wakamwambia, “Hapana! tutarudi pamoja na wewe kwa watu wako.”
11 But Naomi saide, Turne againe, my daughters: for what cause will you go with me? are there any more sonnes in my wombe, that they may bee your husbands?
Lakini Naomi alisema, “Rudini, wanangu! Kwa nini mtakwenda na mimi? Kwani bado nina watoto katika tumbo langu kwa ajili yenu, ili kwamba waje wawe waume zenu?
12 Turne againe, my daughters: go your way: for I am too olde to haue an husband. If I should say, I haue hope, and if I had an husband this night: yea, if I had borne sonnes,
Rudini, wanangu, nendeni katika njia zenu wenyewe, kwa kuwa mimi ni mzee sana kuwa na mme. Kama nikisema, 'Natumaini nipate mume usiku huu,' na kisha kuzaa watoto wakiume, kwa hiyo mnaweza kusubiri mpaka wakue?
13 Would yee tarie for them, till they were of age? would ye be deferred for them from taking of husbands? nay my daughters: for it grieueth me much for your sakes that the hand of the Lord is gone out against me.
Mtasubiri na msiolewe sasa? Hapana, wanangu! Ina nihuzunisha zaidi, kuliko inavyo wahuzunisha ninyi, kwa sababu mkono wa Yahweh umeenda kinyume na mimi.”
14 Then they lift vp their voyce and wept againe, and Orpah kissed her mother in lawe, but Ruth abode still with her.
Ndipo wake wa watoto wake wakapaza sauti zao na kulia tena. Oripa alimuaga kwa kumbusu, lakini Ruth aliendelea kubaki naye.
15 And Naomi said, Beholde, thy sister in law is gone backe vnto her people and vnto her gods: returne thou after thy sister in lawe.
Naomi alisema, “sikiliza, mwenzako amerudi kwa watu wake na miungu yake. Ruri pamoja naye.”
16 And Ruth answered, Intreate mee not to leaue thee, nor to depart from thee: for whither thou goest, I will goe: and where thou dwellest, I will dwell: thy people shall be my people, and thy God my God.
lakini Ruth alisema, “Usiniache niondoke mbali nawe, kwa kuwa uendako, nitakwenda, utakapoishi, nitaishi; watu wako watakuwa watu wangu, na Mungu wako atakuwa Mungu wangu.
17 Where thou diest, will I die, and there will I be buried. the Lord do so to me and more also, if ought but death depart thee and me.
Mahali utakapofia, nitafia hapo, na hapo nitazikwa. Yahweh aniwezeshe, na hata zaidi, ikiwa kuna chochote isipokuwa kifo kamwe hakiwezi kututenganisha.
18 Whe she saw that she was stedfastly minded to go with her, she left speaking vnto her.
Naomi alipoona kuwa Ruth alikuwa ameamua kwenda naye, aliacha kubishana naye.
19 So they went both vntill they came to Beth-lehem: and when they were come to Beth-lehem, it was noysed of them through all the citie, and they said, Is not this Naomi?
Hivyo wote wawili walisafiri mpaka walipofika mjini Bethelehemu. Kwa hiyo walipofika Bethlehemu, mji wote uliwafurahia, wanawake walisema, “Huyu ni Naomi?”
20 And she answered them, Call me not Naomi, but call me Mara: for the Almightie hath giuen me much bitternes.
Lakini aliwaambia, “Msiniite Naomi. Niiteni Mchungu, kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitenda mambo machungu sana.
21 I went out full, and the Lord hath caused me to returne emptie: why call ye me Naomi, seeing the Lord hath humbled me, and the Almightie hath brought me vnto aduersitie?
Nilikwenda nikiwa nimejaa, lakini Yahweh kanirudisha nyumbani nikiwa sina wote. Hivyo kwa nini mnaniita Naomi, wakati mnaona Yahweh amenihukumu, kuwa Mwenyezi Mungu amenitaabisha?”
22 So Naomi returned and Ruth the Moabitesse her daughter in law with her, when she came out of the countrey of Moab: and they came to Beth-lehem in the beginning of barly haruest.
Kwa hivyo Naomi na Ruth Mmoabu, mke wa mtoto wake, walirudi kutoka nchi ya Moabu. walirudi Bethrehemu mwazo wa mavuno ya shairi.

< Ruth 1 >