< Revelation 7 >

1 And after that, I sawe foure Angels stand on the foure corners of the earth, holding the foure windes of the earth, that the winds should not blow on the earth, neither on the sea, neither on any tree.
Baada ya hili nikaona malaika wanne wakiwa wamesimama katika pembe nne za dunia, wakizuia hizo pepo nne za dunia, ili kwamba pasiwe na upepo utakaovuma juu ya nchi au juu ya bahari au juu ya mti wowote.
2 And I sawe another Angel come vp from the East, which had the seale of the liuing God, and hee cried with a loud voice to the foure Angels to who power was giuen to hurt the earth, and the sea, saying,
Nikaona malaika mwingine akipanda kutoka mawio ya jua akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliokuwa wamepewa mamlaka ya kuidhuru nchi na bahari, akisema,
3 Hurt ye not the earth, neither the sea, neither the trees, til we haue sealed the seruants of our God in their foreheads.
“Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, hadi tuwe tumetia muhuri kwenye vipaji vya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.”
4 And I heard the number of them, which were sealed, and there were sealed an hundreth and foure and fourtie thousand of all the tribes of the children of Israel.
Ndipo nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: yaani 144,000 kutoka makabila yote ya Israeli.
5 Of the tribe of Iuda were sealed twelue thousande. Of the tribe of Ruben were sealed twelue thousande. Of the tribe of Gad were sealed twelue thousande.
Kutoka kabila la Yuda 12,000 walitiwa muhuri, kutoka kabila la Reubeni 12,000, kutoka kabila la Gadi 12,000,
6 Of the tribe of Aser were sealed twelue thousand. Of the tribe of Nephthali were sealed twelue thousand. Of the tribe of Manasses were sealed twelue thousand.
kutoka kabila la Asheri 12,000, kutoka kabila la Naftali 12,000, kutoka kabila la Manase 12,000,
7 Of the tribe of Simeon were sealed twelue thousande. Of the tribe of Leui were sealed twelue thousande. Of the tribe of Issachar were sealed twelue thousand. Of the tribe of Zabulon were sealed twelue thousand.
kutoka kabila la Simeoni 12,000, kutoka kabila la Lawi 12,000, kutoka kabila la Isakari 12,000,
8 Of the tribe of Ioseph were sealed twelue thousande. Of the tribe of Beniamin were sealed twelue thousand.
kutoka kabila la Zabuloni 12,000, kutoka kabila la Yosefu 12,000, na kutoka kabila la Benyamini 12,000.
9 After these thinges I behelde, and loe a great multitude, which no man coulde number, of all nations and kindreds, and people, and tongues, stoode before the throne, and before the Lambe, clothed with long white robes, and palmes in their hands.
Baada ya hili nikatazama na hapo mbele yangu palikuwa na umati mkubwa wa watu ambao hakuna yeyote awezaye kuuhesabu, kutoka kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wakiwa wameshika matawi ya mitende mikononi mwao.
10 And they cried with a loud voice, saying, Saluation commeth of our God, that sitteth vpon the throne, and of the Lambe.
Nao walikuwa wakipiga kelele kwa sauti kubwa wakisema: “Wokovu una Mungu wetu, yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo!”
11 And all the Angels stoode rounde about the throne, and about the Elders, and the foure beastes, and they fell before the throne on their faces, and worshipped God,
Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha enzi na wale wazee ishirini na wanne na wale viumbe wanne wenye uhai. Wakaanguka kifudifudi mbele ya hicho kiti cha enzi na kumwabudu Mungu,
12 Saying, Amen. Praise, and glorie, and wisdom, and thankes, and honour, and power, and might bee vnto our God for euermore, Amen. (aiōn g165)
wakisema: “Amen! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele. Amen!” (aiōn g165)
13 And one of the Elders spake, saying vnto me, What are these which are araied in log white robes? and whence came they?
Kisha mmoja wa wale wazee ishirini na wanne akaniuliza, “Ni nani hawa waliovaa mavazi meupe, nao wametoka wapi?”
14 And I saide vnto him, Lord, thou knowest. And he saide to me, These are they, which came out of great tribulation, and haue washed their long robes, and haue made their long robes white in the blood of the Lambe.
Nikamjibu, “Bwana, wewe wajua.” Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu, nao wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo na kuyafanya meupe kabisa.
15 Therefore are they in the presence of the throne of God, and serue him day and night in his Temple, and he that sitteth on the throne, wil dwell among them.
Kwa hiyo, “Wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kumtumikia usiku na mchana katika hekalu lake; naye aketiye katika kile kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao.
16 They shall hunger no more, neither thirst any more, neither shall the sunne light on them, neither any heate.
Kamwe hawataona njaa wala kiu tena. Jua halitawapiga wala joto lolote liunguzalo.
17 For the Lambe, which is in the middes of the throne, shall gouerne them, and shall leade them vnto the liuely fountaines of waters, and God shall wipe away all teares from their eyes.
Kwa maana Mwana-Kondoo aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi atakuwa Mchungaji wao; naye atawaongoza kwenda kwenye chemchemi za maji yaliyo hai. Naye Mungu atafuta kila chozi kutoka macho yao.”

< Revelation 7 >