< Psalms 52 >

1 To him that excelleth. A Psalme of Dauid to giue instruction. When Doeg the Edomite came and shewed Saul, and saide to him, Dauid is come to the house of Abimelech. Why boastest thou thy selfe in thy wickednesse, O man of power? the louing kindenesse of God indureth dayly.
Kwa nini wewe unajivunia kufanya uovu, wewe mtu mwenye nguvu? Uaminifu wa agano la Mungu huja kila siku.
2 Thy tongue imagineth mischiefe, and is like a sharpe rasor, that cutteth deceitfully.
Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
3 Thou doest loue euill more then good, and lies more then to speake the trueth. (Selah)
Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. (Selah)
4 Thou louest all wordes that may destroye, O deceitfull tongue!
Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
5 So shall God destroy thee for euer: he shall take thee and plucke thee out of thy tabernacle, and roote thee out of ye land of the liuing. (Selah)
Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. (Selah)
6 The righteous also shall see it, and feare, and shall laugh at him, saying,
Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
7 Beholde the man that tooke not God for his strength, but trusted vnto the multitude of his riches, and put his strength in his malice.
“Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
8 But I shall bee like a greene oliue tree in the house of God: for I trusted in the mercie of God for euer and euer.
Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
9 I will alway praise thee, for that thou hast done this, and I will hope in thy Name, because it is good before thy Saints.
Nitakushukuru wewe daima kwa uliyo tenda. Nitalisubiri jina lako, kwa sababu ni zuri, uweponi mwa wantu wako wa kimungu.

< Psalms 52 >