< Psalms 108 >

1 A song or Psalme of David. O God, mine heart is prepared, so is my tongue: I will sing and giue praise.
Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2 Awake viole and harpe: I will awake early.
Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
3 I will praise thee, O Lord, among the people, and I wil sing vnto thee among the nations.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
4 For thy mercy is great aboue the heauens, and thy trueth vnto the clouds.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
5 Exalt thy self, O God, aboue the heauens, and let thy glorie be vpon all the earth,
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 That thy beloued may be deliuered: helpe with thy right hand and heare me.
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
7 God hath spoken in his holinesse: therefore I will reioyce, I shall deuide Shechem and measure the valley of Succoth.
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
8 Gilead shalbe mine, and Manasseh shalbe mine: Ephraim also shalbe the strength of mine head: Iuda is my lawgiuer.
Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
9 Moab shalbe my washpot: ouer Edom wil I cast out my shoe: vpon Palestina wil I triumph.
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
10 Who will leade mee into the strong citie? who will bring me vnto Edom?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
11 Wilt not thou, O God, which haddest forsaken vs, and diddest not goe foorth, O God, with our armies?
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
12 Giue vs helpe against trouble: for vaine is the helpe of man.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
13 Through God we shall doe valiantly: for he shall treade downe our enemies.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.

< Psalms 108 >