< Romans 8 >

1 Now then there is no condemnation to them that are in Christ Iesus, which walke not after the flesh, but after the Spirit.
Kwa hiyo, sasa hakuna hukumu ya adhabu kwa wale walio ndani ya Kristo Yesu, wale ambao hawaenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho.
2 For the Lawe of the Spirite of life, which is in Christ Iesus, hath freed mee from the lawe of sinne and of death.
Kwa sababu sheria ya Roho wa uzima katika Kristo Yesu imeniweka huru mbali na sheria ya dhambi na mauti.
3 For (that that was impossible to ye Lawe, in as much as it was weake, because of ye flesh) God sending his owne Sonne, in ye similitude of sinful flesh, and for sinne, condened sinne in the flesh,
Kwa maana kile ambacho sheria haikuwa na uwezo wa kufanya, kwa vile ilivyokuwa dhaifu katika mwili, Mungu kwa kumtuma Mwanawe mwenyewe kwa mfano wa mwanadamu mwenye mwili ulio wa dhambi na kwa ajili ya dhambi, yeye aliihukumu dhambi katika mwili,
4 That that righteousnes of the Law might be fulfilled in vs, which walke not after ye flesh, but after the Spirit.
ili kwamba haki ipatikanayo kwa sheria itimizwe ndani yetu sisi, ambao hatuenendi kwa kuufuata mwili bali kwa kufuata Roho.
5 For they that are after the flesh, sauour the things of the flesh: but they that are after the Spirit, the things of the Spirit.
Kwa maana wale wanaoishi kwa kuufuata mwili huziweka nia zao katika vitu vya mwili, lakini wale wanaoishi kwa kufuata Roho, huziweka nia zao katika mambo ya Roho.
6 For the wisedome of the flesh is death: but the wisedome of the Spirit is life and peace,
Kwa maana kuwa na nia ya mwili ni mauti, bali kuwa na nia inayoongozwa na Roho ni uzima na amani.
7 Because the wisedome of the flesh is enimitie against God: for it is not subiect to the Lawe of God, neither in deede can be.
Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui na Mungu, kwa maana haiitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii.
8 So then they that are in the flesh, can not please God.
Wale wanaotawaliwa na mwili, hawawezi kumpendeza Mungu.
9 Now ye are not in the flesh, but in ye Spirit, because ye spirit of God dwelleth in you: but if any man hath not ye Spirit of Christ, ye same is not his.
Lakini ninyi, hamtawaliwi na mwili, bali na Roho, ikiwa Roho wa Mungu anakaa ndani yenu. Mtu yeyote ambaye hana Roho wa Kristo, yeye si wa Kristo.
10 And if Christ bee in you, the body is dead, because of sinne: but the Spirite is life for righteousnesse sake.
Lakini kama Kristo anakaa ndani yenu, miili yenu imekufa kwa sababu ya dhambi, lakini roho zenu zi hai kwa sababu ya haki.
11 But if the Spirit of him that raised vp Iesus from the dead, dwell in you, he that raised vp Christ from the dead, shall also quicken your mortall bodies, by his Spirit that dwelleth in you.
Nanyi ikiwa Roho wa Mungu aliyemfufua Yesu kutoka kwa wafu anakaa ndani yenu, yeye aliyemfufua Kristo Yesu kutoka kwa wafu ataihuisha pia miili yenu ambayo hufa, kwa njia ya Roho wake akaaye ndani yenu.
12 Therefore brethren, wee are detters not to the flesh, to liue after the flesh:
Kwa hiyo ndugu zangu, sisi tu wadeni, si wa mwili, ili tuishi kwa kuufuata mwili,
13 For if ye liue after the flesh, ye shall die: but if yee mortifie the deedes of the body by the Spirit, ye shall liue.
kwa maana mkiishi kwa kuufuata mwili, mtakufa, lakini kama mkiyaua matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.
14 For as many as are ledde by the Spirit of God, they are the sonnes of God.
Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio watoto wa Mungu.
15 For ye haue not receiued the Spirit of bodage, to feare againe: but ye haue receiued the Spirit of adoption, whereby we cry Abba, Father.
Kwa maana hamkupokea roho ya utumwa iwaleteayo tena hofu, bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambaye kwa yeye twalia, “Abba, yaani, Baba,”
16 The same Spirit beareth witnesse with our spirit, that we are the children of God.
Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu ya kwamba sisi tu watoto wa Mungu.
17 If we be children, we are also heires, euen the heires of God, and heires annexed with Christ: if so be that we suffer with him, that we may also be glorified with him.
Hivyo, ikiwa sisi ni watoto, basi tu warithi, warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo, naam, tukiteswa pamoja naye tupate pia kutukuzwa pamoja naye.
18 For I count that the afflictions of this present time are not worthy of the glory, which shalbe shewed vnto vs.
Nayahesabu mateso yetu ya wakati huu kuwa si kitu kulinganisha na utukufu utakaodhihirishwa kwetu.
19 For the feruent desire of the creature waiteth when the sonnes of God shalbe reueiled,
Kwa maana viumbe vyote vinangoja kwa shauku kudhihirishwa kwa watoto wa Mungu.
20 Because the creature is subiect to vanitie, not of it owne will, but by reason of him, which hath subdued it vnder hope,
Kwa kuwa viumbe vyote viliwekwa chini ya ubatili, si kwa chaguo lao, bali kwa mapenzi yake yeye aliyevitiisha katika tumaini,
21 Because the creature also shall be deliuered from the bondage of corruption into the glorious libertie of the sonnes of God.
ili kwamba viumbe vyote vipate kuwekwa huru kutoka kwa utumwa wa kuharibika na kupewa uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu.
22 For we knowe that euery creature groneth with vs also, and trauaileth in paine together vnto this present.
Kwa maana twajua ya kuwa hata sasa viumbe vyote vimekuwa vikilia kwa maumivu kama utungu wa mwanamke wakati wa kuzaa.
23 And not onely the creature, but we also which haue the first fruites of the Spirit, euen we doe sigh in our selues, waiting for the adoption, euen the redemption of our body.
Wala si hivyo viumbe peke yao, bali hata sisi ambao ndio matunda ya kwanza ya Roho, kwa ndani tunalia kwa uchungu tukisubiri kwa shauku kufanywa wana wa Mungu, yaani, ukombozi wa miili yetu.
24 For we are saued by hope: but hope that is seene, is not hope: for how can a man hope for that which he seeth?
Kwa kuwa tuliokolewa kwa tumaini hili. Lakini kama kinachotumainiwa kikionekana hakiwi tumaini tena. Je, kuna mtu anayetumaini kupata kitu alicho nacho tayari?
25 But if we hope for that we see not, we doe with patience abide for it.
Lakini tunapotumaini kupata kitu ambacho hatuna, basi twakingojea kwa saburi.
26 Likewise the Spirit also helpeth our infirmities: for we knowe not what to pray as wee ought: but the Spirit it selfe maketh request for vs with sighs, which cannot be expressed.
Vivyo hivyo, Roho hutusaidia katika udhaifu wetu, kwa sababu hatujui kuomba ipasavyo. Lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa uchungu usioweza kutamkwa.
27 But he that searcheth the heartes, knoweth what is the meaning of the Spirit: for he maketh request for ye Saints, according to the wil of God.
Naye Mungu aichunguzaye mioyo, anaijua nia ya Roho, kwa sababu Roho huwaombea watakatifu sawasawa na mapenzi ya Mungu.
28 Also we knowe that all thinges worke together for the best vnto them that loue God, euen to them that are called of his purpose.
Nasi tunajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hutenda kazi pamoja na wote wampendao, katika kuwapatia mema, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake.
29 For those which hee knewe before, he also predestinate to bee made like to the image of his Sonne, that hee might be the first borne among many brethren.
Maana wale Mungu aliowajua tangu mwanzo, pia aliwachagua tangu mwanzo, wapate kufanana na mfano wa Mwanawe, ili yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi.
30 Moreouer whom he predestinate, them also he called, and whom he called, them also he iustified, and whom he iustified, them he also glorified.
Nao wale Mungu aliotangulia kuwachagua, akawaita, wale aliowaita pia akawahesabia haki, nao wale aliowahesabia haki, pia akawatukuza.
31 What shall we then say to these thinges? If God be on our side, who can be against vs?
Tuseme nini basi kuhusu haya? Ikiwa Mungu yuko upande wetu, ni nani awezaye kuwa kinyume chetu?
32 Who spared not his owne Sonne, but gaue him for vs all to death, how shall he not with him giue vs all things also?
Ikiwa Mungu hakumhurumia Mwanawe, bali alimtoa kwa ajili yetu sote, atakosaje basi kutupatia vitu vyote kwa ukarimu pamoja naye?
33 Who shall lay any thing to the charge of Gods chosen? it is God that iustifieth,
Ni nani atakayewashtaki wale ambao Mungu amewateua? Ni Mungu mwenyewe ndiye mwenye kuwahesabia haki.
34 Who shall condemne? it is Christ which is dead, yea, or rather, which is risen againe, who is also at the right hand of God, and maketh request also for vs.
Ni nani basi atakayewahukumia adhabu? Kristo Yesu aliyekufa, naam, zaidi ya hayo, aliyefufuliwa kutoka kwa wafu, yuko mkono wa kuume wa Mungu, naye pia anatuombea.
35 Who shall separate vs from the loue of Christ? shall tribulation or anguish, or persecution, or famine, or nakednesse, or perill, or sworde?
Ni nani atakayetutenga na upendo wa Kristo? Je, ni shida au taabu au mateso au njaa au uchi au hatari au upanga?
36 As it is written, For thy sake are we killed all day long: we are counted as sheepe for the slaughter.
Kama ilivyoandikwa: “Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa; tumehesabiwa kama kondoo wa kuchinjwa.”
37 Neuerthelesse, in all these thinges we are more then coquerours through him that loued vs.
Lakini katika mambo haya yote tunashinda, naam na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.
38 For I am perswaded that neither death, nor life, nor Angels, nor principalities, nor powers, nor things present, nor things to come,
Kwa maana nimekwisha kujua kwa hakika ya kuwa sio mauti, wala uzima, wala malaika, wala wenye mamlaka, wala yaliyopo, wala yatakayokuja, wala wenye uwezo,
39 Nor height, nor depth, nor any other creature shalbe able to separate vs from the loue of God, which is in Christ Iesus our Lord.
wala yaliyo juu, wala yaliyo chini, wala kiumbe kingine chochote zitaweza kututenga na upendo wa Mungu ulio katika Kristo Yesu, Bwana wetu.

< Romans 8 >