< Psalms 3 >

1 A Psalme of Dauid, when he fled from his sonne Absalom. Lord, howe are mine aduersaries increased? howe many rise against me?
Yahewh, maadui zangu wako wangapi! Ni wengi wamekuja kinyume na mimi.
2 Many say to my soule, There is no helpe for him in God. (Selah)
Ni wengi wanaonisema, “Hakuna msaada wowote kutoka kwa Mungu kwa ajili yake.” (Selah)
3 But thou Lord art a buckler for me: my glory, and the lifter vp of mine head.
Bali wewe, Yahweh, u ngao yangu pande zote, utukufu wangu, na uniinuaye kichwa changu.
4 I did call vnto the Lord with my voyce, and he heard me out of his holy mountaine. (Selah)
Nampazia Yahweh sauti yangu, na yeye ananijibu kutoka katika mlima wake mtakatifu.
5 I layed me downe and slept, and rose vp againe: for the Lord susteined me.
Nilijilaza chini na kusinzia; na niliamka, kwa kuwa Yahweh alinilinda.
6 I will not be afrayde for ten thousand of the people, that should beset me round about.
Sitaogopa kusanyiko la watu ambao wamejipanga kinyume na mimi pande zote.
7 O Lord, arise: helpe me, my God: for thou hast smitten all mine enemies vpon the cheeke bone: thou hast broken the teeth of the wicked.
Inuka, Yahweh! Uniokoe, Mungu wangu! Kwa kuwa utawapiga maadui zangu wote kwenye taya zao; utayavunja meno ya waovu.
8 Saluation belongeth vnto the Lord, and thy blessing is vpon thy people. (Selah)
Wokovu unatoka kwa Yahweh. Baraka zako ziwe juu ya watu wako.

< Psalms 3 >