< Psalms 142 >

1 A Psalme of David, to give instruction, and a prayer, when he was in the cave. I cryed vnto the Lord with my voyce: with my voyce I prayed vnto the Lord.
Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi. Namlilia Bwana kwa sauti, nainua sauti yangu kwa Bwana anihurumie.
2 I powred out my meditation before him, and declared mine affliction in his presence.
Namimina malalamiko yangu mbele zake, mbele zake naeleza shida zangu.
3 Though my spirit was in perplexitie in me, yet thou knewest my path: in the way wherein I walked, haue they priuily layde a snare for me.
Wakati roho yangu inapozimia ndani yangu, wewe ndiwe unajua njia zangu. Katika njia ninayopita watu wameniwekea mtego.
4 I looked vpon my right hand, and beheld, but there was none that would knowe me: all refuge failed me, and none cared for my soule.
Tazama kuume kwangu na uone, hakuna hata mmoja anayejihusisha nami. Sina kimbilio, hakuna anayejali maisha yangu.
5 Then cryed I vnto thee, O Lord, and sayde, thou art mine hope, and my portion in the land of the liuing.
Ee Bwana, nakulilia wewe, nasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.”
6 Hearken vnto my crye, for I am brought very lowe: deliuer me from my persecuters, for they are too strong for me.
Sikiliza kilio changu, kwa sababu mimi ni mhitaji sana; niokoe na wale wanaonifuatilia, kwa kuwa wamenizidi nguvu.
7 Bring my soule out of prison, that I may prayse thy Name: then shall the righteous come about me, when thou art beneficiall vnto me.
Nifungue kutoka kifungo changu, ili niweze kulisifu jina lako. Ndipo wenye haki watanizunguka, kwa sababu ya wema wako kwangu.

< Psalms 142 >